Sunday, February 19, 2012

MAKINI.


NIangalie,Nione ni natumika katika utofauti wa namna gani ikiwa pamoja na mashine au mashine zinatumika ikiwa kama  ni mifano yangu,zikimaanisha mimi ndiyo mashine na zenyewe zimetengenezwa kwa mifano yangu pia.bora hivi ilivyo maana ikawa haina haja ya kuzoea kile kilicho halisia,kwa umakini ni lazima ujitambue ya kuwa nisiwe mvivu,nataka kazi na nisijue huko makazini kuna nini nachokifuata,Haina haja ya kuwalazimisha walimu na wakati wanafunzi wenyewe hawaelewi,nikisema waelekezwe wanafunzi nitaingilia majukumu ya walimu,tena inaweza kuwa chukizo kwani muda wote huo shuleni wanafunzi wanajifunza nini?au unavyovijua hujui kama ndivyo unavyovifanya,maana tabia yao ni kufundishwa ili iweze kufanyika,ikiwa kwa kuona ama kusikiliza yote ni lazima niwe na umakini nayo,kwani yale yanayopita yananipitia hapa nilipo,utachaanganyikiwa kwa kutokuwa makini,kwa kutokuwa mwangalifu na ufuatiliaji wa mambo yako usifanye kuwa unapelekwa kila mara,kwani itafika kipindi utachoka kupelekwa pelekwa kama mashine,ikiwa ulikuwa unapelekwa basi wapo waliokuwa wana upeleka peleka,na wao wanaweza wakaamua kukupeleka kipindi pale umechoka,hautakuwa utumwa,hayatakuwa mateso,ni sawa na jambo usilolijua,labda kwa namna itakavyo tokea ndivyo italeta maana itakayo kuwepo,labda kwa tahadhari ufikiri na uamue kwamba unahitaji kujitambua.

Yule anayefundisha bila kuyajua mazingira yake ana uwalakini wa kuitwa mwalimu,lakini ya kuwa kuna uhaba wa kufikiri bora ikawe kujikimu,maana imefikia wakati utaamua kuwa mwizi alafu ukakataza kuiba, ,na ukija kukamatwa uelewe ulikuwa kama magurudumu ya gari,ikiwa kuna kona ulikatishwa tu,kwa hiyo siyo mageni sana katika kutokuyaelewa,wachache wanaelewa  kwa jinsi tunavyoelewa,anapotangulia mwalimu darasa hupanga yale waliyoambiwa na mwalimu,njia mara nyingi huonekana kutokana na hali ya hewa,ingawa unaona kwa umakini lakini unajikuta ukielekea mahala usipopafahamu,na hii yote ikiwa bado unaona labda njia hizi zinahitajika kufanyiwa ukarabati kila muda na watu wakajua,maana tulio maskini tunalia muda wote,na sio kwamba hatupo makini,kwani mengine sio ya daktari.unapolia sio ni watoto,unatoa machungu uliyonayo ukifikiria ulipotoka mpaka ulipofika,kama mtu afanyapo kazi kwa nguvu na kutoa jasho ndivyo ilivyo kwa mateso ya moyo inapokupasa kulia.
Kama walivyojijengea,nguvu usimalize kwa yale waliyokuwekea,ikiwamo inaruhusu usiiruhusu kwanza,wajichunguze wenyewe wanafunzi,hata ukageuza ramani Yule aliyemakini hapotei kwao,ingawaje, zaidi uendelee na umakini wako ili yale ya mbele yakafanane na ya nyuma pia.Umakini unahitajika kwani yaliyobadilishwa kutoka juu kuja chini mengine ni mepesi yakaweza kudondoka yenyewe ,ukumbuke wokovu upo,na kama uliokolewa jana haina haja ya kurudia kwani wengine wanahitaji pia,vingine ujiokoe mwenyewe maana umepewa kila kitu,na Yule asiye nacho kwa kuona hivyo afanye lolote na ataelewa maana, ,maana tena ikiwa wale ambao hawawezi wamepewa nafasi za mwisho kabisa katika kufauru,ikiwa umakini mdogo pamoja na fikra  ndiyo huo unaweza kuwa uwezo wetu.

By:         Benson G.Makaya.
Email:bensonsmakaya@gmail.com

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...