Saturday, June 2, 2012

BINADAMU..

B inadamu,tunajua zaidi ya anaye jua’binadamu,tunabisha yale tusiyoyajua,tunayasemea yale tusiyoyajua,tunajifanya tunajua yale tusiyoyajua,mwanzo huu ni mbaya sana,mwanzo huu ni mrefu sana,maana tusipojali muda hata nafasi zitachukulika,pengine tukasingizia kila kitu kina sababu,huku ikiwa hata hizo sababu hatuzijui,tusibishe yakuwa tunayajua,kaa kimya mengine ni kwa Yule asiyeyajua,sio wewe hata mimi sijayajua,ni mengi sana yaliyopo chini ya hilo jua,kama mwenyezi mungu asingeyajua,kuona  mapambo na ua tusingetambua,akili ya mkubwa ni vigumu kwa mdogo kuijua,akili ya mkubwa ni nyepesi mdogo kuijua,akili ya anayejua ni rahisi kwa anayejua,maana hata tukaandika upumbavu tusioujua,pengine itakuwa ni chaguzi kati ya kama mvua na jua,machache tunayasema bila ya kuyatambua,pengine ni hekima kwa nyani kula mabua,yataenda wapi viwanda vilituumbua,wachache wakali wamekuja kuviibua,

Mwacheni mnyonge aje na mvua,maana wababe wamekaa na kuotea jua,litakuja joto tutasema moto,tukikosea kusema kuwa kama watoto,simaanishi hivyo mengine ni yangu wala sio ndoto,tunafundisha sana mashairi kama mrisho mpoto,na tutaimba sana bila mtoko,ijazane dunia pasipo viroboto,iwepo dunia palipo na watoto,nay a wakubwa yakabaki huko,mbali sana haina haja ya kuitana,si karibu sana kwa vile mmoja kufikiria,ukubwa ndiyo ubinaadamu maana tumekosa kwa mengi yaliyona uzuri na hata yasiyo na uzuri ndani yake,hapo tukapoteza mitoko,hapo tukakamatwa na joto,hapo tutakanyaga moto,hakuna anayesikia kama Yule anayeelewa,tusindikizane hivi kwa namna ilivyo..wala hata tusijari na hiyo mioto.

Dunia inakwenda kule inapoelekea,dunia inajizungusha katika njia zake,maana pasingekuwepo njia haina haja ya kutembea,pengine tutakimbia wapi wakati njia yenyewe ni mbovu?tutengeneze njia na zenyewe zikatutengenezea mahala pazuri,maana ule mti mkavu ndiyo wa kushukuliwa na kabati,hata vitanda pia,ule mti mkavu ndiyo ule hasa usipate jema mwanzoni,kwa kuwa wenyewe unakuwa mkavu,si kwamba hauna maji bali yale yaliyopo yametosheleza shina,ikiwa na wenyewe unaweza kushika moto,baadaye ikawa ni heli kwetu pale tunapotaka moto,pengine moshi utakuja kwa miti hii mibichi,tukiachana na moto kuna moshi,hapo hatutaona,hapo hatutaonekana kana kwamba hata kuna njia,tutabaki kutengeneza nyusi tusijue wapi macho kuona,tusielewe nini na wapi pa kuelekea,tukabisha kwa kujifanya lakini kwa ukweli utaeleweka.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...