Sunday, May 20, 2012

MAMA



Bila wewe nisingekuwepo.
nguvu na imani imepitia kwako,umekuwa mshindi kwa  njia zako za ukuzaji,umeweza hakika nakupa saluti,maana jeshi uliloliunda si kama vile likafikirika,nguvu zimeongezeka kuona uwepo wako mama,sio tu leo ndiyo maana naendelea kupigana,mimi na nafsi yangu pamoja,nikiwa naimani kwa zuri la kujengwa hung’aa limalizwapo,maana ndiyo sijui utakuwa mwisho ama ni mwanzo wa kutembea,hapa sasa ntakuwanimesafiri muda mrefu sana,

machoni pangu umekuwa mbali hata sitaki kukusahau,
ni hapa bado nina hitaji la kukuona mama,unajua kwa nini hata sikuite mama,maana sidhani hata ingekuwa vile isingekuwa hivi,umenijaribisha kwa mengi sana,hiyo ikiwa ni njia ya kutaka nifanikiwe,sisemi mengi yakuwa nakuona haya inaweza kuja na baadae tusiitane wanafiki,maana watoto wengine wana tabia mbaya sana,hawawaheshimu hata wakubwa  zao.

Punguzo linazidi kukujaa,
ongezo linazidi nifika maana,hapa ndiyo ulijua tu,
hapa ndiyo ulijua kama nasikia joto ama vile nitakiwapo kuvaa sweta,hata kama sio baridi,umenikinga sana na mvua kwa kiti kunipisha,heshima ya upendo sio moja kwa chozi la kushoto kudondoka,mengi yanatokea karibu kushikiria mkia,hapo ukitaka nisidondoke,leo ije isikatazwe nawe kwa kujua ni mpya,maana nap engine ulielewa yako sana mama,kwani hata hali ya hewa ya mwili wangu kuifahamu,kujua marelia inaanza hii ikiaminika vilitoka katika nafsi,ndani lifikiriwapo jambo kama vile ilivyo kwa yako nafsi.

Tungetafuta wangepata ,tungetafuta ingewezekana,
tungetafuta nisingepata,maana kwa uwepo wa peke yako nasema asante mungu,maana amenijuza wewe sasa,mwelekeo na mwenendo akinionyesha kwa kisomo ni jitihada zangu,ingawe jitihada ziwe za nini,maana nasoma mwisho nisielewe kwa nini kutokujua kushona nguo uvaayo,maana zamani  hawakuvaa nguo hivyo,vile ilikuwa adamu na hawa.

Mengi yamepita ni magumu kuyapata kwa kusema,
ikiwa ni maumivu basi karibu tunafika vumilia mama,ni hapo tu karibu ya kuwa na uvumilivu,fahamu zangu zinaendana na mengine ya  umri wako,nifanye vile utakavyo,nami ntakusikiliza bado nakusikiliza mama,bado nahitaji kukusikia mama,bado nina hitaji la kukufikia mama,huko ni mbali kumbukumbu zinanijia,ntakuja karibuni ya moyoni yatakufikia,salamu kwako mama mpendwa,
Mwenyezi Mungu atajalia daima

By.Benson G.Makaya

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...