Monday, June 11, 2012

SEMA KWELI..

               
Hakuna sababu ya kudanganya wakati unahitaji useme ukweli,
uzungumze ujue kile kilicholeta maana,maana haijaja kuwa kweli bila kudanganyana,haijaja kusema kweli bila kuchanganyana,
pengine ukaona pale umekosea kufanya vile,pengine ukaona pale tu ulipopatia,
haki iliyo ya mtu lazima kusema ukweli,pale walipo matapeli  usogee ili kuepukana na ukweli pengine ukajua bora kwa kuchanganyana na matapeli.

Karibu mgeni nyumbani hakujazimwa taa,karibu mwenyeji ya ndani na njiani hakuna kukataa,pengine ulikuja mara ya kwanza na uliona bila taa,pengine ukakataa kurudi kwa kufanya bila manufaa,kwa ukaribu jirani angalia njiani.

 Kinachoendelea ndiyo majibu hasa ya uliyoyapanga,ikiwa kama ufahamu ni mdogo basi litagundulika hilo na sio kwamba kwamba kwa anayefeli maisha anakufa,
hapa ndiyo unamwelewa mungu,hapa ndiyo utakaa na kujua msamaha wa mungu maana ingawa ukashindwa yeye atasamehe,na usikatae hilo kwani umesamehewa mara ngapi?

Yatakuja mengi mengine mapya yatasemeka yalikuwepo,hiyo ikiwa na yenyewe yamechoka huko yatokako,
yakiwa yanahitaji msaada basi yatapenya hata kwenye nafasi iliyo ndogo yako,
ukataze  yale yasiyokuwa na msingi ili uone kitakacho bakia,
maana haitakuwa na maaana dunia kujazwa na vyoote hivi.

Sema kweli visikuchanganye na kwa uwingi uliopo usidanganye !!


No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...