Monday, February 6, 2012

MWISHO WA KUTENDA,NI MAAMUZI.


Asichekwe yule atayetenda bila ya kujua  ni nini,ikiwa mtendaji anatakiwa kutenda zaidi ya vile bila ya yeye kujua mwenyewe..basi aachwe hivyo.Maana katenda,ya hivyo na yenyewe kaamua,na linalokuwa na msingi ni kuweza kuelewa pale vifanyikapo vitu,kwani na mara nyingine visieleweke,yaweza kuwa ni nusu au nzima iliyokuwepo katika matendo lakini msimamo wa jambo wenyewe umekuwa mgumu,mda mwingine kwa yale ya kiswahili huwa ni mazuri zaidi lakini yanaharibu yanapokuwa mengi,maamuzi ni zaidi ya mtu kutenda moja kwani yamekuwa mengi sasa,hapa tukatenda hivi na baadae kumalizia mengine,pale kwenye kumalizia si lazima yawe yalianza zamani mengine yakiwa ni marahisi,kama maamuzi yako yataamua kubaki,muda  hua ni kwenda mbele,kwani nao umeamua,tena shikilio la amuzi moja tu,la kwenda mbele.

Kipindi cha kujutia hakitakiwi endapo tu pale imetokea,kwani wengine hukaa kabisa na bila kuyakataza mawazo yao,kama mtoto anakatazwa kuchezea wembe ndio ije mtu mzima kwa mabovu?kama tutachukulia kila kitu kilivyo ndivyo kitakavyo kuwa kwani kilivyokuwa ndio kilikuwa kinaelekea hapo,hatua tusipoichukua ni tumetoa ruhusa kwani muda kazi yake ni lazima utumike,sio lazima wewe kwani ndiyo nani?alieutengeneza alikaa kila mda huohuo kuutengeneza,akijua itafika kipindi ataumaliza,tunapokimbilia kule tunamaana ya kuwepo huko,

Hatuwezi kuamua au kuacha wengine waende bila yetu kuamua tubaki,
Ijulikane hakuna wa kuishi maisha ya mwenzake,tofauti isiwe sababu ya kuishi tofauti,tena tusiamuliane,lile lililo la mmoja likafanyike katika yeye,maana mda utapita,sio tunahofia ingawaje hatulazimishi kuelewa ndio maana tukaamua tofauti,kuepuka ubishi na maamuzi yasiyo na msingi,ikiwa hatutaki ubishani usio na maana,maana itafika kipindi tuwaze vilivyopotea na wakati vizuri ndio hivyo vinajongea,ni ukaribu ambao katika moyo unaweza usikia,sio kama ule wa kunyata na miguu ukaishtukia,maana mda mwingine tusiseme tu maneno yasiyo na msingi,ikawe tutaelewana kila mmoja akawe na maana katika lake,akiwa katika mahala pake ndipo atakapofika.mahala pake pale alipo yeye kimawazo,akili na uhalisia wa mwili wake.

Ili matendo yapendeze ni kuna ulazima wa maamuzi sahihi kufanyika sasa,isiwe lazima kwa wale wachache,maana hao watakuja na kusema wanataka baadae,yule atakayebisha naomba nisiwe mimi kwani nitakuwa nje ya vile alivyoamua yeye,ikaja yeye au wewe umeamua jinsi vile nilivyogoma mwisho waweza kuwa mbali sana,kwani bado wengine tupo mwanzo na kinachosubirika hakieleweki kwani hatukueleweshwa kama haya ya muda huu yanahitaji maamuzi yake,wakiwa kama wao wanaogopa kutuambia kwani ni heli kumwacha nyani amalizie maembe katika mti kuliko kumshtua,maana mpaka kapanda aliyatafutia,

sijui nani amesikika akiakataza.eti yale walipasa kula wao,sijui walikuepo wapi maana muda wote mpaka yakaoza hawayakuona.binadamu tunalidhika na kile tunachokiona,wala hatunashida na kuridhika na kile tunachokitafuta,machache yawe ni majina na wala sio watu hapo tunaweza kupata hekima,maana tukijazana tutaonekana wazembe,ikiwa muda wote huo tulikuwa wapi?itakuwa zamu ya wengine bila ya kuamua,tuangalie kipindi maana huwa vinatofautiana dakika.

MAWAZO YASITUTENDESHE MAOVU, MDA MWINGINE MWANA ADAMU ANAPOKUWA HAJIELEWI.


By:          Benson G.  Makaya,

Tel:           +255714336657

Makaya's Forum: WATOTO WANAHITAJI KUINGIA KATIKA MATATIZO ILI KUJI...

Makaya's Forum: WATOTO WANAHITAJI KUINGIA KATIKA MATATIZO ILI KUJI...:  Matatizo ni sehemu ya maisha,matatizo ni sehemu ya yale magumu yaliyo machache yanayohitaji kufanyiwa marekebisho kupitia ya kwamba yameis...

WATOTO WANAHITAJI KUINGIA KATIKA MATATIZO ILI KUJIFUNZA JINSI YA KUTOKA KATIKA MATATIZO.


 Matatizo ni sehemu ya maisha,matatizo ni sehemu ya yale magumu yaliyo machache yanayohitaji kufanyiwa marekebisho kupitia ya kwamba yameisibu jamii au mtu binafsi katika ufanisi wa kufanya mambo fulani,matatizo huwa hayaangalii hali halisi ya mtu husika endapo atakuwa na uwezo nayo ama la,matatizo ni maswali yanayoijia jamii,kwa upande mmoja ama mwingine matatizo huwa hayakaribishwi kwani yanaweza kuja magumu zaidi.Wakubwa ndiyo watu wanaoeleweka kuwa na matatizo ndani ya maisha ya mwanadamu kutokana na kile kitu tunachoweza kusema wao ndiyo watafutaji wa maisha kama inavyoeleweka,na  matatizo yanaweza kuwepo ni kutokana na ugumu wa maisha katika mawazo ya klila mtu pale inapomtokea,tukitolea mbali ya kiafya,watoto wamekuwa wakihesabika kama ni watu wasio na maatatizo na hata kama wanayo  ni si kwamba utofauti wa ukubwa na udogo..

Yale yaliyopita ndiyo haya yanayokuja,kwani ifikapo kipindi cha ukubwa,mtoto hufanya kile alichofanya kipindi cha utoto,kubaki kuwa mtoto kwa sababu umri ni unasogea.Wakaona tofauti ambayo hao ndiyo uliowatendea,ikiwa nikiwa litaendelea kusemeka kwa muda wote na ukawa mwingi bila hata ya mageuzi hapo kuna uwalakini wa mafunzo kutokupatikana kwa mtoto na hata kuendelea kukua na tabia kama hizo.Tabia chafu humnyima furaha mtu mwanadamu,Yule anayetenda uchafu ni sawa na mtoto maana haelewi lolote,akiwa anaelewa na kufanya maksudi basi tunaweza kukaa mbali na huyo mtu,kwani mwishowe atatufanyia maksudi na sisi wenyewe.

Wakubwa wengi wanaelewa ni kwa sababu ya kupita kwingi pia,watoto wakafundishwe na wakubwa,ikiwa wakubwa wanaofundisha na wao hawana uelewa basi hapa kwa mtoto itasemeka vile ya namna 'umleavyo ndiyo vile atakavyokuwa',ikawe sio ni  makosa zaidi ya lawama,na hii huwa haiji kwa mzazi kwani 'chanda chema'..!,hata kama tunalifahamu hilo lakini hatujui la kufanya,kwani akili  inaweza kumfanya akafanya kitu kama ni mtoto ndiyo naye akatambue yake,maana matendo sio ya kuchaguliana,zaidi tutaumizana kwa dhana za kwenda katika vifungo vya maisha,hata kupelekea vifo bila hali kukaa sawa,maana vinakuja vizazi sasa,vizazi vinavyoelewa yale ya kwao,maana hata nimesema yale ya kuwa ni vigumu ya kuyafahamu.

Yanayotushinda ni ya kufikiri na sio kutumia 'nguvu',ikiwa hivi hata kabla ya kutenda tungelikuwa tunajifikiria na kama yangetokea basi yangekua na upungufu kidogo  wa makali,ingawa kila mtu ana matatizo yake na ule uchungu anaufahamu yeye muhusika,ni sawa na pale inapokuwa mbaya kwa mwenzako mwengine naye akapata kuchekelea,si ya kwamba tu ni rahisi bali ni yametokea katika upande ambao yeye haumuhusu,na hata kama ulipita vibaya wao watataka kujua hilo, mtoto anapokuwa haelewi ni haki kumrekebisha ikiwa nawe mzazi umeelewa jambo,mtoto anapofanya kitu sio kama mtu mzima,mtoto ni kama mashine,mara nyingine ikaende yenyewe itakavyo au vile mzazi akaendesha,ikiwa ni kwa pupa bila uhangalifu basi mali hiyo si ya kukaa muda mrefu,hakuna kinachodumu kwa mateso zaidi ya kuteseka.

Bila ya kusahau maisha ya mtu anayatengeneza mwenyewe,ikiwa kama vile tukajenga nyumba,kununua magari na kusema tumefanikiwa,tukiwa na msingi ulio bora,msingi wa maendeleo kutoka kwa jamii na wakubwa wengine,mtoto anapaswa kuelewa pale anapoelekezwa,mtoto mwenye kiburi na sio usikivu ni Yule aliyefundishwa hivyo,akazembewa na akakua,tabia ni kama samaki,haswaa samaki  aliyekauka ndiyo hatakiwi hata kukunjwa,maana atavunjika na baadaye kuwa hasara.

"Mali ni mali tu hata ikiwa mbovu ili mradi uwe na umiliki nayo".


By:            Benson G. Makaya,
Tel:             +255 714 33 66 57.
email:bensonsmakaya@gmail.com

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...