Wednesday, September 19, 2012

MIMI SI KITU

Maisha yangu yameniweka kuwa kitu cha muhimu katika maisha ya watu wegine,hii hainipeleki kuwa kitu cha maana katika vile vingine na la mtu huyo mwingine,nikiamini uzima hauji kwa mmoja pekee,ingawaje tumeumbwa na tukaamini basi kila mtu akashike hilo analoliamini,ona malengo na namna ya kuweza kuyafanikisha kwani yale mema yanakuwepo ndani yako,tena lazima ujue mafanikio ni namna unavyofurahi kwa vitu unavyoviona.,lakini ikiwa  furaha yako ni kuweza kuungana pamoja katika kusafiri ndani ya dunia,yaani maisha tunayoishi,na kila kitu ndani yake vikiwa si kitu zaidi yetu.
Mimi si kitu,lakini katika safari hii kamilifu kama sio uharibifu ndipo unaanza kutokea kwani kwa wengine kitu cha ukamilifu ni uharibifu upande wake,fikiri kwa isiyo kuwa nzuri ikapendeze maana si lazima iwe nzuri pengine hata ikatakikana sana,kama ingalikuwa safari yangu ni sawa na jaribu japo la kufanya kubadili yale yaliyo wekwa kwa kudhani pengine ni ya hatari,kwa muda uliopo mdanganyifu basi nina mengi ya kufanya,mengine nikiwa siyajui nikiomba kwa mwenyezi japo nguvu za kushindana kuwapenda maadui.
Kila kitu kipo sawa,kila kitu kina maana ya kuitwa kitu,kama vile ulivyo wewe kwa mzazi wako,nani ukamwita baba na mwengine ukamwita mama,hiyo yote ukiwa unajua kuwa dada siyo mama,sisi ni kitu kimoja mimi na wewe,tunaumia pamoja na ingawa tusipokuwa kitu pamoja.furaha ya safari inapatikana ndani ya safari,hivyo tumai la maisha  lina ulazima kulitupia maishani yakiwa ni maisha  yakiafrica,maisha yaliyojaa uasili na  na hisia
inayotia ukakamavu machoni,ikiwa na maana ya nguvu. .

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...