Tuesday, July 24, 2012

KUSUDI


Unaweza kufanya jambo bila hali yoyote,maana kutokuifikiria na hata ikikatalika mwanzo mwishoni ukikosea utasema samahani,kwa sababu unafanya bila hata ya kuuliza,ukasema haukujua kwa sababu haukusikia mahala pengine,kumbe unafanya maksudi,maana kama kosa linakujaje na mwalimu yupo katika mahala husika,Pengine mwalimu hajui kufundisha.

Unapokaa chini labda ujiulize ni kwa sababu gani unapenda,na hapo utausingizia moyo,na baadaye useme kuwa moyo wako unauma,ya kwamba haujiskii vizuri,kumbe mwanzo ulikuwa unakujiskia vizuri. kumbe haujielewi,haukujielewa ni namna gani furaha unayoitaka unaweza kuipata,yapasa kwenda mahala fulani,yapasa kuthubutu kwa kuufahamu uzuri wa ua mwanzoni,na mwishowe unaweza kuona kweli lile ni ua,lakini baadaye ni lazima kuelewa   unafanyaje na hilo ua.

Kufa ni lazima hata maana yahitaji ua  kumwagiliwa na sio kukukaukia,mapenzi yamejaza matunda yote,maana hata kama ni mgonjwa anachagua lile alipendalo na usipojielewa hutapenda,ni maana ya kutokujua asili ya mapenzi yako labda haifai kuumiza wala kuumizwa pale unapopenda,na hii haina maana viongozi kutowapenda wanawaongoza

Mengine haya ya leo unalaumu kwa kukosewa,bila kudhani ya jana wamefanyaje,maana ni yale yale tu,na kama kubadilisha basi haina maana ya kushindwa,labda kuwapa miji kwa wale wa maksudi,kama ilivyo maksudi huwa haiumi,mtu anaweza tenda vyovyote,hasara ya mwanzo yaipasa kuibeba,kwani walishaamua kufanya maksudi,Angalia kesho yako inakujaje maana mambo yanaweza kubadilika tena na kudai Pumziko la jana.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...