Friday, June 22, 2012

ISHI UTAKAVYO


Wengi wameonekana wakiishi maisha ya samahani hiyo ikiwa hawajafikiria ni namna gani waweze kuishi,kwa bila ya kujua nini wanachokifanya yaweza kuwa umefanya mengi lakini yakaonekana machache,umegandamizwa na maumivu mengi maumivu ya maisha na bado upo na pengine unapomaliza jambo uwe unafikiria kabla labda baada ya hili nini kitafanyika ili kugeuza kuwa na kufanya kile mtu unachokihitaji ukiwa unahitaji kuishi maisha yaliyo sababu yako.

Muda mwingine ushangae yale unayoyafanya pale yakaleta mshtuko,ukiwa umeelewa cha kufanya na ukachagua hapo unaweza kujua ukweli wako wa maisha na maisha ni kuishi tena vile unavyoweza ikiwezekana vile unavyopenda ,mafanikio yaweza kuwa hakufika ndiyo maana akaondoka ama kughairi hilo hutajua lakini Kile kinachokuja baaada ya muda unahaki kukijua na kukifauru maana kimekuja muda wako,hapa usipofikiria hofu ya  kuachwa na muda angalia usichague hivyo pengine wengine watakula kichwani na wewe uanze mkiani ama mwingine atataka paja na mwenzake kidali,pengine ni kutokana na ilivyo ama vile waipendavyo baadhi ya kila mmoja wapo.

Ishi ukiamini unajituma  na sio kutumwa,ishi ukiamini wewe ni bora Zaidi ya mwengine akuchukuliavyo,ulizaliwa peke yako sina hakika kama kua mtu mnagawana shida na raha,wengi wanaopenda na kuishi wanavyotaka hula raha zao na shida zao wenyewe na wewe ukifanya hivyo utakuwa umeishi vile unavyotaka na sio lazima iwe hivyo ila kuishi kutakuwa pale pale.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...