Tuesday, July 24, 2012

HAPO ZAMANI..

Sio lazima kuuongelea wakati uajo bila ya uliopo,ni watu tuliopewa hali,mali na utambuzi mkubwa sana juu ya dunia hii,inapofika kipindi haujajua kuhusu hali au mali basi jaribu kuelewa maana ifikapo baadeye hiyo itasemeka ilipokuwa zamani,zamani ilikuwa ukiamshwa kutoka kulala ni kula ama uende shule,nikiwa nazungumzia vijana wazee ni vigumu hata kukumbuka enzi zao.

Tulivaa vizuri bila majina yetu ya kisasa,zamani bwana ni kama majumba ya kitasha,maana utakutamani kama vile kwa mwizi pale mlango unapokuwa hauna kitasa,tunaenda tunafikiria mbele,tunaenda tunaangalia mbele,naipenda sana hii namna ya vijana wa sasa,maana wale wazee wa zamani walitabiri mavazi yao,na kama ukifuata matakwa yao jiandae kuwa maana watu wamekuwa zamani.

Zamani kuna mengi ambayo hata hayasemekani,zamani hata sitaki kutamani maana nikikumbuka ni sawa nguvu kuirudisha imani,kuna watu wa kisasa wana akili chafu sana,hii ikiwa ni tofauti na zamani,kwani kwa kuwa na muonekano mpya na akili za zamani,ama tuseme akili za nje lakini mwili ndani,hatari sana tukilinganisha ya sasa na zamani.tutaenda kwa imani tu.ya zamani ni mengi,hapa yalikuwa kama chenji tu.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...