Thursday, September 13, 2012

ANZA UPYA..

Ni katika kuanza mwanzo,pale ikiwa kuna makosa ama ni njia mpya,ikiwa unahitaji la kuwa peke yako ama kukaa gizani ikiwa jua litawaka kesho,hivyo ni lazima kufanya katika uwezo wako ili inayofuata ije vizuri,pale inapofika kipindi cha kuanza upya,moyo ukiwa na yake kama mistari ya rangi ikiashiria mvua kunyesha pasipo taarifa,ama ni kuzuia endapo italeta uharifu.miaka haita weza kuchukua vile ulivyofanya,ikiwa nafasi ya kuanza upya ni pekee kwa sasa,hivyo bado ndoto zitakuja kweli.

Ukiwa muda uwapo na upweke sio peke yako,njia yaweza kuonekana nyembamba ikiwa hata sauti hazisikiki,pengine sauti ndiyo zikatembeze nafsi,pale unapokuwa peke yako,hiyo ikiwa umeishia hapo unasubiri kile maisha itakuletea,katika kila maisha ikitakikana asubuhi njema,kwa mabaya ya maisha kuyaacha na kuchukua nafasi yako iliyo mpya,pengine ikiwa ni muda wa kufanya vile uvifanyavyo,yaani ipasavyo.

Magumu huwa yanaonekana baada ya kufanyika ikiwa haikueleweka mwishoni utasikia ‘nilijua’maana hata ya kushindwa yanajulikana,na hii ikiwa kwa kufahamu ama kwa vile ilivyo inavyoweza kwa makosa kuyafahamu,maana kwa kipindi kilichopo yahitaji kuwa kiongozi bora ndani ya maisha yako,ukiwa kijana anza kwa kuweza hata kuendeleza maana yote yanayokuja ni baadhi ya yale uliyoyafanya mwanzo.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...