Monday, July 9, 2012

YAACHE YAENDE..!!


Maana mengine yamekuja kama tishio,mengine yamekuja ili yakionekana yaonekane ya kileo,wanajua wachache wale wanaoitwa walevi,maana kila mtu anajiona yeye mwema,katika kuishi maisha yale mtu akaishi anavyotaka,maana hata ukahamia kaburini nahisi utasikia wachache wakinong’oneza,maana wao si hawajawahi…!!hawajui nini maana ya kuona pale,ama kufika pale,pengine yale ni mengine yaache yaende,pengine yale ni mengine waache watende,

Muda huo unapofika ndiyo unakuwa wakati wangu,maana pengine ndiyo wako sasa,kama vile tunamcheka Yule anayecheza kipindi kifupi bila ya kujua urefu ukoje,mengine ni ya lazima kuelewa pale inapotakiwa kufanikiwa,maana kila mtu na mwenzake wanataka kufanikiwa,wakiwa  na tegemezi na kwenda nayo yale waliyo nayo na kama ni maadui basi kheri waongezeke,hapo wakiwa wawili pamoja na Yule mshamba,maisha sio kuelewa sana sana ya kutaka kuelewa sana,maana hapo tutakuwa tunaelewa tu,labda kukumbuka,na wala haina haja ya kuyakumbukia wacha yaendee..

Kesho tutalia zaidi ilivyo ya leo,maana hichi cha leo tulikijua tu,pengine tumezoea sana ili kutaka kueleweka,akiyafuata  Yule mjinga na mwenzake atamcheka,hapo tutapigana na kukumbuka umoja wetu usioeleweka,kuna Yule amepata kitu na asijue nini kile zaidi ya Yule anayepata kitu na kujua nini hiki,hiki kinatumika,zaidi ya vile ikafikirika maana kwa mwengine anaweza kuwa hafikirii mmoja unapofikiria,pengine sio wengi,pengine sio mengi,haya mengine tuyaache yaende tu!!

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...