Sunday, May 20, 2012

PAMOJA


Mara ya kuwaza ndiyo inayoweza kuzungumzika vingine kwani haikuweza kuwa pamoja,
tumefanya sana,tumepigana sana,tumeona sana,yote yakiwa yanaeleweka,yanapokuja mengi yanakuwa na uchangamfu,kwa pale moja litakalo leta umoja kuwapo na utofauti,kwa mmoja aliye na umoja ni rahisi kuelewa utofauti ya kuwa ametoka huko,tusizungumze vitu tukiwa na maana ya wote,bora ikawe ni kwa umoja unaoleta umoja ili kuikimbilia kheri,

kheri ya wote ipo mbali palipo na yale ya kuchanganya yanayovunja umoja,ikiwa kwa upande mmoja kueleweka hivi na baada ya muda kueleweka vile,baadaye ukaseme ulikuwa hauelewi ni kwa sababu ya muda,imekuja kubwa ukataka ndogo na ndogo umeishindwa,maana unapofikiri kukataa basi umeweza kukubari katika lilelinalokubarika,

yakaja machache yakawa mengi,yakaja mengi na kuonekana machache,yote yakitumia muda ambao unaeleweka tofauti,wenyewe huja kwa namna ile ya kusemeka,
upita kwa namna ile ya kuhadithika,kwani yaweza kupita mbali na kuwa historia,
yaani ni kipindi kirefu sana

Umoja wangu ni katika kuyaunganisha mawazo yangu,ni katika kuunganisha mawazo yangu yanayoitembeza akili yangu,haki kwa aadui kuwaza kuua ikiwa upendo kwa adui mfu,maana hata lile la kuua si lamaana kwake,labda tuone kwa umoja,pengine labda tunakataa kuona kwa umoja,pengine ndiyo maana ya ufilisi wa mali zetu,ikiwa po na utofauti chuki huwa karibu

umoja hujaa mahala pamoja na kushindwa kubebeka,hiyo ikiwa nguvu zimezidi pamoja,kwa upande fulani hatutazungumza ya kufundishwa ili wengine wasielewe,basi tuongee ya asili ili na sisi wenyewe tuendelee,tena hapo tutaelewa wote,pale ukimkuta mwalimu hajaelewa basi ahairishe somo,ubongo ni wa pamoja kwa kujua leo si kujifanya kulijulikana,

maana kila leo linatoka lake,hili litasema lina umoja wake,lile litazungumzia umoja,
lile litaleta umoja,malengo yatakuwapo,hapo hapo panapokuwa na maungano,sio mwingiliano kwani uweza wa umoja ni mapigano,na sio kama meza ilivyogeuzwa kwa kula chakula cha jana tukidhani cha leo hakijapikwa,wandugu wanaficha cha leo maana na kesho kitafika,kwa kufikiri ya leo pia,kumbe hata bila jana leo siyo siku nzuri,asante kwa chakula leo imeonekana,ni umoja usiojali siku,ni umoja unaojenga siku

Tusirudie tena tukashindwana kuelewana,hapa na maandishi kidogo kwani utakumbuka yale ya ndugu mtayaona,watu hawa,sisi yaani na wao pia,usifanye kwa vile zimewekwa alama,
ujue hata ni wapi pa kuweka alama,ukafikiri kwa madini,ukayaona ya leo maana hazina yetu ni ile ya jana,

basi hata ikawa zamani,tunasubiria kupata nguvu ili watupe mashamba,
tunasubiria kumaliza ili watupe makazi,tunasubiria kueleweka angalau tukaletana pamoja,
hapa sio ya mbu wala kipindupindu inzi,ni ukali usioleta madhara na hasara kwa mpigaji,hakuna kupigana kwani kuelezana utaratibu kwa pamoja.

By.Benson G.Makaya

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...