Saturday, March 30, 2024

ELEWA 1

Usidharau upendo unaoupata,sio kila kinalengwa kinalengeka,ukiona mchele umeota kwenye maji kuna ardhi chini ,haihitaji nguvu kupanda mbegu,itakuchosha mapema na utapoteza furaha yako vivo hivyo,asikwambie mtu kucheka wakati mrefu wa kununa ni nguvu tosha na ikakupa amani muda wote.

kama hakuna jibu kwanini uliingia kwenye mdomo wa mamba basi utakuwa unaishi nao,kujua kuogelea sio kuitii kiu ya maji ya kunywa,sehemu nyingine za kuogelea kuna mamba,wazee hupendelea sana swimming pool,sehemu za kuogelea ndogo ,vijana hujitupa maziwani na mabaharini na wakifika katikati hushituka na kujilaumu,na huo huwa msingi wa kubomoka.

Kuna maziwa na bahari nyingine zina ghasia sana,utaratibu mtu mmoja lakini wao huwapanga hata ishirini,mawimbi yanatoka popote kwenye mwelekeo,bora swiming pool mawimbi utayaleta wewe.wanasema saidia uendelee na safari,ni vile unatoa dhaka na mchungaji anaenda kununua shamba ili alime apate chakula cha kuuza na familia.

Elewa kwamba sio yote unayoyaona lazima uyaelewe,hata kama umeyasoma sio lazima uyaelewe,elewa wengine wa kuwaacha,kataza moyo wako kushikamana na matendo,Elewa duniani kuna watu watataka kwa lazima kufikiria tofauti ya wewe unavyofikiri ili wao kuonekana tofauti.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...