Ikiwezakeana sura yangu iwekwe
kwa kaisari,kilichoniweza ni kile nilichokiongeza,cha kwanza nilikuwa nacho
mapema,ndiyo maana ya kuja na kusema,ni maongezi nikifikiria,pembeni haina haja
ya kukuitia,tuongee pamoja tuelewane tusije jutia,ni mjita wa suguti mara
musoma nimetokea,muda wote haina haja ya kuitajia,tumefanya vingine kwa
waliotofauti ikaeleweka,wale wachache..tusiotaka hongera kwa makosa yetu,kila
mtu anayafahamu ya kwake!! inanikumbusha kulee,kule kwenye sura yangu,angalau
basi tufikiriane ndugu zangu,labda nimesema hivyo hata nikiwa nina nia mbaya,wala
si uongozi wangu utakuwa mzuri,ubaya wangu hautadhuru lolote ni mimi na uongozi
wangu.Labda tufahamishane kwa hili,nikipata nafasi ya kupiga picha ntapiga kama
ile katika shilingi mia,moja ile ya upande fulani,muda unavyoenda tutachaguliwa
wake ,maana naona nguvu zetu zinaisha,viwili kwake chake,moja kwetu vyetu,hii
ni mbaya ikitokea kwetu,labda tusijue nini maana lakini ombi langu ni
hilo,moja..hili la sura yangu kuwapo pale,najua ntaweza ikiwa sijafika hapo
waje wawaambie,zikiwa kama hadithi kwa wale watakao chelewa sana.
Tusitake maisha ya kurudi utoto
bila kujua tutawarudishia wapi watoto wetu,maana tuwape na njia ili wale wenye
watoto wengi wengine wajisaidie,hata kama ni njia na zenyewe zimekuwa ni
nyembamba zikihitaji nguvu ili kupita,tukisema kukonda ili kupita vyema wao
wanasema tumepata ugonjwa wa mawazo na tukinenepa inakuwa vibaya kwa
mapitio,itabidi tutafute njia yetu.kilichozidi zaidi lazima kiwe na sifa yake
iliyoongezewa zaidi,ni kweli maisha yalikuwa ni magumu lakini hii iliyopo ni
zaidi,hakuna asiyejua kuishi labda asikuelezee,yale tunayoyataka yataleta
maafa,nikiwa sijui maana yake labda,niseme maswali ya dunia nakumbuka kauli hii
nilipoulizwa kwa nini maswali ya dunia jibu likaja ya kuwa hilo nalo ni swali
la dunia,hatuwezi kwenda na maswali huku majibu tumemwachia mwengine,maana kama ni
shule zimekuja hadi za lugha tofauti,hili si kosa kwani shule ni kujifunza na
endapo unataka kujifunza unatakiwa kujifunza kitu ambacho wewe unataka
kujifunza,haina mshangao ila ni ya kustaajabisha sana shule watu tumeenda za
nini?maana ionekanavyo tu wengi sana tumesoma na maswali yakiwa hayana majibu.
Labda kama sijamaliza lengo
lieleweke,maana inaweza kutoka picha tofauti na ndugu zangu wakasema 'tulijua
sisi' ,wengine humaanisha vyao daima,bila ya kumjali mlengwa,hakika matangazo
tunayaona,tumejitahidi kulemba sura zetu zikiwa na ujumbe mbalimbali
tofauti,hiyo yote ikiwa ni kushawishi,hapa napo tunashawishi lakini imekuwa ni
namna tofauti,kwani lengo hapa ni uwepo wa sura tu mahara pale,pengine hata nkikumbuka kwa kipindi kile waswahili ndugu zangu walikuwa na usemi juu ya
upendo ingawa unawezekana bado ukawepo,nakupenda sana nikinywa maji nakuona
kwenye glass,yaani mzungu hapa anakwambia ‘indeep’,huu ni undani..ingali bado
tunaendelea kuishi basi ukawe undani wangu mwingine.tumalize na hili...
‘Ikiwezekana sura yangu ikae katika shilingi’
By: Benson G. Makaya,
Tel: +255
714 33 66 57.
Email:bensonsmakaya@gmail.com
NB: 10
Outfits Parents Love But Kids Hate
http://www.enannysource.com/blog/index.php/2011/12/11/10-outfits-parents-love-but-kids-hate/
http://www.enannysource.com/blog/index.php/2011/12/11/10-outfits-parents-love-but-kids-hate/
No comments:
Post a Comment