Sunday, June 17, 2012

BABA DAY..!!

 Imefika siku yangu leo,mimi mwana mwanangu aliyeniita baba,akiwa na maana ya kushukuru kwa kile kilichopo,pengine utanasema wakiwapo na usijue wasipokuwapo,labda ukiwa na woga ikiwa kiendacho kwa mganga hakirudi tena au  iwe katika mazingira ambayo sio ya lawaida kwa vile tuyaitavyo,labda ya kishetani ikisemekana na bila ya haja ya kuwa na uhitaji wa kumfahamu huyo shetani mwenyewe.

Pengine wengine wamekuwa wakimkimbilia mungu kuliko mababa zao,hiyo ikiwa wamesikia mungu ni mwema sana,wakifikiri mabaya yale yaliyopo na baadaye yaweza kuja kushangaza kama ya zakayo na hapo ni lazima ikaeleweka kwa maana umeweza kusoma kwa sababu yao,ndiyo yao ni kwa sababu unakemea ulipokataa fulani kwenda shule na vile mchafu sana kwa kuchezea vyombo vya vumbi basi inalazimu kuoga hata iwe muda gani hapo mapenzi mengi utaonyesha kwa kuhesabu idadi.

Leo siyo ya kina mama na sio kwamba zawadi zote ale baba,leo ni siku ya wanaume kwa walioweza na bila kungoja,maana wameitwa hata kwa lugha vile zikawa tofauti,leo tunaweza kuwakumbuka pia mababa zetu kwa  wale waliotangulia na kumpendeza mungu kama ilivyoaminika,''baba yangu ulale mahala pema''

sina zawadi nyingi nyengine zitashindikana,maana kama ni baba zawadi leo zitajaa dunia.

NAKUPENDA SANA BABA..

Saturday, June 16, 2012

PANAPO!!


Muda ukiwasili palipo inatakiwa kuelekea,
maana ikiwa ni kufanya hata kwa ilivyo kwa namna ya kuweza kuutenganisha muda ili uje kuleta maana,kauli ya kusema hapo ndipo palipo haikusemeka kana kwamba ndipo ilipo maana pale ukakamatana mashati na hata kushindwa kuelewa kwa yale yaliyopo na mengine yasiyozungumziwa,
pengine ikiwa hakuna aliye yafahamu kama mimi pia,au labda ukategemee ile  baadaye,
Ukaja kungoja nayo ikiwa  pameonekana pana uwepo,
maana watu kama wameamua tu kukaa hapo basi palipo kidogo au hata vile nafsi ikaridhika.

Mizunguko inatengeneza duara,
ya kuwa na maana ya kuacha kijiti na kukimbia sana kwanza  ukafika na kusema pale au hapa nimewahi,
hakuna gumu  lisilo tegemeka ikiwa kuzunguka imeamulika,hapo maana kuzunguka ni vigumu,
hivi pengine ndiyo watu wanaamua kupita njia zao.maana hizi zetu zimekuwa  za kuzunguka zaidi,
kwa kipimo cha uwingi unaweza kuleta maana ya umoja,
hii ikiwa unazunguka pamoja  na ukiwa hauna maana ya kujipa namba.
Muda huu  ulizungumziwa lakini kuna wale wapya,mapya yamekuja pia kwa ajili ya wale wa zamani,hii ikiwa wale wapya wamekuja na mapya na wale wa zamani wameendelea na yale ya zamani lakini yakionekana ni mapya,hapo ni matunzo sema sasa ukutane ubadilishane,japo sio kitu kikaonekana ila hata kimazingira kuonana,maana panapo kuwa na nyuki lazima asari kuwepo.

Pengine ukakutane pasipo nyuki wenyewe kuwa na asali,
hapa usilalamike na manundu,kwa wanaoweza kulala chini,isiwe walizoea na kuona raha,juu pia kuna raha,embu panapo fika na nyuki kuwasilli ubadilishane,hapo ujue aliye kuwa akilala kuwakwepa nyuki ni nani?maana palipo kwa zamani panaweza kujirudia tena.

Makaya's Forum: ELEWA 2

Makaya's Forum: ELEWA 2 :   Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye n...