Sunday, July 1, 2012

UCHUNGU


Uchungu wa uzazi aujuae mzazi,tena ikiwa Yule anayeujua uchungu katika kuzaa,hapa isiwe nazungumzia uzazi,pengine tukafikiri ni namna  gani pale ikaeleweka Fulani ana machungu..si ya kuwa kwa kwengine ikajulikane namna hiyo,bali Yule aujuae uchungu,akauelewe kwa vile uumavyo,kumbe ni maumivu,kumbe uchungu unauma,haya si mambo ya Kiswahili,pengine tusitake ya kizungu ila yakawe yanaeleweka basi..nakubali katika lile mtu asemalo,kwani kweli yake ipo humo,humo anakuwa ameamua yeye maana ni mahala,kama ilivyo pale,yaani ndani humo,pengine ni duniani,yakuwa machungu yameonekana kuwa mengi,duniani kuna maumivu..!!

Sikatai hakuna kulalama,pengine tukawaruhusu wezi kutuibia,maana kama hatutasikia machungu basi wezi endeleeni kuiba….maana ifike wakati hatujaelewa kwa nini wanaiba,maana hayo si ndiyo maovu..mengine machache lakini si yote hata hili moja linatosha sana,katika kifo cha mwizi kinatia uchungu sana,sijui Yule anayaekufa huwa anasikia maumivu gani?ikiwa hatujaelewana nitafanya kurudia,lakini tukubari na machungu yatakayo tujia,maana tunyoshe mikono haya tumeyashindwa,na tusiposema hivyo lazima tuulizwe yaliyopitwa…hapo ndiyo tutaona machungu,maana yalipitwa na imepasa kuyarudia,’ni kazi kubwa kuirudia adhabu’

Kila ya jana yanaisha ninapoamka asubuhi,hii ikiwa nimeamka,nafsi yangu ikiwa inaniambia kufanya kile kizuri cha jana kilichobaki,maana ndiyo kitaleta kesho,hapo nikiwa naogopa machungu,sasa huyo sio mimi na mimi nitasema machungu yangu yapi?ama iwe mimi wa sasa ndiyo kama mimi..hapa nimezunguka sana,baadaye itaitwa mizunguko,maana ikinyooka wanaita minyooko labda iwe na majungu,yakifikirika kinamna yoyote tofauti na msemaji hayo ni majungu,,maana si vile kila mtu ana machungu yake naye afanye yake,ikiwa kila mwanadamu hapendi kulia uvunguni.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...