Friday, February 3, 2012

TUNAWAZA KUKOSA,TUSIPOJUA NI VIPI TUMEPATA..


Mawazo ni sehemu ya maisha ya mwanadamu,katika kupitia na kufanya vile au kile ilivyotakiwa.Kuna mengi ambayo mwanadamu anaweza kuwaza ikiwa  ya furaha,kejeli,chuki,upweke,na ya ki kawaida kabisa,mawazo huweza kurudisha na kukamilisha mipango au malengo ya mwanadamu ikiwa sahihi pale anapokuwa na utambuzi zaidi.

Kweli inapasa utofauti,ikiwa wengine wako kawaida basi na sisi tuwe,ili ikaonekane tofauti kwa wengin,labda tuseme tumepata ikiwa ni mvuto wa kupata na vingine,vile ambavyo yeyote yule anavyo kwa miliki ya uhalisia wowote,ikawe na maana ya maamuzi kwani yeyote anayeishi anayo mawazo,katika yote na hata yale asiyoyaomba,juzi hapa tulifanikiwa kama mvua isingeendelea kunyesha,kumbe hatukufanikiwa ila ilipasa kwa mwelekeo wa mienendo na shughuri zilizokuwa zikifanywa ziliashiria jambo,ikiwa kila mwanaadamu anaukaribu na yaliyobora yake,na sio kwamba tulifeli sasa,labda tumefauru tofauti,mda mwingine uhakika tunakuwa hatuna ni kwa sababu mengine mambo yanakuwa ni ya wengine,hatutaweza kuyafuatilia ya wenzetu na yetu tumeyaacha chumbani,hapa tutajiongezea mawazo,labda tuseme tumeweza kuyafuatilia ya wenzetu na yetu tumeyaacha chumbani,haya mengi sana yamechanganyika na ya watu..na hii ndio hufanya kushindwa,au hata kufauru ikiwa lengo,asiyependa upumbavu ndiyo yule anayetaka maana,kile kinachoingia hakiingii hivi hivi ni lazima kiwe na njia,na kama walisema tusikie na tukaziba masikio yetu basi hatutaelewa vizuri kwani yaliyosikika si yale yaliyoonekana mdomoni.

Katika kufanya ni kunatokea na kile unachokitaka kitokee,kama hatutajua ni namna gani tumevifanya basi hata tunapovipata tusiseme ni sisi tumefanya,maana wapo waliofanya ndio wakasema tugawane,kwa yule aliyegawa..ikiwa anaye gawa anagawa chochote kilichomzidia,ikiwa tumemwita mwenzetu mmoja na kibri ni lazima tuelewe kimetoka wapi,isije ikawa ni chetu maana chuki hugawika kwa upendo,tukawapa wengine wasiwe na hatia na kwa uzito tu ikawe kujibu kwa mitetemo,yule akaonekana muongo kwa kutetemeka,tuache kufanya kufahamu herufi kabla ya maneno,maana hayo yakiunganika yatatuangamiza zaidi.mwanadamu amependa basi amepata ikiwa alitafuta,tutafikiria yaliyo sahihi na mabovu yataendelea kuharibika,kwani malengo yapo,na nani anaweza kuyafuatilia,kwa kutokujua idadi maana tungesema ni mengi,au machache endapo yangehesabika,hivyi vyote hata ikawa hakuna lolote yaani hakuna cha kuhesabu hata vingi vikawa idadi,mwanzo ukigundulika mwishowe hueleweka,mtu anaposema pole sio kaumia yeye,

Yale yaliyopatikana sasa ndio yaliyokosekana mwanzo,yakiwa na ukosekanaji pale palipo na uhitaji,haya mengi sio ya kuyasumbukia labda iwe imeeleweka hayo ni mengi kiasi gani,tutasaidiana sana lakini tutafikia tofauti ikiwa usaidizi mwingine haufanyiki baada ya kusikilizwa,na ndio baadae tusiseme yale ni ya Fulani na haya ni ya nani,vichwa vitauma endapo dawa zitaonekana,maana bila hivyo tena wanaadamu watahitaji kula nyama ya  mwanadamu mwenzao,tunaweza tengeneza njia ya msitu wa miba,,haiwezi kuonekana njia ikiwa wale wengine walikataa kusikia,hatutaweza kuyafikia ikiwa tu tumekaa na kushindwa kutembea,yule anaye tembea anajua mengi,maana atakuja hata nyumbani akikwambia ana njaa,njaa haijatokana na kazi za huko ya kuwa mwanadamu ni lazima ale.labda iwe na awe ameelelewa hivyo.

Yawepo,yasiwepo yatatafutwa.
Lengo ni kuyapata!!

By:Benson G.Makaya,
Tel:+255714336657.

Wednesday, February 1, 2012

LENGO NI KUYAELEWA.


Lengo ni mambo au vitu ambavyo mwana adamu anavyomiliki katika akili au fikra yake ikiwa ni katika kuyakamilisha yale ambayo yana kusudi katika upande wake,katika kuelewa mambo au vitu ni lazima tujue ni sababu gani au ni katika namna gani ambavyo hivyo vitu tunavyovihitaji vinaeleleweka,ndipo hapo inahitaji wote tupaswe kuelewa,hapa tuelewe,ni lazima tuelewe vile vilivyo katika malengo yetu.

Katika baadhi ya mambo kuna yale mabaya na mazuri zaidi mengi hasa pale lengo linapotimia,yale mabovu ndiyo haya mazima katika upande mwingine,na yale tunayoyasema ni magumu ndio hasa yanayohitajika,ikiwezekana.tunayoyafikiria ni mengi mno,ikiwa yamo yote hasa zaidi tunapoyasema nayo tukayajumuisha,

Hii yote ni katika kuweza au kuelewa jambo au mambo,kadri siku zinavyoenda wanaadamu tunapaswa kujua zaidi,ikiwa ni kuongeza ufanisi na uwezekano wa nafasi endapo hata ikatokea isiwe ni tofauti ya vile malengo yetu yalipo,hata kama bado hatujapanga tufikiri nini kitakacho tusaidia,

Angalau kwa sasa ili na baadae wakafanye wengine mazuri yale.Lengo sio kubishana,sio tu moja na likaeleweka,tuyatafute,tusiyafuate,tuyatende au wengine ndiyo watende,ikiwa tu kwa umoja imeshindikana,tuone kwa yale yanayoelezeka na yasiyo elezeka,lengo ni kuyaelewa,yote yanafanana ingawaje yote yakawa ni tofauti,vile vilivyoumbwa kwa mfano ndiyo vile vinavyoleta utofauti yaani vile vilivyopita katika mikono yetu sisi wanaadamu na tukavisema kwamba ni vyetu,

Tukiwa na maana halisi ya chanzo na mahala Fulani yalipotokea,kimsingi ili kukuchanganya ni lazima tuelewe ni wapi palituchanganya,ili mwalimu asiwe na kazi kubwa ya kurekebisha au hata kuacha tuangamie ya kuwa tumekuwa wagumu sana kuelewa.

Usitumie nguvu wakati uwezo unao,ninaposema usitumie nguvu sio kwamba usishinde njaa wakati ni wazi uwezo hauna,kwani ikawa hivyo ni dhambi za kuiba zitaongezeka,na ikiwa lengo ni kuyaelewa kwa wenye dhambi hufurahia majumuisho,kwani yaweza kuwa utajiri pia.

Kushiba kwa moyo ni kuridhika,kuelewa ni pale akili inaposhiba vyake pia,pale aelewapo mmoja sio lazima na wa pili afuate hivyo,tuogope wengine wasije wakazidisha maana na wao ni furaha yao kucheka wengine,kama inavyokuwa hakuna njaa inayoshindikana kwa tumbo,kwani inapozidi na yenyewe huuma,hapo ikiwa inataka kutambulika kwa lengo lake.

Tujenge madaraja yaliyo imara,kwa upande mmoja wengine tutadhani tutapita sisi tu,wengine labda watajenga ya kwao,ikiwa na sisi tuliyojijengea hatuwazi tumejenga wapi,isiwe tumeelewa tu utofauti wa tumbo na moyo kiuhalisia,ni kama pale iwapo shida na raha ikatokea,pale baadhi wakidhani shida za mmoja ndiye raha zake,ikiwa kwa wao hizo zinaweza kuwa ni raha,lakini yote ni malengo tu,na labda tufahamu shida zipo tu labda iwepo kuna unafuu.

Kwa yale moyo uyapatayo ni rahisi zaidi kuliko haya mengine niyasemayo,tusifahamau pale tunapohitaji mabadiliko,fahamu ziwepo na hasa zikawe ni suluhisho pale mabadiliko yanapotokea kwani tuna haki ya kuyafahamu mabadiliko hayo kabla,tunapojua tunaelewa,kuelewa sio kufahamu,kufanya ya kuwa vile si hivyo,au hivi ilivyotakiwa lengo ni kuyaelewa,yote ni mambo,ule uzuri au ubaya ni utofauti,kama vile chafu na safi,au kueleweka ama sio kueleweka,chaguzi ni lako katika nzuri au tofauti,chafu au safi ikiwa ni kueleweka ama la.tufanye yataeleweka tu,kwa Yule aelewaye yawe yanaeleweka tu.

Lengo hili halikuwa langu,ikiwa limeonekana katika upande mwingine ni lazima uelewe  maana usibishane ingawaje hatujaambiana,hili au lile liwe lengo letu tena tulilolikusudia,lengo letu linapokuwa moja si kwamba wewe utafanya vile mimi nitakavyo fanya,au tutafanya pamoja ikawe mwalimu akasema Fulani ame nakili kwa mwenza,tuyaelewe na tuone utofauti wa malengo yetu.

By: Benson G.Makaya,
Tel: +255714 33 66 57.

Tuesday, January 31, 2012

MENGI YAMEDONDOKA.


Ikiwa ni kutoka juu hadi chini,chini hadi chini kabisa au juu kwa juu huko huko,pale pasipo kuwa na uangalifu mzuri na mara nyingine ukaseme ni bahati mbaya,Yaliyokuwa yameshikiliwa ndio sasa yanahitaji msaada,maana hata wale walio kuwa na nguvu wameamua kuachia,yanayodondoka huwa hayasemi zaidi ya yale yanayoshindikana.Kwa nini kama kudondoka tusingedondokea juu huko huko,maana yule anayedondoka akiwa chini yeye hubaki pale,na kwa yule aliye juu ikawe ni mshangao mkubwa tena.

Ikiwezekana umesahau maneno yetu ulipokuwa mtoto tukiyasema na ndiyo maana imefika muda shikamoo zimezidi,sio kwa utani lakini muda umesogea,angalia tusije kuwa sisi ndiyo wazee,kwani watoto wanazo zao,na kamwe mtoto hawezi kulingana na mtu mkubwa ikiwa hata anaumwa,ukumbuke ile ngoma ya watoto inakesha kwa namna yake,yale ya zamani yamekuwa ya kisasa zaidi,hawakua na mambo ya ujana ambayo yapo katika kipindi hichi na yanamaliza nguvu ya taifa,ingawa ilikuwa ni kipindi cha ujana wao.

kwa sasa wazazi wanashindwa kufanya lolote na watoto kukua katika namna wawezavyo wao,hatukatai mtu kuwa mzungu,kuwa mwarabu,lakini ni lazima mtu anaye taka kuwa katika jamii tofauti na yake ajielewe yeye,ajitambue ya kuwa hakuna muda wa kufananisha zaidi ya kufanya,yakuwa mwanzo unaonyesha mwisho upo katika namna zipi,njia hufanya mwanzo kuwa mwisho mara nyingine,kwani inapaswa kuurudia kwa makosa machache yanayotusibu katikati ya safari yetu ya maisha kabla hatujayamaliza.

Wale wanaotembeza sio wale waliopendeza,ikiwa haikusemeka hivyo,uzuri kila mtu anao wake,tukiambiana watu ni wabaya basi itakuwa ni vita ya kuutaka uzuri kwa lazima,tukiwa tunatoka safari tuangalie mizigo yetu tusije kuisahau nje,maana na wachache tukaonekana tumependeza wanajua tunapesa,tumefanikiwa kumbe ni tumefanya ili kuweza kutembea vyema,maana wachache hawachelewi kukwambia umepungukiwa akili,ila wakifanya wazee si mbaya kwani ndiyo walivyokuwa navyo na walitembea hivyo.

hata ikiwa akaja mgeni na kubisha hodi,mshikishe jembe huyo,mwambie ndani wasafiri walipaki vyao na wamelipia pesa nyingi ikiwa hawataki usumbufu,tukalime na hao wageni maana si wamekuja na majembe wenyewe?angalia unapofundishwa na mwalimu mgeni,kwani lazima ujiulize wa kwanza yupo wapi?kama kashindwa uangalie Yule aliyeweza,muda unapita na utakao fuata ndiyo wetu maana sisi ndiyo wazee,na usikubali kuacha mafao maana utasumbuliwa tu,taarifa za mbali zinaweza kuja zikiwa zinatuhitaji na lazima ujiandae kwani ni sisi wa kuongoza,umwangalie sana Yule mzazi wa mtu mwingine anapomwambia mwana wa mwingine kuwa hana adabu,ikiwezekana ijulikane kama adabu yake ni nzuri ili tuache za wazazi wetu.
‘sio kila kitu wazee’.


By:Benson G.Makaya,
Tel:+255714336657
Email:bensonsmakaya@gmail.com

NAMI NIWEMO.




Ikiwezakeana sura yangu iwekwe kwa kaisari,kilichoniweza ni kile nilichokiongeza,cha kwanza nilikuwa nacho mapema,ndiyo maana ya kuja na kusema,ni maongezi nikifikiria,pembeni haina haja ya kukuitia,tuongee pamoja tuelewane tusije jutia,ni mjita wa suguti mara musoma nimetokea,muda wote haina haja ya kuitajia,tumefanya vingine kwa waliotofauti ikaeleweka,wale wachache..tusiotaka hongera kwa makosa yetu,kila mtu anayafahamu ya kwake!! inanikumbusha kulee,kule kwenye sura yangu,angalau basi tufikiriane ndugu zangu,labda nimesema hivyo hata nikiwa nina nia mbaya,wala si uongozi wangu utakuwa mzuri,ubaya wangu hautadhuru lolote ni mimi na uongozi wangu.Labda tufahamishane kwa hili,nikipata nafasi ya kupiga picha ntapiga kama ile katika shilingi mia,moja ile ya upande fulani,muda unavyoenda tutachaguliwa wake ,maana naona nguvu zetu zinaisha,viwili kwake chake,moja kwetu vyetu,hii ni mbaya ikitokea kwetu,labda tusijue nini maana lakini ombi langu ni hilo,moja..hili la sura yangu kuwapo pale,najua ntaweza ikiwa sijafika hapo waje wawaambie,zikiwa kama hadithi kwa wale watakao chelewa sana.

Tusitake maisha ya kurudi utoto bila kujua tutawarudishia wapi watoto wetu,maana tuwape na njia ili wale wenye watoto wengi wengine wajisaidie,hata kama ni njia na zenyewe zimekuwa ni nyembamba zikihitaji nguvu ili kupita,tukisema kukonda ili kupita vyema wao wanasema tumepata ugonjwa wa mawazo na tukinenepa inakuwa vibaya kwa mapitio,itabidi tutafute njia yetu.kilichozidi zaidi lazima kiwe na sifa yake iliyoongezewa zaidi,ni kweli maisha yalikuwa ni magumu lakini hii iliyopo ni zaidi,hakuna asiyejua kuishi labda asikuelezee,yale tunayoyataka yataleta maafa,nikiwa sijui maana yake labda,niseme maswali ya dunia nakumbuka kauli hii nilipoulizwa kwa nini maswali ya dunia jibu likaja ya kuwa hilo nalo ni swali la dunia,hatuwezi kwenda na maswali huku majibu tumemwachia mwengine,maana kama ni shule zimekuja hadi za lugha tofauti,hili si kosa kwani shule ni kujifunza na endapo unataka kujifunza unatakiwa kujifunza kitu ambacho wewe unataka kujifunza,haina mshangao ila ni ya kustaajabisha sana shule watu tumeenda za nini?maana ionekanavyo tu wengi sana tumesoma na maswali yakiwa hayana majibu.

Labda kama sijamaliza lengo lieleweke,maana inaweza kutoka picha tofauti na ndugu zangu wakasema 'tulijua sisi' ,wengine humaanisha vyao daima,bila ya kumjali mlengwa,hakika matangazo tunayaona,tumejitahidi kulemba sura zetu zikiwa na ujumbe mbalimbali tofauti,hiyo yote ikiwa ni kushawishi,hapa napo tunashawishi lakini imekuwa ni namna tofauti,kwani lengo hapa ni uwepo wa sura tu mahara pale,pengine hata nkikumbuka kwa kipindi kile waswahili ndugu zangu walikuwa na usemi juu ya upendo ingawa unawezekana bado ukawepo,nakupenda sana nikinywa maji nakuona kwenye glass,yaani mzungu hapa anakwambia ‘indeep’,huu ni undani..ingali bado tunaendelea kuishi basi ukawe undani wangu mwingine.tumalize na hili...

‘Ikiwezekana sura yangu ikae katika shilingi’

By: Benson G. Makaya,
Tel: +255 714 33 66 57.
Email:bensonsmakaya@gmail.com


Monday, January 30, 2012

Makaya's Forum: TUBADILISHANE KILE TUNACHOKIFANYA,NA SIKU !!

Makaya's Forum: TUBADILISHANE KILE TUNACHOKIFANYA,NA SIKU !!: Yanayofanyika ni matendo,kwa mtenda ndiyo ikafahamike haswa,ikiwa naye mtendwa akifaahamu zaidi kutoka kwa mtenda,yaani ilikuwaje?sio mawazo...

TUBADILISHANE KILE TUNACHOKIFANYA NA SIKU


Yanayofanyika ni matendo,kwa mtenda ndiyo ikafahamike haswa,ikiwa naye mtendwa akifaahamu zaidi kutoka kwa mtenda,yaani ilikuwaje sio mawazo haya ya kila siku uliyonayo lakini ndio baadhi yanayopelekea kutenda,yote ni matendo tu,ikiwa siku zinaenda wengi wetu ukiendelea kufanya vile unavyovifanya ili mradi siku ikapita,ikawe ili mradi sio tu ndiyo yapite bure,bure isiyo ya pesa,bure ikawe ya kutokufanya jambo kwa siku hiyo,kwani kama unabadilishana vinaenda wapi?yaani hivi vibovu na yale mazuri kwani kuyafikia na yenyewe yanahitaji siku iwe nzuri,itakavyo kuwa ndiyo jinsi ya kuelewa ielewekavyo,

Utasumbuka endapo ukitaka kubadilisha mazuri yawe mabaya,kwani ni uadui utakuwepo hapo,usije kosea na kubadilishana hewa,ili kesho ukapumue na wakati unazo tokea kuzaliwa,kipindi na cha kukifahamu ili ukabadilishane na vile vizuri,maana kipindi hichi kimekuja kinamna nyingine,siku hizi sio kama za zamani,wale wa zamani wanajua hilo yaweza kuwa nao hawaelewi kipindi chao,maana siku zao walibadilishana vyema,ikawe mbuzi kwa ng’ombe,naye mfanyabiashara akalizika kwani alitafuta mbuzi ili abadilishane na ng’ombe.

Ikiwa ni leo sijui kesho kutwa itaitwaje,maana mabadiliko yaliyofanyika ni ya leo tu,kesho ilisemekana watakuja wengine,lakini nao bado hawajaandaliwa ikiwa nao wakija wataanza yao,hata ukawa ni upepo ni lazima ujue unavumia wapi,ikaja hadithi uwahadithie ulikuwa unatokea pande ya kulia na kuelekea kushoto,zote ni pande nzuri labda iwe ujiamini leo na kesho,hapa ukitaka kufahamu ubora mwingine ulio wa zaidi ya leo na kesho.

Siku ni muda,kesho ni siku ya pili,muda huu ukauite wa kwanza ikiwa unategemea wa pili uje ukiwa umejiandaa kwa muda huo au useme muda wowote,usifike mbali wakati mwanzo unaonekana,ikiwa anayeanza hufikiri mwanzo bora iyo ikawe siku,maana hata kesho ikija itakuwa na yake,yale uliyoyapanga na haya mengine yatakayokuja,lazima yaje kwani wengine wanakufikiria kwa yale ya kesho na sio leo,utatafutana huko na usipokuwepo watakutafuta wakufunike,kwani hata walizani wao wamelala wakaandaa na mashuka kumbe yalikuwa ni yetu,unaposhindwa kurudia mema na kusahau mazuri ni kama pale unapofikiria yale maovu yaliyotuumiza siku za nyuma,yule anayefanya kazi bila kuomba mshahara anategemea kulipwa mengi,ikiwapo na mshahara wake mwenyewe.maana hakuupata,na hakuna kazi isiyo na mshahara,labda siku zipite ili ujue nini haja ya mshahara,tena sijui umekujaje baada ya kufanya kazi.

Wanaopaka ina wakiwa na yetu majina ,siku zimepita nyingi mengine yafutike,ikiwa mengine sio ya kuyatendea,utajiuliza kama ni kweli zimepita,bila kukanana pengine huwafahamu wasichana,kwa urembo wazee kuonekana vijana,hata ya jana yasingewezekana,muda mwingine inakuwa ni kujifunza kwa kuchanganyana,siku za zamani watoto ndio walieleweka kutokujua,maana nyingine hata hizo zilizopita zinaweza zisifike kwa wale wenye watoto kujisifu ikiwa ni wana wazazi kama wao,siku zinavyozidi kwenda utafahamu tu,labda uchelewe lakini ni lazima ufahamu ingawaje mpaka sasa umechelewa.

Lengo ni siku kupita,iwe imeeleweka kinamna yeyote.yule anayesema ameelewa vile aiambie siku yake,maana ndicho kitakuwa cha muhimu kwake..

By: Benson G. Makaya,
Tel: +255 714 33 66 57.
email:bensonsmakaya@gmail.com

Sunday, January 29, 2012

HITAJI,,


Hitaji huwa linatokana na mtu mwenyewe,nafsi yake na mapendeleo ya kwake.Pale mtu anapohitaji liwe la ulazima ama si la ulazima katika mazingira yaliyo au yatakayo ya ulazima ikiwa na maana ya uwekezaji,yale ya hasara hakuna asiyeyapata labda tusikitike kwa kupoteza watu kwenda kuwa wafu na isiwe hasara,hiyo mitazamo inatokana na kile kilichomo kichwani na sio mwilini,maamuzi yanatokana na mtu pamoja na nguvu zake,pale nguvu zinapotumika tunaweza kusema maamuzi yalichukulika mahala Fulani,Ni wengi wetu tunaohitaji,hii haitokani na kwamba mahitaji ni ya lazima,mahitaji mengine ni yale yanayotupelekea kuhitaji.kuna kipindi mwanadamu hutenda katika mahitaji yake,hii inaweza ikawa ni kwa ulazima au ombi ikiwa mahitaji yako yamekulenga wewe mwenyewe.

Bidhaa zinapouzwa zinataka bei,ikiwa unahisi kulaliwa bei..usiuze,kwani yaweza kuwa matokeo unayoyahitaji siyo yenyewe.Isiwe lazima kumfanyia mtu mahitaji yasiyo kuwa na ulazima kwako.Kwa makusudi yapi sasa?pengine tunawaza tukiingojea samahani au itakuwa ndiyo mahitaji ya kutumia nguvu,maana lugha nyingine hutumika kurahisishia mambo,zikiwa pamoja na samahani,wachache tukatumia lugha hizo tukijua bado tunamahitaji mengi ndani yetu,pengine ikiwamo misemo hiyo tofauti inaendana na thamani ya kitu,tumekuwa wajanja saana katika kufanya mambo yetu,na hii inatupelekea mahitaji yetu kuwa ya kijanja janja tu,hatutafika mahala endapo tutahitaji kijanja,kwani tutapata kijanja hivyo ilivyo.

Pengine wengine hubaki pale jambo linapotokea,sio kukaa na kuwa nyuma bali kufikiri vyema mahitaji yao,ikiwa ni wao ndio wanataka kufanikiwa,mara nyingine tunapokuwa safarini tuwafikirie na wengine maana wao wamebaki huko,hatuna haki ya kupaita ni nyuma kwani kila mtu anahitaji lake,na ikiwa mlengwa amekuwa na malengo halisia.tusiseme tuna shida wakati wenye nazo wametulia,maana wao sijui ndiyo wamezizoea au ni mahitaji kama ilivyo kwa uhalisia,na tunaposema hitaji hilo linaweza likawa ni la mtu basi tusifikirie vibaya kwani iliyo nyeupe kwa mmoja si impendezayo mweusi anayependa hiyo,ni kama vile uongozi,ikawe pale tukajua ni nini maana ya uongozi na sio tukaenda na bado tukazidi tukidhania lengo letu,hapa watu watatushaangaa sana,ingawa uchache ndiyo uhalisi wa hitaji,vile vingi vinatafutwa baada ya kuona utamu,utamu wa jambo na wenyewe huja baada ya kutaka kuwa na miliki,tunapomiliki vitu vingine vinaweza visiwe katika mahitaji yetu,vingine vikawe kama ni mwongozo katika mahitaji yetu,Yule anayetaka kuyajua ni lazima akubari ,tena ikiwa kwa maelezo maana ujanja unaweza kuingia pia.

Pengine tuseme hakuna anayetaka kutangulia,na hili tusiliite hitaji,maana tumefanya kwa ulazima,kwa wale wanaojinyonga waliamua,hawakuonja kifo lakini walipaswa maana lilikuwa ni hitaji kwa muda huo,haina budi kushangaa kilichocheupe na wakati ni cheusi tukitafutacho nacho hatuna,labda tufikiri kabla ya matendo,matendo yetu yakatupelekee kuwa watu wenye mahitaji mazuri,kwa Yule anayelenga ni lazima apate na kama asipopata atakuwa amelengaje?labda tuseme lengo la mlengwa halikulenga malengo,matokeo ndiyo malengo ya mahitaji,katika kufeli hakuna kufauru ila tunaweza jitahidi zaidi tukafauru,hivyo basi tunaweza kufanikiwa kwa jambo lolote ikiwa tu tumelenga na kuwa na hitaji nalo.pengine imefika wakati tuyatangaze,maana wachache wameanza kununua,ingekuwa ni kuhama tungeshafika huko,au tukaupande ili uishe ikiwa ule ulio bora kabisa tusipewe ruksa,mambo ya msingi ndiyo haya yanayotupita kwa kusikia hata,kwani ikiwa kumbukumbu zimejaa na tusisahau pale hitaji linapofikia turudi tena tusimame kihisia pia,kwani walioweza walianza hawakuhusika ya kuwa kila mtu ana lake hitaji.

By: Benson G.Makaya,
Tel: +255714336657.
Email:bensonsmakaya@gmail.com

Makaya's Forum: ELEWA 2

Makaya's Forum: ELEWA 2 :   Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye n...