Tuesday, May 29, 2012

NGUVU ZAKO..



Endapo tulizaliwa wanadamu kunakuwa na urahisi Fulani wa kuweza kuelewana,hapa hata ule uwezo wa kuelewa zikajulikana kama ni nguvu,tusijali zilizopotea kwani zinazokuja ndiyo tunazoziombea,maisha ya mwanadamu sio ya kulalamika zaidi ya furaha,pale tulipoambiwa tajiri kwa tundu la sindano na ngamia sio pale tulipotupia nguvu zetu,yaweza kuwa ni hapo lakini utambuzi usio kuwa na uwezo unaweza kufanya yale mengine kuwa mengine,hapo watu wakiwa wamechoka,hawataki yale magumu na kutaka mepesi,wakiamini kuweza kwa hali ya kawaida wakiamini kuweza kwa kusema ilikuwa rahisi bila ya kutumia nguvu zako,kile kinachoisha kimetumika,yanapokuwapo maneno ni lazima tuseme,

Yanapokuwapo maumbo ni lazima tuyaunganishe,maaana kutimilika kuwa moja si sawa na nusu inayoelea,hapa tukiunganisha nguvu zetu ingawa sio lazima zangu na zako ama za Yule bali zako,zangu na mwengine yeyote,haujafika wakati wa kulalama wakati bado hakuna wa kumlalamikia,maana kama ni kwa mungu huku ndiko tunapoelekea,tunapompa lawama Yule aliyezoea tutaweza kuonekana wajinga wenyewe maana hapo tunahaki ya kuulizana kwani nguvu nyingine ziko wapi?ama hatuna na kama ni hiyo ieleweke hata kwa kusema,isemeke ikiwa inahitaji msaada maana inaupungufu wa nguvu

Pumziko la mtu anayetafuta ni nguvu kwa mmoja aliyelala,hapa tusilale,hapa hakuna kulala maana wakati ndiyo huu,muda wakuupoteza ulipita na kubaki wa kutumia nguvu,tumelishwa sana na wakubwa zetu wakiwa wazazi pamoja na ndugu baki hiyo yote ikiwa ni kutaka kuonyesha nguvu,,hakika misemo ipo lakini si kwa mwanadamu ikaonekana kwamba hapa au pale alishindwa nguvu,kwani maana ya hakifai ni kile kilichoachwa jana,hakikufahamika kama kipo ama kilifahamika na nguvu hazikuwepo,

Tusiwakaribishe wale wengine wasio na uwezo wa kufikiri,wao nguvu zao hutumia kwa utofauti na wenye akili,wao nguvu zao hutumia ipasavyo ya kuwa ni tofauti na sisi,wa kuchekwa hakuna maana wote hatujafanya,wote bado hatujatumia nguvu zetu,kama tumetumia embu tuambiane ni mahara gani,yaweza kuwa zilitumika bure na umekuja wakati ni ieleweke sasa,kipindi cha kupita hakifai kupita tena,kipindi kinachokuja ndiyo kile tunachokisubiri,Yule anayeandaa nguvu kwa ajili ya jana hataki la leo,ingawaje na lenyewe lilibaki tokea jana hiyo,ni kama mpiga picha hutumia nguvu zake ili apate kula,hutembea pengine asipokuwa na ofisi na hiyo ni kudhihirisha maana ya nguvu,akirudi aseme amechoka na mwingine akaulize kwa nini maana yaweza kuwa alitumia nguvu ndogo katika kufikiri iliyompelekea kutumia nguvu kubwa katika kutembea,labda tuandae mazingira kwanza,tuyainue,tujiinue.

Onyesha nguvu zako tokea moyoni,onyesha kwa kile ukifanyacho tangia usoni..!!










No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...