Monday, February 6, 2012

MWISHO WA KUTENDA,NI MAAMUZI.


Asichekwe yule atayetenda bila ya kujua  ni nini,ikiwa mtendaji anatakiwa kutenda zaidi ya vile bila ya yeye kujua mwenyewe..basi aachwe hivyo.Maana katenda,ya hivyo na yenyewe kaamua,na linalokuwa na msingi ni kuweza kuelewa pale vifanyikapo vitu,kwani na mara nyingine visieleweke,yaweza kuwa ni nusu au nzima iliyokuwepo katika matendo lakini msimamo wa jambo wenyewe umekuwa mgumu,mda mwingine kwa yale ya kiswahili huwa ni mazuri zaidi lakini yanaharibu yanapokuwa mengi,maamuzi ni zaidi ya mtu kutenda moja kwani yamekuwa mengi sasa,hapa tukatenda hivi na baadae kumalizia mengine,pale kwenye kumalizia si lazima yawe yalianza zamani mengine yakiwa ni marahisi,kama maamuzi yako yataamua kubaki,muda  hua ni kwenda mbele,kwani nao umeamua,tena shikilio la amuzi moja tu,la kwenda mbele.

Kipindi cha kujutia hakitakiwi endapo tu pale imetokea,kwani wengine hukaa kabisa na bila kuyakataza mawazo yao,kama mtoto anakatazwa kuchezea wembe ndio ije mtu mzima kwa mabovu?kama tutachukulia kila kitu kilivyo ndivyo kitakavyo kuwa kwani kilivyokuwa ndio kilikuwa kinaelekea hapo,hatua tusipoichukua ni tumetoa ruhusa kwani muda kazi yake ni lazima utumike,sio lazima wewe kwani ndiyo nani?alieutengeneza alikaa kila mda huohuo kuutengeneza,akijua itafika kipindi ataumaliza,tunapokimbilia kule tunamaana ya kuwepo huko,

Hatuwezi kuamua au kuacha wengine waende bila yetu kuamua tubaki,
Ijulikane hakuna wa kuishi maisha ya mwenzake,tofauti isiwe sababu ya kuishi tofauti,tena tusiamuliane,lile lililo la mmoja likafanyike katika yeye,maana mda utapita,sio tunahofia ingawaje hatulazimishi kuelewa ndio maana tukaamua tofauti,kuepuka ubishi na maamuzi yasiyo na msingi,ikiwa hatutaki ubishani usio na maana,maana itafika kipindi tuwaze vilivyopotea na wakati vizuri ndio hivyo vinajongea,ni ukaribu ambao katika moyo unaweza usikia,sio kama ule wa kunyata na miguu ukaishtukia,maana mda mwingine tusiseme tu maneno yasiyo na msingi,ikawe tutaelewana kila mmoja akawe na maana katika lake,akiwa katika mahala pake ndipo atakapofika.mahala pake pale alipo yeye kimawazo,akili na uhalisia wa mwili wake.

Ili matendo yapendeze ni kuna ulazima wa maamuzi sahihi kufanyika sasa,isiwe lazima kwa wale wachache,maana hao watakuja na kusema wanataka baadae,yule atakayebisha naomba nisiwe mimi kwani nitakuwa nje ya vile alivyoamua yeye,ikaja yeye au wewe umeamua jinsi vile nilivyogoma mwisho waweza kuwa mbali sana,kwani bado wengine tupo mwanzo na kinachosubirika hakieleweki kwani hatukueleweshwa kama haya ya muda huu yanahitaji maamuzi yake,wakiwa kama wao wanaogopa kutuambia kwani ni heli kumwacha nyani amalizie maembe katika mti kuliko kumshtua,maana mpaka kapanda aliyatafutia,

sijui nani amesikika akiakataza.eti yale walipasa kula wao,sijui walikuepo wapi maana muda wote mpaka yakaoza hawayakuona.binadamu tunalidhika na kile tunachokiona,wala hatunashida na kuridhika na kile tunachokitafuta,machache yawe ni majina na wala sio watu hapo tunaweza kupata hekima,maana tukijazana tutaonekana wazembe,ikiwa muda wote huo tulikuwa wapi?itakuwa zamu ya wengine bila ya kuamua,tuangalie kipindi maana huwa vinatofautiana dakika.

MAWAZO YASITUTENDESHE MAOVU, MDA MWINGINE MWANA ADAMU ANAPOKUWA HAJIELEWI.


By:          Benson G.  Makaya,

Tel:           +255714336657

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...