Saturday, June 16, 2012

KUWA..


Hapa tunataka kukua,sio kutajirika bali kuwa na furaha,pengine inapasa kujua kama tunakuwa,haitaleta maana kwa mmoja kufanya kazi bila ya kuonekana na kukua,ingawaje tunaendelea kukua lakini  tusione kwa mengine tu kukua,pengine kama ilivyo kwa mfanyakazi anapoona kazi yake inakuwa,bila kujali ni imekuwaje,pengine kwa muonekano kwa vile unapoondoka uzuri basi iwe katika furaha,hapa ikiwa sio vyote vizuri vinauwezo wa kukua tena na furaha.

Katika kukua kuna  kuzoea,na endapo inafika wakati tunazoea yasiyo ya kuzoeleka hapo furaha itapotea,ikiwa kwa mmoja kama ni mke ndiyo wa kukupa furaha,ama ilivyo kwa biashara hapo tutakuwa,lakini katika kukuwa  haitokani na mtu zaidi ya mtu mwenywe,hata ikaonekana katika upande mmoja kwamba wachache au mtu Fulani amekuwa lakini japo kidogo hiyo nayo haimaanishi furaha zaidi kuwepo,zaidi tunaweza kusema katika mabadiliko ni lazima kufanyika kila siku,na hii ikiwa ni kuleta maendeleo katika kile chochote kinachofanyika.
Ikiwa kama ni kazi inatakiwa kukua katika mwonekano bora basi yapasa mtu kama mtu kukua  na kukuza yale unayoyafanya,hapa inawezekana watu wakataka kukua kwa haraka,hii ikiwa katika afya,kiakili,kimwili na mengineyo watu wayakuzayo,katika kujua kukua lazima kuelewa ni namna gani mtu anaweza kujikuza,sio ya kwamba Fulani amekuwa mnene basi ikaja na kueleweka kuwa amekua,kukua ni kubadilika,lakini  kukua ni kuwa katika namna ile mmoja anayoipenda,

Kwa mmoja anataka kuwa mwanamichezo na mwengine anataka kuwa mwanamichezo lakini hii ikiwa watakuwa wanamichezo wa michezo tofauti,na hapa ikaja maana ya kuweza kufundishana maana kwa wengine wametaka kukua lakini haijulikani ni namna gani ambayo inaweza kukamilika ya kufanya kama ilivyo kusudiwa,kazi yetu iwe ni kuingia na kutaka kukua zaidi katika ufanisi hasa kwa yale tuyafanyao.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...