Tuesday, September 11, 2012

FIKIRI

Fikiri Leo umetumwa wakibaki peke yao,maana wakitaka kupata faida wazijuazo wenyewe,ikiwa unasikia ni lazima kutaka kuacha maana ukweli  umeonekana,ikiwa chini ni utata basi tujaribu kutafuta vya kupunguza maumivu maana kwa starehe tutapona ikiwa hata kama tutachelewa isionekane kwani mazuri mengi hutokea pindi pale mtu anapojidai yeye ni yale anayotaka na kusema yeye,maana kutokutaka ni namna ya kukosea,haina haja ya kumfunua aliyelala maana adhabu iliyo tamu ni maumivu yanayoifurahisha nafsi.

Usitukane kwa kupiga maana mwanzo  ukiwa mwisho ni furaha inayoleta karaha,iliyokuwepo tangia jana tusiifuate kesho maana hata tukatukana tutahitaji maana ili kuleta namna za kuelewa,usiseme wewe kwani kesho ndiyo zamu yangu,kile kilicho chako ni changu katika upendo usio kuwa na maana ya hitaji,nawapenda sana wageni maana wao niwahitaji wa mambo mengi sana.

Katika ukweli tumenyamaza maana pengine itajulikana ni uvumilivu uliopo katika kukubariana ili mradi ikaeleweka kama ndivyo vile ilivyo katika kuelewa ama ilivyo pangika kimfano maana hata matusi katika kutaja majina itaeleweka kuwa ndiyo naamna ya kuitika ili leo wakaja pembeni wakisema na wao walisikia wakiitwa kumbe majina yanafanana bila kujua.fikiri uliitwa wewe na majibu hukutoa eti ya kuwa hukusikia au pengine mwitaji alijibanza pindi akifikiria ndiyo.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...