Wednesday, January 24, 2024
Makaya's Forum: ISHI NA YAKO
Makaya's Forum: HASIRA YAKO
Tuesday, January 16, 2024
HASIRA YAKO
Unakasirikia maisha yako wengine wakiwa na furaha,ikiwa lengo si kutaka kuijua furaha ya mwengine bali kujua ni namna gani hasira zako zinakupeleka,binadamu tupo tofuti,mmoja hali nyama ya mbuzi kwa kuwa inamtoa vipele mwengine hali nyama ya nguruwe kwa sababu ya dini sasa nikikasirika usiniulize nimekasikia nini,nina mengi.
Kasirika,usikarike pasipo na
sababu.upumbavu wa mtu mmoja usikufanye uvunje simu na mwengine kufikia kumkata
mtu panga.angalia unapokasirika sauti yako ya ndani inakwambia nini na kabla
haujatenda kwa kutumia kiungo chochote cha mwili yakupasa kutafakari,maana kuna
wale wenye hasira za ndani(chuki) hawafanyi mambo yao hadharani.
kama ilivyo katika michezo
mmoja akamchezea rafu mwenzake basi wanamichezo waliiga kwenye maisha,na ndiyo
maana unasikia michezo haiitaji hasira,ukisusa wenzako wanakula na wenzako huwa
wanakula mpaka baadaye ukakitamani tena hicho chakula,kasirika vizuri.
Dunia hadaa utakasirishwa
wakitaka kujua maamuzi yako,ukishajua umekasirikia nini maamuzi yako yawe
tofauti na hasira zako kwani kweli maisha yana mengi lakini kuna mengine sio ya
kukasirikia fikiri mtu anakasirikia mafanikio yako na atayekumbatia maamuzi ya
hasira zako yampasa kuwa yeye.
ISHI NA YAKO
Watakwambia unabahati kwakile ulichokifanya kilichokufanya uwepo hapo,kujipa ufalme na kuzungumzia maisha ya mwengine kwa kuwa umefika mahala fulani,tambua maisha yana stepu,uliyopo sasa mwengine alipita juzi ukicheka leo mwenzako kulia ni sawa na kulia wakati mwenzako anacheka.
Usibabaike na waliowahi
kufikia ukitakacho,tambua muda wako ikiwa unajiandaa jiandae vyema ili ukikosa
isiwe lawama kwa wengine,maana imekuwa mmoja akishindwa akatoa sababu za
mwengine kumuangusha.
Usifikiri ni raisi kukaza
jambo,kuna mengine yanakaza mpaka kufungua inakuwa kama ni kukaza,ujiandae
vyema maana kuna vilio,maumivu yasiyo na machozi na hata usumbufu
usiohitajika.yatambue magumu yako na jipe muda kuyatatua ikiwa humu duniani
wote mpaka muda huu tunatafuta maisha.
Kheri udongo unarudi utokapo
maana ingekuwa foleni kubwa barabarani kwa kuwapa heshima wajionao
miungu,usifikiri wakati wa magumu peke yake mwishowe ukawapa lawama watu wasio
husika na maisha yako,tambua nafasi yako si ile aisemeayo mwengine,watu huwa wanaongezea
kwa kile ulichonacho.
Makaya's Forum: ELEWA 2
Makaya's Forum: ELEWA 2 : Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye n...
POPURAL POSTS
-
Makaya's Forum: ONA KUSIKIA. : Mapema ni kheri kuona bila ya kusikia,maana haya machache tumeyasikia hapa kwa kuwa yalionekana mwanzoni,...
-
Makaya's Forum: ELEWA 2 : Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye n...
-
Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...
-
Makaya's Forum: NI SAWA.. : .......tunapokwenda ni sawa,kwa kuwa kila siku kadri ya zinavyokwenda mwanadamu anaishi katika ile hali ya k...
-
Sauti zimezidi kuwa kubwa,zimejaa na chumba ni kidogo,ikabaki ikawa na sasa imekuwa ni mtafaruku,sio mda wake huu,ingawaje kihalisi ime...
-
Unapokwenda ni sawa,kwa kuwa kila siku kadri ya zinavyokwenda mwanadamu anaishi katika ile hali ya kutokusema kwamba!! na sio haielewe...
-
» Most people with personality disorders have what is sometimes referred to as "disorders of the self," because they often do...
-
Makaya's Forum: MFUMO.. : Leo tumetaka kuongozwa na nani maana inaashiria mfumo unapajua unapoelekeza ,pengine ikawa vyote ni vya kija...
-
Makaya's Forum: SAUTI KALI... : Sauti zimezidi kuwa kubwa,zimejaa na chumba ni kidogo,ikabaki ikawa na sasa imekuwa ni mtafaruku,sio mda...
-
Ningetaka kulia ningejifungia maana ingekuwa haina maana kuonyesha machozi hadharani,kwa kila mtu akiuliza unalia nini maana wata...