Friday, June 1, 2012

LULU-(Toleo maalum)

Zaidi ya vile upendo wangu kwako,umezidisha nafasi na namna ya kuweza,
umeniwezesha pale palipokuwa pagumu umenipa ujasiri hata wa kutokukwambia,
maua mazuri yanamwagiliwa japo ulifanya kujimwagilia,
umekuwa kiongozi wa wale wengine na kwangu pia,
hakika ntakupenda daima,kuwa na mimi karibu zaidi nizidi kuelewa,
ni mwanadamu gani asiye na hasira au za kwako usifanye mbele yangu,
ni heshima tosha,ni ujumbe tosha,umefanya yaliyokutosha 

haki akienda mtu tumwalakishe awahi maana nafasi zinajaa,
watu wanataka kumiliki vyao ikiwa baadaye isiwe taabu,
usinifanye nilie zaidi kwani yanatosha nasema tena,
nimekupenda kukupenda,nimefurahi kukupenda,maana pengine hata kwa mwingine isieleweke,
tujaribu kuinuka pamoja,tujaribu kuwa pamoja si kwa mda huo tu uliopangwa basi tuendelee,tukue,tuzidi mapana yaliyokuwa na ncha,
yasiyokuwa hata isiwe kwetu wakali,

maisha kuyatoa kwa mwana ni vyema kuliko kwa mwana,maana zikazalika ili jambo lile lije,ama kweli wewe ni mama yangu,ama kweli wewe ndiye unanifaa kukupenda,
pengine ni muda wako,pengine ilistahili kutokea kwa mara ya kwanza,
maumivu unayonipa si haba pale napojaribu hata kushika simu na kukupigia,hapo ninakuwa nimekumiss yaani kukumbuka,nakukumbuka sana mpenzi wangu,huwa nakukumbuka sana uwepo wetu wa pembeni,maana huwa tunazungumza sisi tu,
sisi ndiyo kumetufanya tuwe hapa,tumefika bila kujali vitu,ingawaje umekuwa kama ngao lakini ujasiri wa kuyachukua maisha yangu pia umekuwa nao,maana asidanganye mtu kwa kusemea mwingine,
fikiri hayo haraka kwa kuchagua wengine,
maana wa leo ndiyo asili,wa leo ni wa leo tu,wa leo ndiyo ametimilisha haya,mama yangu mpenzi umenikuza,baba yangu mpenzi umenilea,ndugu zangu wapendwa tumekuwa pamoja,
maana kuna kukosea na tukasema pale ilikuwa vile na sio ulifanyaje kwa kutaka kujua,umebaki lulu kwa yote,umekuwa dada yangu mpenzi,
sasa na milele ntazidisha mapenzi

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...