Tuesday, June 5, 2012

JANA NA LEO.


Jana ikawa siku ya maandalizi na leo ndiyo leo,ndiyo ikawa na maana ya uangalizi pale la muhimu likawa matoleo,ikiwa kwa mara chache yakikaribia usoni huruma kwa mwenzio,ikiwa mara chache yakikaribia rohoni ya nini kwa mkeo,hakuna asiyependa maana maadui wapo,hakuna asiyechukia maana tunaopenda tupo,maisha yameharibu kuta kufanya nyufa na kuonekana leo,maisha yameharibu vitu kufanya watu na mahusiano yao,isiwe hatari ya mwenzako ikawe kinywani baada ya kileo,isiwe adhabu ya mwenzako ikawa samahani kwa leo

Pengine umechelewa kucheka,pengine umewahi kununa,maana ulipaswa kucheka jana na kununa leo,vile ikawa jana na leo,pengine hata mavazi ya jana yasionekane ni yaleo,tutasahauliana jamani tusijefanyiana ya haya ungeyafany a jana,usijeugua magonjwa ukasema yamekuja leo,ukitafuta sababu na kurudi jana na kusema walipasa,walileta wao.

Mengine haina haja ya kumwachia mungu,pengine haina haja ya kumsemea ndugu,ya leo uyaache ya jana kafanya nani uangalie usije vuna mabua ukaja fanana na nyani,ya dunia yameongezeka na hizi pilika kiu zikijaa vinywani.

Ya leo yamekuwa machache kwa imani ya wasio tamani,ya jana yalikuwa mengi kwa imani iliyotamani,maana umetaka uje sasa,maana umetaka ufike leo,kumbe ulitamani yale ya jana yaje leo,kumbe haujatamani kwa ya leo yakafika kesho,hapana haya ya leo kwa kweli yabaki hapa,yaishie hapa na kama yakitaka kuondoka yakaenda basi yarudi jana.

Kesho ije itatukuta vizuri,kesho ije kama ni kuta
umezipamba vizuri,

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...