Tuesday, June 5, 2012

IKULU..

Kule kwetu kuna mahala panaitwa makunguru,ali hali ingalikuwa nzuri tungalihamishia ikulu,



  

mambo yamekuwa mengi hata ya kujistili nayo yamekosa uhuru,ikabaki kupuuza uliyonayo na kusubiri msururu,maana vya kugawiwa  na yenyewe imekuwa ndiyo vinakunusuru,ikidhihilisha nia za watu kuelekea ikulu,ubadilishe maana na tafsiri ya  safari yako usije kupata laana yasiyo ya maana kwa sababu pengine hata sizo zako,ikulu ni patamu labda ujaribu nafsi yayule,ikiwa kila mmoja anayo nafasi ya kuona kile akifikiliacho,ikiwa kila mmoja akitaka yale mazuri machache kumfikiapo.

Matunda yametoka mtini pale,vijana wahini mwende illi mkayale,miti isije kauka mashambani,kijana ufanye hima usilale,pengine wakati wa kueleweka ndiyo huu,ikiwa watu wanahitaji kuelewa tu,kujua kama iliyopo ndiyo sahihi na hakuna nyingine,maana zaidi utafanya kukopi na baadaye kutoa kile kilichotoka,hapo unakuwa umetohoa,usipende viongozi hao,kila aliye mtu aonyeshe nguvu zake na ainuke,shamba liko tayari kwa kulima na miti ni michache,shamba limekuwa laini kwa kulima kwa wa mjini wachache.

Kuitangaza nia sio kama kuzamia,kuitangaza nia sio ya kutaka kushika mkia,maana wa kuongoza akiwa ametangulia wakuongozwa hupaswa kuvumilia,sio zikaje taabu ukasema ungevumilia,yatakiwa upate sababu na moyo kuutia utaishia njiani pale madongo yanapokujia,yataishia kinywani kwa kidogo utakayopatiwa.usiumize sana matumbo kwa kula chakula na mawazo kufikiria,usipate presha sana na moyo wako kwa uwoga wa kutokuchaguliwa.

Leo twende kesho wengine walitangulia,kwa uchache uliopo usipofanya leo ya kesho ni kwa wengine kuwatukia,yapasa sasa ukiwa na imani utaingia,yapasa sasa kuomba ruhusa ili ukafikirika kuingia,haujabuluzwa sana kwa nguvu ukaingia,haujaambiwa sana kwa macho na masikio yakasikia.unaisubiri kesho ije maana wengine walitangulia,unasubiri kesho ije maana majibu yalitangulia,maswali ya leo umetakiwa kujibu kesho kwa kuamkia,maswali ya kesho ujibu leo ukifikiria,ikulu imenona kwa utamu ninaouhisia,ikulu sio Dodoma ni dare s salaam naskia!

Ngoja tuache tuone na utasikia,maana ya kesho kwa wengine ni vigumu kuyafikiria..

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...