Tuesday, November 20, 2012

MAPENZI YANAISUKUMA DUNIA..



Usipoelewa hautaweza kujua hata kama unashiriki vipi maana kwa kutokuyapenda na kujifanya unajua zaidi kujikuta unaumia bila faida,katika vitu na watu wanaoisukuma  dunia ni vile na wale wanaojifanya kujua kila kitu,unaweza ukawa unafanya sahihi na usikute lolote limefanyika,pengine hata nguvu za kusukumia zikawa hamna,kwa  kuwa mwenye nguvu umesahau kuangalia akiba,usipojua nini kupenda nini utafanya,wengine huwamo ni kwa sababu ya kuvaa,pengine nguo zikichanika hakuna jipya litakalo tokea,maisha ndiyo mapenzi na mapenzi ya mtu anayeishi yasikufanye mwanadamu kutokuujua wakati wako.

Hakuna mtu aliyekatazwa kupenda lakini fikiri kwamba utapenda nini au wangapi?wangapi umewapenda?je kile au yale mabadiliko unayoyataka yametimia?penda unavyoweza ukielewa unapenda ili uishi,maisha yaliyojawa na upendo ni maisha thabiti kama umeyaishi usijaribu kuyaacha zaidi ya kuongeza,ikiwa kumpenda mwenzako ni zaidi ya kujipenda wewe mwenyewe,haukatazwi kujipenda zaidi,ili mradi kwa mwenza kisiwe cha ukaidi.

Hautakiwi kuishi kwa taabu kwa sababu ya upendo,upendo hautafutwi kama inavosemekana,upendo umezaliwa kwa kila moyo wa mmoja wetu,unapochagua kufanya jambo fikiri kama umelipenda,fikiri endapo una uhitaji nalo ili inapowezekana kufuta baadhi ya uchafu,maana moyo ukiwa msafi hata uje msafi ,usafi utabaki pale pale,upendo ni asili ya mtu,jinsi ulivyo,usikimbie kimbia ya kuwa ni lazima kupenda,ili mapenzi yakatimie,maana unaweza kuisukuma dunia ya wengi na kuacha yako.hapa nasema umependa pasipo pendeka.

No comments:

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO : Watakwambia unabahati kwakile ulichokifanya kilichokufanya uwepo hapo,kujipa ufalme na kuzungumzia maisha...