Monday, July 9, 2012

NASHANGAA.!


Nashangaa kuona watu wanashangaa,maana sijui kipi ni kigeni,ama mimi ni nani,wewe je?pengine tusifikiri utamu wa sukari tukasahau wa asali,wengine watasema si yale yale tu lakini ile kuandika nyingineyo yenye maana mbadala bila kujua kama kuna maana tofauti hapo hatutaelewana ,hapa nafsi zitatutoka zana baada ya kuja kushangaa kama kweli ya fulani ndiyo ya kweli,ukisahau anaendelea kuishi kwa nini tusimkataze utapeli wake,maana zaidi utaingia kwa watoto wetu hapo inakuwa ni jasusi na mtutu.hatutashangaa vifo hapo,yamkini uwepo tu.

Karibu nyumba ya pili kuna sherehe,kumbe hapo mgeni kamkaribisha mgeni,hapo mwenyeji kaingiliwa na mgeni,haya mengine ni baadhi ya furaha katika yale machache yanayokuja,pengine tusijekushangaa hata yaliyopita,hapo yatupasa kuyarudia na sijui mageni ni yapi..?zamani ndiyo watu walikuwa wanashangaa mataa kwa sababu walikuja kwa ajili hiyo,siku hizi hata vijijini kuna mataa..kila mtu anatafuta lake,kila mtu anasiri yake moyoni..kila mtu na kitu vipo hivyo kwa sababu hiyo.

Tunakuja kustaajabu haya ya musa sasa,naona tunashangaa jua kuwaka mpaka jioni,maana yawekuwa nastahili la kuzama,kaisari kama unataka nipe ila kama unaitaka chukua,maana lipi limekuwa bora kama sio la kuambiwa?angalia hayo yote ni kwa sababu ya kaisari,mwanangu angalia pengine usisahau kusali.nashangaa kuona nilitaka kuandika mengi na nimeishia hapa,hili geni sasa,hili jipya akilini pengine linatoka ama linaingia,kumbe kwa geni yastahiri..

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...