Saturday, May 5, 2012

HALISIA.


Zote ni namna za kuweza kuwa halisi nikimaanisha unaweza kuwa katika namna nyingi,kuwa halisi ni kuwa wewe,ni kuwepo na vile vinavyotakiwa,
ninaposema halisi simaanishi ilivyo kama neno lenyewe,halisi katika mazungumzo huleta picha nzuri,maana wengi watataka kujua hapo,hapo ni  nini maana yake halisi,
tena bila kusahau  kwa kuwa unajiona upo juu ama chini,usijisahau kwa namna yoyote uliyonayo,
maana hapo unataka uhalisia,ikiwa ni chakula kina mapishi,na wala si matamshi kwa yule msemaji.

katika namna iliyo moja ni lazima kuufahamu uhalisia maana unaweza kunenepa kwa vitambi na kujisifia kuwa umeweza,tena utakuwa umeweza kweli kama uhalisia ilikuwa ni kutafuta hilo,
labda unene halisi ni mzuri,pengine haina haja ya mazoezi kwani sio halisi,
yenyewe huleta namna nyingine yenye uhalisia wake,

Kwa jicho dogo kuona sio kuona kidogo,kwa macho makubwa kuona sio kuona kikubwa,akionacho mtu ni kile anachokifanya,uhalisia haulazimishwi ,
siwezi kuwa mtumwa halisi,naweza kuwa mfanyabiashara halisi,
siwezi kuwa mfanyakazi halisi,hapa sijui uhalisia wetu uko wapi,
maana wangu ndiyo ninaoufanya.pengine katika nafsi toa uhalisia wako na itakusaidia maishani mwako.

Katika maisha  kuwa halisi ni kuishi kiuhalisia pengine halisi inatafutwa,halisi katika namna yoyote inavyoweza kuwa kwa mmoja kutokupenda siyo halisi ya mwingine,maana bila kuwepo usingepata picha,ikipatikana ya tatu basi ya kwanza ilikuwepo,ndiyo idadi zikaja ili kuleta namba halisi,
ikiwapo moja yenyewe yapasa kuitafuta na mbili,
maana inahitajika uhalisia katika kuhesabu pale tu unapothubutu kuutaka uhalisia wako

muda ungekuwa hauendi nigebaki kuwa vile,kubaki. maana nimetoka pale nyuma ama mbele kuelekea katika namna nyingine ambayo nyingine hiyo ndiyo inatenganisha na kuleta uhalisia,
ikiwa lengo liwe  ndiyo ama sio kuutafuta,hata ikawe lakini lengo ni la mtu,
Siwezi kuwa na lengo moja na kufanya kimoja,
hapa ikiwa mmoja yupo na mwingine,

Pale awepo mwingine ni kwa sababu unataka kujua namna ya uhalisia wa kwanza,
tena ukauona maana pengine ni ule wa nyuma,kama ilivyo halisi ya umoja na utofauti wa hasi yake,
kuwa hasi sio chanya hiyo ni halisi,kumbe hata halisi sio nzuri kwa wakati mpya,
kujua jambo si mwisho ukitafuta wanaojua lazima walikuwa hawajui,
na huo ndiyo ulikuwa uhalisia wao,pengine unapofanya na kuona hayaishi ujue ndiyo halisi yenyewe,
kama ulizoea kuvaa rubega sasa ni nguo za pamba na mengineyo ya halisi yake
pengine uhalisia unakuja kwa yale ya asili,
kama mwanzo vile,

yapi mema mpaka mtu ukatamani kurudi na kuwa mtoto?
hapa unatamani asili,maana ulivyokuwa na asili haukuufahamu uhalisia,
kumbe uhalisia unatembea tofauti na asili

Benson G.Makaya

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...