Friday, June 1, 2012

SIJUI..

Kwa muda mwingine huwa nawaza niandike nini lakini kwa sababu zingine huwa nawaza kwa nini sababu za nini?maana mengi ya duniani ndiyo ya vinywani,mengi yakusemeka,mengi ya duniani ndiyo yale kawa maandishi,pengine tukajua huko.pengine tukaona ni nini kipo huko,tukisema sasa tumerudi hapo tutaulizwa tulikuwa wapi,hapa tuweke sababu,hapa tudanganye tena ikaaminike,isije aminika ya kuwa ndivyo ilivyo bali iaminike ya kuwa ndivyo ulivyo,sio kutafuta ni kufanya,sio kufanya ikaeleweka,sio kueleweka ikawa imetafutika,hapo sababu zitakuwa nyingi  sana,hapo tutashindwa kujiuliza na kujiuliza na kujipa majibu,tena ndiyo haswa tueleweke kama hatujaelewa kwa maaana ya kushindwa tena labda hatukusoma  vizuri ama yalikuwa tu hayaeleweki kwa kubisha,sisi wengine ni wabishi sana,sisi wengine ni watata sana,hata kama maneno yanafanana,kwa machache lazima kuelewana.

Muda  hauji ukaja ukasema,muda unasema wenyewe kwani ni lugha nyingine pengine wakaelewe wale waizungumzayo lugha hiyo,katika kujifunza kuna kujua endapo mtu amefahamu,akiwa amejua au hata amehitaji kutambua,najua tumechoka sana,pengine tukiwa tunahitaji lakulifahamu kulingana na huo muda,pengine ni sisi wenyewe wa kujifahamu maana hata huo muda ukawa hauna maana,kwa kuwa mdogo ama kupungua katika yale yanayotakikana

Hakuna mtu anayependa kuchelewa kama sio kuwahi sana.pengine watu wameshangaa kuona mwezi wakati wengine wakiwa na hitaji la jua,wakilitafuta kwanilinasikika tu,wengine wachache walilliona wale tunawaita wazee tena wazamani maana siku hizi kuna wazee wakisasa,hapa sijui tuliuchelewa  muda ama tuliona tofauti,au pengine ndiyo namna halisi ya ilivyo..ilivyo maana na namna ya mtu akatambue akaishi vipi,ilikupata moja lazima kufikiri na mwisho,kwani sio tatu pekee ni bora,hata kumi pale ikawa bahati nasibu.na hapa watu wanabahatisha sana na kusema wameweza,hiyo ikiwa ni imani ya kutaka kuweza na kushindwa.

Mwisho wa kumalizia ndiyo mwanzo wa jambo,ikiwa tu limeonekana,limesikika hapo kutakuwa na mwisho na mwanzo tusiufahamu,tena tukasema kwa yale tunayoyafahamu na kuyaweka kweli,hapa huwa tunaongea sana,huwa tunajiona tumeweza tusipojua hitaji ni tofauti maana tusingeweza kuwaza pamoja,hapa isinge kuja ile namba moja,ikiwa hivyo tunahitaji umoja,maana kwa umbali tusijifanye zaidi hata tukasikilizana,hapa lengo ni kuelewana,kwani hata ingekuwa namba zinajipanga zenyewe sidhani kama mbili ingependa kukaa nyuma ya moja na wakati yenyewe ni kubwa,fikiri kuwa na nyumba mbili na mija pale unapohitaji,pale unapokuwa na kitu chako kimoja fikiri mbili kuwapo kama si furaha ndani yake,labda isivyo amani kwa yale mabaya kwa mwengine.tumalize kwa kumaliza.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...