Tuesday, May 29, 2012

UZOEFU HAUULIZWI.


Wale wazuri wamefanya yao,tena ni mengi na mpaka yakawa mazuri bora,pengine walitumia ujuzi wao na katika maisha kitu ujuzi sio kitu kusikia,sio kitu kusema wala kufanya katika wakati wowote wa muhitaji yaani ni mtu kuelewa kujua na kuthamini kinachoendelea kutokana na muda,haina haja ya kutafuta ujuzi ikiwa kazi unayo,kuishi ni kufanya kazi ama shughuri ambapo unatoka ujuzi,sasa ukifikiri unaishije ndiyo utajua ujuzi ni nini maana unatakiwa kutoka mahala Fulani unapopaona,kuishi vigumu sio taabu ni kupenda ni kama huwezi kuoa ikiwa unaishi vigumu,na kama una uthibitisho wa ugumu ulionao hapo itakuwa haukupata mafundisho yangeyokuzoesha kufanya hata usichokipenda.

Kusudi halina sababu ya kwanini ilete maana yenyewe,ingawa hatuwezi kufanya kitu bila kusudi,kusudi sio sababu ama mazoea kusudi ikiwa ni dhumuni,na hata tusifanye mambo ya sababu maana tumejawa na sababu nyingi sana katika kila tukifanyacho,lakini kusudi huwa linatimiza nia,ni kueleweka kwa kutimiza dhumuni lililotokana na uzoefu,kujua tena ni  kuijua sababu iliyokosewa mwanzo,sasa ikiwa ni kwa sababu ipi ndiyo pale tutauliza dhumuni la kila mmoja ili tuonyweshe uzoefu.

Kuna uzoefu mwingine haufai kuuzoea,hasa ule ambao hauupendi wewe mwenywe kwani ndiyo utakuwa ni uzoefu wako baadaye unapoendelea,utakuwa umezoea hivyo kama ni kupenda au kutokupenda,pengine unataka uzoeane,uwe na umoja uijenge nchi pamoja maana hata ukibisha wazoefu watazitafuta sababu na kufanya yao bila ya kuuliza,umezoea kufanya nini hata ujiulize basi na kama umezoea hivyo na haujaambiwa ni vizuri basi usubiri majibu,ulimwengu hutoa ushindi,Ushindi wako upo mikononi Mwako uko mahala pale Umezoa.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...