Friday, November 9, 2012

USIOGOPE,KUWA NA FURAHA…


Ni namna ya maisha yanavyokwenda,maana leo ikaja lakini siyo kesho,ukawa na hofu ya leo maana ile ya jana nusu imeishia leo.. kama ilikuwa ni chuki wazi ukawa na wasi wa kesho kuja na kukudhuru tena,usiogope kwa kuwa haujui,na tena kuwa na furaha kwani ukijua hautaweza kuogopa,hivi muda unavyokwenda unapelekwa na wewe,hivi kesho giza baadaye ujue unaileta wewee...mwangaza wa kung’aa humulika mbali kwa kuwa huitaji kukumulikia,ikiwa mazuri unayaogopa basi kuwa na furaha na mabaya ya baadaye.

Muda wa kutokuzungumza utafika,ile shule ya maisha yako ukaja kuijua shuleni.tena ukajifunza mawili kwa kuogopa kujua lako moja,leo ukiwa unajitahidi kesho utaweza maana njia ya mpita njia hueleweka yake kwa kuwa hupita kila siku hapo kwenye njia yake,pengine ikiwa ni mara chache acha jina basi,maisha mengine hayajulikani,hayo ndiyo maisha yako,pengine ukitaka kuyabadilisha ni uyabadilishe hapo ulipo,ujibadilishe,ukaogopa kupangua kwa sababu ya uwingi wa kushindwa kupanga tena jua unaidhurumu furaha yako,dhuruma mbaya maana hitaji lake wakati wa kurudi ni FURAHA.

Sitaweza kuogopa kukwambia ukweli kwani naihitaji furaha yangu baadaye,kwa Yule anayeogopa kwa kusema uwongo wakati ukweli upo,hafai hata kujifunza jambo,maaana ataangamiza jamii kwa kutengeneza siraha inayodhuru bila woga.pengine usiogope kusema utakavyo maana hautaishi tena,kama ikiwa  ni katika namna tofauti,hata kama umewahi kusikia pale mtu akisifia “ahh yale siyo maisha”..yapo yale yaliyo ni maisha pengine kama ulikuwa unaogopa kuuliza ijue furaha yako.

No comments:

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO : Watakwambia unabahati kwakile ulichokifanya kilichokufanya uwepo hapo,kujipa ufalme na kuzungumzia maisha...