Saturday, February 18, 2012

Makaya's Forum: MACHO YANAONA SAHIHI..

Makaya's Forum: MACHO YANAONA SAHIHI..: Ni wazi macho hutumika kwa kuangalia,kuona,kutazama yote yakiwa kama ni matendo yake,na hii yote inatokana na namna tofauti ambazo zim...

MACHO YANAONA SAHIHI.



Ni wazi macho hutumika kwa kuangalia,kuona,kutazama yote yakiwa kama ni matendo yake,na hii yote inatokana na namna tofauti ambazo zimefikirika,na hata ukazifikia.macho ni moja kati ya viungo vya mwanadamu,NI macho!!

Pale mtu anapofahamu inapoelekea yeye mwenyewe katika nafsi yake kuwa na utambuzi na wakati mwingine unaweza usiwe wa kiujumla mtu wa kujielewa,unapoelekea ni mbali zaidi ya ulipotoka,ni kama pale umefika mahala  na kusahau yote uliyokuwa ukilalama nayo kwa mara ya mwanzo,yakiwa yale yamegeuka kuwa mazuri,na uzuri wake haujaja tu baada ya kuacha kulalama,bali ni pale uliposifia vizuri,maana unaweza kushukuru mungu kwa kufika bila kujua mahala unapoelekea,ulipo.tumshukuru mungu,tena kwa njia nyingine hazina waelekezaji…inahitaji nguvu kweli na uvumilivu ili kujua pia kuelekeza,si watakuja na wengine,wao ndiyo wakiwa hawajui kitu kabisaa,watatulilia pamoja na hata ukiwakataa utakuwa umezikataa nafsi zetu,maana ikiwa unakubari mifano hai isiyoonekana ,uangalie yasije timamu yasiyowezekana,yatatusumbua tu ingawa yanaonekana yasiyokuwa na ufahamu,tena hata kuwa na ubishi,wakiamini wao ndiyo wameishi,au tuone labda kama utasahau hata majina yetu maana ingali wote tungeitwa “SALUMU” ingelikuwa haina haja ya kuhukumu,labda ubaki ukituhumu ingawaje wanaonekana lakini ushaidi hautadumu,wanapoteza wao ili ieleweke wanayoitaka,maana ndiyo chaguzi pekee litakalo baki.na hii pekee usizani kwamba ni ya kwao tu hata kwako pia,yaani yangu ndiyo itabaki.maana kila mtu ataona ya kwake.

Yaliyopo yametoka mahala,yaliyopo sijui yametoka wapi,kwani nasema hivyo ya kuwa siyo yote mwanadamu akayafahamu,mengine yapo katika miliki na uwezo wa watu wengine,na endapo ukikubariana na hili basi lazima ujue kwamba lile au yale uliyoyashindwa ndiyo yetu,maana yangelikuwa si yetu usingeyafanya,au useme kweli sio yetu basi uangalie mara ya pili,maana wakati unavyosema si vile unavyomaanisha,ikiwezekana ujue wakati ni mwanadamu mwenyewe,kama kijana wa kiume akaota ndevu na asinyoe huo utakuwa ni wakati wake,amemaanika hivyo.na hata ikawe siyo mara ya pili ila ni tendo lililoonekana,maana kama tendo linaloeleweka ni litatimia kwa kitendo ni lazima ujue chanzo,ili  yakija mafuriko usilalame,maana ulijua yatakuja na kutuzomba,tena kwa walio mbali wafahamu..MAFURIKO!!.shida za kuonekana hazipaswi kumwinua  na kumtuma mwanadamu,anayeona na kutenda katika utatuzi ni mwana adamu mwenyewe,isifike kipindi ukalazimishwa kuishi,tena ikawe ni amri kwamba sasa ni “LAZIMA” ,ingawa usipoitumia lugha hii katika mambo yetu utashika mitutu,watoto wataona baba zao wanachokifanya na kwa sababu wao wamekuja kujifunza,wamekuja kukua,wamekuja ili wawe wakaitwe watu wazima na wakajue,watashika mitutu yenye technolojia ya kizazi chao,hapo vita itakuwa haina heshima..watoto wataonekana wakubwa,na kwa wakubwa labda uwasikilizie,ingawa wanasema vita haina baba. 

Tunapoelekea hakutazamwi mtu ukaambiwa ona,sio kwa macho.unapoelekea ni mbali lakini si kama kule ukasema ulipotoka,kwani wengine watasema ni karibu kutokana na maisha yao kiujumla,unapoelekea ndiyo kwa mungu.tunapokaribishana majumbani mwetu tunategemea HODI,kama kuna mgeni ataingia bila hodi huyo atakuwa mwenyeji sema ni sababu ya mgeni aliyetangulia hakumkuta mara ya kwanza.

 UKITAKA KUJUA NI LAZIMA KUJUA UMEJUAJE?

By:        Benson G.Makaya,
Tel:     +255714 33 66 57.
email:bensonsmakaya@gmail.com

Friday, February 17, 2012

Makaya's Forum: USHINDI…UNAHITAJI KUJIANDAA.

Makaya's Forum: USHINDI…UNAHITAJI KUJIANDAA.: Maandalizi ni malengo katika kutekeleza yale yanayotaka kufanyika,ikiwa katika mmoja mmoja hadi pale ikafikia kundi,hii yote hutokana ikiw...

USHINDI UNAHITAJI KUJIANDAA.

Maandalizi ni malengo katika kutekeleza yale yanayotaka kufanyika,ikiwa katika mmoja mmoja hadi pale ikafikia kundi,hii yote hutokana ikiwa kila mmoja aliyepo naye akiwa na timamu ya kutaka kufanya jambo lisiloonekana na likaonekana kama ni jambo limefanyika,ikiwa tu,kwake naye lilikuwa ni lengo.katika kujiandaa kuna mengi ili kufikia mwisho,mwisho ndio timilisho la maandalizi ikiwa hapo ndio tunaweza kujua kama ni maandalizi yalikuwa mazuri au la kuwa vyote hivyo inategemea na mtu kufuatana na (ma)lengo lake,USHINDI ni pale mtu anapotimiza lengo,ikiwa tu alijiandaa,hata mara nyingine ushindi huja kwa watu wasio jiandaa,na hiyo siyo ya kuitegemea ikiwa ni bahati,wala hatuwezi kusema ushindi usio kuwa wa kutegemea ni ule wa kukosa.tuna hitaji ushindi ili kutekeleza mambo yetu,tunahitaji kujiandaa ili tuweze kushinda.

useme ni wangapi wanaojiandaa,na utakuta ni wote maana kila mtu ajiandaaye hujiandaa mwenyewe,yule anayeandaliwa ni lazima ajue kuandaa pia kwani endapo akishinda hataweza kuulinda ushindi ya kuwa hana maandalizi useme wale wanaoamka ndio wa kuweza kujiandaa kwani walikuwa wamelala,na wale walio lala ni kuwaamsha ili waweze kujiandaa ikiwa ushindi mtu anaupata pale hasa alipojiandaa mwenyewe,maana unaweza kuja kidogo ama ukazidi na kufanya karaha,kivingine ikawe ni ile bahati maana haukuwa wa maandalizi yale,ushindi wa bila kuongea unaweza usisikike,na mara nyingine ukiongea sana wanaweza kunyamazisha,maana wao hawamjui mungu na labda nisiseme hivyo zaidi iwe wanamjua mungu wao.pale unapokosa ndio pale majibu yalipo,ni kama pale unapopata ingawa haitaweza kulingana,ni tofauti ya kuwa moja ni ushindi nyingine ni kinyume yake.

Kile kinachoweza kuzuilika ni kile kisichopangika,maana kitakaaje?kama maji hupita kokote,hata yakaleta uharibu hata ikawe sio lengo kubomoa,pale yanapobomoa yenyewe ushinda ikiwa yalipotoka yalikuja na yakabomoa,labda yangeenda pengine ili ungejua kuwa haikuwa lengo,na iweje yangefanikiwa ungeeiita ni bahati yake,kwa yule anayejenga ukuta kwa ajili ya kuzuia maji hayo anajiandaa,kwa yule anayeyasubili yaingie mpaka ndani basi atafanikiwa,maana amesubiri hivyo,muda mwingine huwa inakuwa haiwezekani,ikiwa katika hali ya kawaida hasa mtanzania ikiwa wengi hatufahamu mazingira yetu,ikiwa ni miili pekee tunayoifahamu,tukisahau mazingira mengine tukataka afya bora,hii itakuja kwa kunenepa ikiwa ni bora basi itakuwa bahati,siwezi kusema sana hapa labda tungeulizana nani au na flani wanapenda nini,maana utofauti upo,na matokeo sio maandalizi,ikiwa yenyewe yakawe na kusudio la kuleta ushindi.

Vizuizi ni haki kuviweka pale unapojiandaa.lakini ni pale tu utakapo jua ni unazuia nini,Katika utofauti wa malengo tuseme yawe yanayofaa yote,yakitofautiana kwa mabaya na mazuri kwani tunaweza kuchanganyana kwa muda mbadala,endapo yale yasiyokuwa ni malengo kufanyika kama malengo wakati Fulani,yule anayejiandaa ndiye anayejua lengo hasa,labda na ije tofauti..hapo tunasema anapanga mungu.
mda mwingine lawama hazifai labda ujue nini unachokifanya,maana kama ni unajiandaa na imetoka kipindi maandalizi yakawa magumu unaweza kuyakimbia endapo haujafahamu unajiandaa na nini, 

'tutaishia kunawa maji ikiwa na chakula tumekiona mbele yetu'.
kwani hata meza zenyewe waligeuza kitambo!!

By:          Benson G, Makaya,
Tel:         +255 714 33 66 57.
email.   bensonsmakaya@gmail.com

Thursday, February 16, 2012

Makaya's Forum: BINADAMU ANAPOTEMBEA..!!

Makaya's Forum: BINADAMU ANAPOTEMBEA..!!: Binadamu anapotembea anaangalia wapi..?maswali mengine bwanaa!!tuseme ni kushoto ama kulia,wale wenye uwezo huangalia kote,hatuwezi kuan...

BINADAMU ANAPOTEMBEA..!!



Binadamu anapotembea anaangalia wapi..?maswali mengine bwanaa!!tuseme ni kushoto ama kulia,wale wenye uwezo huangalia kote,hatuwezi kuangalia kote bila kuwa makini,yaani utambuzi kiujumla kujielewa.
Hatuwezi kusema wote tunaangalia kote,kwani wote sio wale tunaotembea,na hii haiwezekani,ni kweli tunatembea,na ni kweli sio wote.muda wote tuseme sio haki kutendeka lakini ndio inatendeka,hakuna yule atendaye lisilotendeka na likaitwa tendo bora,matendo ni yale hasa tuyatendayo,ndiyo na yote sio mageni,sio yale ya kushoto wala kulia,ya chini yatabaki huko maana hayana haja ya kuyafikia,wengine watasema hawajawahi na kama kutenda ni kuwahi basi wote tumechelewa.

Sio yale tuliyonayo tukimaanisha tumeyatenda,hata kama tumeyatenda si yale tunayoyasema tumeyaweza,yapo yote na tuliyoyashindwa,tunapotembea sio miguu tu kwani hata akili nayo hufanya kazi kubwa mikono nayo pia ikatembee,muda mwingine tutembeze na mioyo yetu.Wengi watu hatuelewani,tumesahau kuwa hata wale wa zamani waliandika,ndiyo wale waliotembea wamefika hadi hapa,waliacha akili zao zinatembea,sasa wengine wakiangalia wanavyotembea wanapofika ni pale walipo,mahala na muda wanautaja kama ulivyo,ya kuwa wapo hapo.Kama matembezi ya maelfu yameshindikana basi hatutaweza yoyote,wataweza wachache,ni kama ilivyo shule kwani chochote kile sio cha kusoma,cha kusoma huwa wanaambiwa soma hapa,elewa pale unaposoma,jua unachokisoma sio kile unachokiona,macho hayadanganyi lakini kwa dunia jinsi inavyotembea haiangalii mwanadamu amesimama ki namna gani.

Tusherehekee vyote na tujipongeze hasa pale tunapoona tumeweza kukimbia,ikiwa ni wengi wanapenda kuwahi,labda tutembee haraka tu tusikimbie,yakuwa hatujui tunakimbilia wapi,tusije kimbilia bomu,bomu hufyatuka endapo pale kunakuwa hakuna uangalizi na yule anayekimbia uangalizi wa sehemu aliyopo ni mdogo sana,tukubari yote ya kuwa tunauwezo wa kukataa yote,kwani hata tukisema ni kutaka ufikiriavyo wewe lazima wengine watakubari huku wengine watakataa,labda tuseme haina haja ya vyote hivyo,watakao kataa na kukubari vyote kheri kwani yule anayekataa njia hii anayo nyingine,yakuwa anataka kupanua uelewa,ili asaidikike atakua ametembea.

TEMBEA UYAONE..

By: Benson G. Makaya,
Tel:  +255714336657.
Email:bensonsmakaya@gmail.com

Wednesday, February 15, 2012

Makaya's Forum: SAUTI KALI...

Makaya's Forum: SAUTI KALI...: Sauti zimezidi kuwa kubwa,zimejaa na chumba ni kidogo,ikabaki ikawa na sasa imekuwa ni mtafaruku,sio mda wake huu,ingawaje kihalisi imet...

Makaya's Forum: ELEWA 2

Makaya's Forum: ELEWA 2 :   Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye n...