Tuesday, July 31, 2012

MACHONI..


Machoni kama watu mwishoni hawana utu..hawa si watu kabisa alisemeka hadi moyoni,hawa si watu kabisa kabisa.maana yawezekana na sisi tumezoea sana kupewa kwa nyuma,tunataka tunapotenda wema basi turudishiwe na wema,hawa watu wa machoni sio wa mafichoni ndiyo maana kuna kuonana,pengine hata kuonekana na kusikika.tenda wema achana na ya mwengine na tembea zako,pengine ikiwa imekulazimu kutokea isije kuwa imeilazimu ikutokee,sijui utaonekana wa namna gani machoni pa watu.

Umepewa kijiti peleka mbele unarudisha nyuma kufanya nini?tuachane na story za kuonekana machoni wachache wakilia moyoni,hili halitakuwa la mmoja lakini kwa kila Yule moyoni litakayemuingilia.tena ikiwa kwa vurugu maana hata moyo unaona katika namna yake,pengine ndiyo maana tunachagua ya kufanya,yupi mbaya aliyeamua kufanya mabaya au moyo wa uliyeamua kufanya mabaya?maana pengine kila mmoja wapo angejua angefanya mabaya tu.

Karibu tusogeleane maana tusikie mioyo inavyodunda,asante mama karibu yako mikono kuitizamia presha,sijui zitakuwa ni homa au maralia za taifa,kwa macho hatutaona tukisubiri hatuonani,tenda unaloliona ukisubiri usimsingizie shetani,kama ilivyo kutokutenda ni ‘kutenda’kwani kinachofanyika hapo ni maamuzi,nafsi ya mtu ndiyo inaamua.hivyo tokea machoni mpaka katika nafsi ya mtu hapo ni kasi sana,maana tunasema haya mengine tumuachie maulana.nafsi,moyo,utu vimebebwa na kitu machoni

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...