Friday, June 8, 2012

NAMNA..

Tumeyachagua wenyewe,hapa machache yameongeleka lakini yasipigiwe vigeregere,
usiombe kusubiri,usiombe usubiri,
maana pengine mazoezi yatakuwa makali sana kipindi hicho,
yataongezeka kwa kulingana na muda,pale tukitaka kupumzika bila hitaji letu,

Tukataka kutulia na kupigiwa makelele majumbani kwetu,
pengine tukiwa hatutaki usumbufu,
pengine sisi ni wasumbufu sana,
hapa ni kuelewa,hasa kwa mmoja na mwenzake mwenye uelewa.

Yanayochagulika ndiyo hasa tuliamua kuyafanya,
maana hapo baadaye tukasema ziikuwa ni ndoto,tena tusijue tumeota wapi na lini?
bali tukafananisha si tunaijua jumamosi?ya kila mtu ndiyo iliyo ya kwake maana pengine ilipogeuzwa ilifanyika kwa namna ya kugeuka,

pale itakapogeuzwa zaidi itageuka na yenyewe,
maana muda unasema unataka kwenda na sisi ili na wenyewe ufurahi,
pengine ndiyo maana tunahadhibiwa kwa kutokuwa na muda.
Hapa mengine yaliyochagulika yakawa ndiyo hayo yaliyopita,
si kama imegeuka vilee..tumefikiri sasa bila kujua uzee wa mbao kabla ya msasa,
tutazeeka sana,kama tutapigana na bila  ya hamasa.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...