Friday, February 17, 2012
Makaya's Forum: USHINDI…UNAHITAJI KUJIANDAA.
Makaya's Forum: USHINDI…UNAHITAJI KUJIANDAA.: Maandalizi ni malengo katika kutekeleza yale yanayotaka kufanyika,ikiwa katika mmoja mmoja hadi pale ikafikia kundi,hii yote hutokana ikiw...
USHINDI UNAHITAJI KUJIANDAA.
useme ni wangapi wanaojiandaa,na utakuta ni wote maana kila mtu ajiandaaye hujiandaa mwenyewe,yule anayeandaliwa ni lazima ajue kuandaa pia kwani endapo akishinda hataweza kuulinda ushindi ya kuwa hana maandalizi useme wale wanaoamka ndio wa kuweza kujiandaa kwani walikuwa wamelala,na wale walio lala ni kuwaamsha ili waweze kujiandaa ikiwa ushindi mtu anaupata pale hasa alipojiandaa mwenyewe,maana unaweza kuja kidogo ama ukazidi na kufanya karaha,kivingine ikawe ni ile bahati maana haukuwa wa maandalizi yale,ushindi wa bila kuongea unaweza usisikike,na mara nyingine ukiongea sana wanaweza kunyamazisha,maana wao hawamjui mungu na labda nisiseme hivyo zaidi iwe wanamjua mungu wao.pale unapokosa ndio pale majibu yalipo,ni kama pale unapopata ingawa haitaweza kulingana,ni tofauti ya kuwa moja ni ushindi nyingine ni kinyume yake.
Kile kinachoweza kuzuilika ni kile kisichopangika,maana kitakaaje?kama maji hupita kokote,hata yakaleta uharibu hata ikawe sio lengo kubomoa,pale yanapobomoa yenyewe ushinda ikiwa yalipotoka yalikuja na yakabomoa,labda yangeenda pengine ili ungejua kuwa haikuwa lengo,na iweje yangefanikiwa ungeeiita ni bahati yake,kwa yule anayejenga ukuta kwa ajili ya kuzuia maji hayo anajiandaa,kwa yule anayeyasubili yaingie mpaka ndani basi atafanikiwa,maana amesubiri hivyo,muda mwingine huwa inakuwa haiwezekani,ikiwa katika hali ya kawaida hasa mtanzania ikiwa wengi hatufahamu mazingira yetu,ikiwa ni miili pekee tunayoifahamu,tukisahau mazingira mengine tukataka afya bora,hii itakuja kwa kunenepa ikiwa ni bora basi itakuwa bahati,siwezi kusema sana hapa labda tungeulizana nani au na flani wanapenda nini,maana utofauti upo,na matokeo sio maandalizi,ikiwa yenyewe yakawe na kusudio la kuleta ushindi.
Vizuizi ni haki kuviweka pale unapojiandaa.lakini ni pale tu utakapo jua ni unazuia nini,Katika utofauti wa malengo tuseme yawe yanayofaa yote,yakitofautiana kwa mabaya na mazuri kwani tunaweza kuchanganyana kwa muda mbadala,endapo yale yasiyokuwa ni malengo kufanyika kama malengo wakati Fulani,yule anayejiandaa ndiye anayejua lengo hasa,labda na ije tofauti..hapo tunasema anapanga mungu.
mda mwingine lawama hazifai labda ujue nini unachokifanya,maana kama ni unajiandaa na imetoka kipindi maandalizi yakawa magumu unaweza kuyakimbia endapo haujafahamu unajiandaa na nini,
'tutaishia
kunawa maji ikiwa na chakula tumekiona mbele yetu'.
kwani hata meza zenyewe waligeuza kitambo!!
By:
Benson G, Makaya,
Tel:
+255 714 33 66 57.
email.
bensonsmakaya@gmail.com
Thursday, February 16, 2012
Makaya's Forum: BINADAMU ANAPOTEMBEA..!!
Makaya's Forum: BINADAMU ANAPOTEMBEA..!!: Binadamu anapotembea anaangalia wapi..?maswali mengine bwanaa!!tuseme ni kushoto ama kulia,wale wenye uwezo huangalia kote,hatuwezi kuan...
BINADAMU ANAPOTEMBEA..!!
Binadamu anapotembea anaangalia wapi..?maswali
mengine bwanaa!!tuseme ni kushoto ama kulia,wale wenye uwezo huangalia
kote,hatuwezi kuangalia kote bila kuwa
makini,yaani utambuzi kiujumla
kujielewa.
Hatuwezi kusema wote tunaangalia kote,kwani wote
sio wale tunaotembea,na hii haiwezekani,ni kweli tunatembea,na ni kweli sio
wote.muda wote tuseme sio haki kutendeka lakini ndio inatendeka,hakuna yule
atendaye lisilotendeka na likaitwa tendo
bora,matendo ni yale hasa tuyatendayo,ndiyo na yote sio mageni,sio yale ya
kushoto wala kulia,ya chini yatabaki huko maana hayana haja ya
kuyafikia,wengine watasema hawajawahi na kama kutenda ni kuwahi basi wote tumechelewa.
Sio yale tuliyonayo tukimaanisha tumeyatenda,hata
kama tumeyatenda si yale tunayoyasema tumeyaweza,yapo yote na
tuliyoyashindwa,tunapotembea sio miguu tu kwani hata akili nayo hufanya kazi
kubwa mikono nayo pia ikatembee,muda mwingine tutembeze na mioyo yetu.Wengi
watu hatuelewani,tumesahau kuwa hata wale wa zamani waliandika,ndiyo wale
waliotembea wamefika hadi hapa,waliacha akili zao zinatembea,sasa wengine wakiangalia
wanavyotembea wanapofika ni pale walipo,mahala na muda wanautaja kama ulivyo,ya
kuwa wapo hapo.Kama matembezi ya maelfu yameshindikana basi hatutaweza
yoyote,wataweza wachache,ni kama ilivyo shule kwani chochote kile sio cha
kusoma,cha kusoma huwa wanaambiwa soma hapa,elewa
pale unaposoma,jua unachokisoma sio kile unachokiona,macho hayadanganyi lakini
kwa dunia jinsi inavyotembea haiangalii mwanadamu amesimama ki namna gani.
Tusherehekee vyote na tujipongeze hasa pale
tunapoona tumeweza kukimbia,ikiwa ni wengi wanapenda kuwahi,labda tutembee
haraka tu tusikimbie,yakuwa hatujui tunakimbilia
wapi,tusije kimbilia bomu,bomu hufyatuka endapo pale kunakuwa hakuna
uangalizi na yule anayekimbia uangalizi wa sehemu aliyopo ni mdogo
sana,tukubari yote ya kuwa tunauwezo wa kukataa yote,kwani hata tukisema ni
kutaka ufikiriavyo wewe lazima wengine watakubari huku wengine watakataa,labda
tuseme haina haja ya vyote hivyo,watakao kataa na kukubari vyote kheri kwani
yule anayekataa njia hii anayo nyingine,yakuwa
anataka kupanua uelewa,ili asaidikike atakua ametembea.
TEMBEA UYAONE..
By: Benson G. Makaya,
Tel:
+255714336657.
Email:bensonsmakaya@gmail.com
Wednesday, February 15, 2012
Makaya's Forum: SAUTI KALI...
Makaya's Forum: SAUTI KALI...: Sauti zimezidi kuwa kubwa,zimejaa na chumba ni kidogo,ikabaki ikawa na sasa imekuwa ni mtafaruku,sio mda wake huu,ingawaje kihalisi imet...
SAUTI KALI...
Sauti zimezidi kuwa kubwa,zimejaa na chumba ni
kidogo,ikabaki ikawa na sasa imekuwa ni mtafaruku,sio mda wake huu,ingawaje
kihalisi imetimia,labda upate mawaidha,yaani utiwe moyo,unaweza kuleta
usikivu na ikiwa hivyo ukakaa chini na kufikiria,lakini isiwe hadi kufika
kilele,maana hapo nguvu zinapungua,uwezo wa kufikiri unatokana na nguvu pia,na
hapa ikaeleweke sio wazee wanawasemea,ni vijana mkaweze kukaa na kuweza
tazamia,milango usifunge,makelele yatakuzidia,ingawa ulikuwa hujui ya
mwanzo yaliyokufikia,usingeliyafahamu hata kwa nguvu kupayukia,vile sauti kuwafikia,labda ufikirie na kwa makini kusikilizia,tunavutiana kwa
namna isiyowezekana,na hii itatupelekea kukaa kimya sana,hata ukaweka utamu wa
lugha kwa jinsi zinavyojulikana,haita leta msingi zaidi ya watu kupigana,ikiwa
wengi wanasoma shule yale ya mtaani yamekuwa hayana maana,ingawa ni yetu ya leo
na wala siyo ya jana,tumekuwa wazembe wenyewe haina haja wa zamani
kuwatukana,hata ukatembea mbali kutafuta nyama,majani yatakuotea karibu na
kuchafua bila hiyana,unahangaika kwa pesa na zimekuwa hazina dhamana.ikawekwe
barabara iliyo jaa rami kama mkeka,faida ya nani kama siyo ya malaika?maana
imekuwa ikipita siku chache na kubomoka,sijui ni raslimali au ujuzi wa
kutokujali,ntaongelea machache yasiyo kuwa na hali,siyo yale ya wanaume wasio
lijali,ni wazi kwa mwenye vichache apaswe kuongezewa,maana ni anavyo vichache
kweli,ile ya mwenye nacho kuongezewa ni ya watu hai,wafu lao kaburi,na maombezi
ndiyo nyongeza yao,nao wafike salama mahala pema mbinguni.
Mambo yanapozidi
kuwa magumu ndiyo mwanzo hasa wa yale maraisi,ni kile alichonacho mwanaadamu,ingelikuwa kila
mtu anazaliwa anaambiwa nenda kaendeshe baiskeli sidhani kama angetoka mtu na
kusema ni rahisi,tena bila kufundishwa..kwani hata hiyo baiskeli yenyewe
ingelikuwa ngumu kuitaja bila ya kuiendesha,mbadala wa matembezi
yanayotoa sugu miguuni ni mapumziko ya viungo hivyo,hawakuchoka hawa
wanaotengeneza baiskeli tangia mwanzo,wakarahisisha mpaka wakaweza kusafiri nazo,sio
uwezo ni namna ya kuweza na kigezo,inapochakaa baiskeli makelele
huanza,ukapita mikoa mbalimbali kama mbeya na mwanza,baiskeli zinapokuwa kitu
cha kwanza,ni maendeleo haya kwani hakuna aliyeyakataza,barabara zikaonekane
hazina maana kwani hata mijini ukawawekea bado ni mtafaruku kwa wao kupita
yapitapo magari,na ikiwa ni mmoja wapo watakupigia kelele ya kuwa unaleta
foleni.mambo ya mjini ni mengi,lakini mji huo huo ndiyo kijiji,sasa uchague
moja kati ya kijiji au mji,maana unaona watu wanatoka morogoro wanakuja
kutibiwa hospitali ya mkoa dare s salaam,wale wa dar na wenyewe wanafanya hivyo,mshangao
kwa wale wanaosafiria nje magonjwa yao,kenda rudi ni maralia na baada ya hapo
ni mapumziko..kule hakuna kelele tatizo
hapa ni pale unapopumzikia kodi za watu huku wenyewe wakiwa hawazijui hata
haki za kwenda hospitali,sauti kali huleta ugomvi kwa kutokuelewana,na baadaye
ni vita.
Macho yasitoboke,masikio yameziba sasa wanaopiga kelele
waendelee,maana hata ukikataa sauti zenu hazipayuki na haipiti siku,pigeni
kelele wanafunzi na mwalimu akija mwambieni ni kwa sababu hakuwepo,maana
hujifanya kuelewa yao mara nyingine,hata hivyo ikiwa ni namna ya kutaka kujua
ni nini kifanyike mda huo.
By:Benson G.Makaya
Tel:+255714336657
Email:bensonsmakaya@gmail.com
Tuesday, February 14, 2012
Makaya's Forum: MAKUBWA ZAIDI YA FIKRA.
Makaya's Forum: MAKUBWA ZAIDI YA FIKRA.: Makubwa ni neno linalosifia kitu,kitu yaweza kuwa ni kitendo,kifaa,mawazo,nafsi ya mwanadamu mwenyewe na mengineyo mengi yanayomzun...
Subscribe to:
Posts (Atom)
Makaya's Forum: ELEWA 2
Makaya's Forum: ELEWA 2 : Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye n...
-
Pengine ukawe umemaliza mambo yako,au ukawe upo katika njia ya kuutaka ufalme,kipindi kile cha ngamia kupenya kwenye tundu la sindano ...
-
Makaya's Forum: AMUA YAKO. : Duniani wengi humkimbia mtu kipindi cha kifo,maana wakiona taabu ndiyo utasikia Yule kachanganyikiwa kabisa...
-
Yafanye mapito yako kuwa nguvu inayokusukuma kwenda mbele ukitegemea kuishi ndoto zako na sio kile unachokiogopa na kuhofia,wengi hawafanyi...
-
Makaya's Forum: YAFANYE MAPITO KUWA ELIMU. : YAFANYE MAPITO YAKO KUWA NGUVU INAYOKUSUKUMA KWENDA MBELE UKITEGEMEA KUISHI NDOTO ZAKO NA S...
-
Duniani wengi humkimbia mtu kipindi cha shida,wanaoamini kufika darasani ni kuelewa zaidi ya maisha yalivyo wameelewa tofauti,ikiwa...
-
Hulazimishwi kulia na wakati wewe unataka kufurahi na kucheka,swala la msingi ni kujua unapokatazwa kulia,hapa nikiwa sina maana ya...
-
Makaya's Forum: MAPENZI YANAISUKUMA DUNIA.. : Usipoelewa hautaweza kujua hata kama unashiriki vipi,maana kwa kutokuyapenda na kujifanya ...
-
Makaya's Forum: ONA KUSIKIA. : Mapema ni kheri kuona bila ya kusikia,maana haya machache tumeyasikia hapa kwa kuwa yalionekana mwanzoni,...
-
Unaweza ukawa unakataa mazingira uliyonayo,ukajikataa ukakataliwa ama ukakatalika hiyo yote ikaonekana kwa kuwa maisha yana msukumo tofaut...