Monday, June 11, 2012

KITAELEWEKA TU.

Vijana ni taifa la kesho,ujana ni nguvu ya leo inayoleta faida kwa ajili ya kesho,unapenda sana kusema maneno fulani,hapo ikiwa ni katika kujipa matumaini na hata vile ilivyo katika kuweza,maana utasahau ulisema nini ulipokuwa unatumia nguvu zetu,hata pengine isije usielewe,

Pengine isije kuwa nguvu zako ulizitumia tofauti,hapa ukiwasahau hata wale waliokuwa wanakugaia vitu ulipokuwa mtoto ukilia,pale ulipokuwa hujui kusema lolote la kubisha maana haikuwa na maana ya kuweza kufanya jambo pekee.

Hakuna yasiyokuwa magumu bila kujua kwamba ni zamu yako,umeona washindi wengi wametutoka dunia,hivyo ikiwa ni namna ya zamuzamu inapokuja,
lazima upokee vile unavyopewa hata kwa kusema asante,maana wengine wanashukrani zao za kutoa.leo usiisuburi sana kwani inaweza kuchelewa hivyo ujaribu kwenda,twendeni kwa mwendo huu huu ikiwa ni kwa umoja,pamoja tukaungana.
Hasira ya mkwezi ni kama ya daktari,pengine ujue kama daktari ni mkwezi..maana uhesabu kwa nini imekuwa hivyo,pengine na sisi tukawe hivyo,kwa kutokusema sio kama ingewezekana,bali kuweza kwa kuonyesha tu kama unafanya,yapo mengi ya kufanya pale uvumilivu unapokuwapo,hii ikiwa kuna mahala fulani furaha ipo tu hewani.

Ujana ni shimo la taka linalohitaji kujisafisha,vijana ndiyo watu watata na hata mitaani kupigana,hii ikiwa inaondoa maana,hapa ni sawa na kusema hautaweza kuwaombea walevi waache pombe bila ya kujua kwa nini wanalewa,yatakuwa sio maombezi haya,mitume walikuwa wanajua,hivyo hata matibabu yamekuwa sahihi tokea enzi zetu za mababu.

Cha mwisho kinachoelekea katika namba moja ni vyema ya kuwa kimejua chenyewe ni cha mwisho,hapa vijana tujijue ili kieleweke,maana utaishi kimfano na kulalamika kama hakijaeleweka.nguvu na imani viambatane,

SEMA WEWE KWANZA VINGINE VITAFUATA..

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...