Friday, July 20, 2012

TABIA..

Leo ikiwa inatakiwa kujijua zaidi ya maana ya kujirudia,ingelikuwa ni mpya ningesema usihofu lakini haina maana ya kuingoja wakati ni bure muda unaenda,leo ndiyo siku ya kukwambia maana jana ilikuwa inaanza kujirudia,tena ikafahamike kwamba imerudi kwa ajili ya kuelewa,tena kufanya sahihi kwani ni tabia,tabia kila mtu anayo ya kwake,mwanzo ikaonekana ni makosa yaliyo na samahani kumbe hata wengine walikuwa wakitamani,si wanaujua ukweli,tena hakuna kubisha maana imejirudia. 

Unaweza kujaribu kuwa tofauti na ilivyo lakini mwishowe ni kukubali maelezo,tena ukahisi kuna usaidizi kwa kujulikana ni bahati mbaya lakini tabia yako imejulikana,maana ukionekana sijui ni vipi utasema haina maana,ya kuwa umegundua ni makosa,ni makosa makubwa sana  kwa kutokufanya lile usilokusudia,maana wakati mwingine unaweza kutenda jambo ukihisi umeweza bila ya kujiuliza yaweza kuwa unayarudia,tena yale yale..

Tabia yako chafu sana maana Ikiwa unajua kama unayoyatenda ni makosa alafu unatenda,sasa labda uitwe ni mpumbavu,maana kwa vile ya kutokujua ni mkosa baada ya kufanya kosa,ikiwa mwanzo lilipuuzika tu,hiyo ni tabia ya binadamu kuchagua njia zao katika kuelekea kifo pia,unachagua wenyewe,unajijenga wenyewe,maana kuna vitu unaweza kuishi navyo maishani mwako na usivifurahie,baadaye ukitegemea uvafurahie,inakuwaje usipofurahia milele?maana kwa hapo tu yanakuwa yamewezekana mengi sana..tena yale yale.

Inatakiwa kiingilio sasa katika kuwekeana tabia njema,hapo ukianza tangu utoto,hakuna Yule mwenye tabia nzuri kati yetu wote humu duniani zaidi ni wote tunayajua mema ni yapi na mabaya ni yapi,hapo haikuwa na maana ya kusema mimi,kizuri ni kile cha mtu chake maana mkubwa anasema ili mtoto afuate tabia fulani,tena ikiwa mkubwa amekuwa katika tabia fulani..uelewa ni swala tofauti na tabia,maana tabia ni wewe,ndiyo maana hakuna kama mungu,ni yeye lakini yu ndani yetu,yupo kama sisi,yamkini yeye ni mkuu.yeye anatabia zake..

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...