Sunday, September 23, 2012

KWA MUDA MFUPI...


Ni wazi mandeleo ya mwananchi huletwa na nafsi yake mwenyewe,hii ikiwa ni katika kuamua endapo kuna  jambo lifanyike ama la..na ikiwa imechagulika na ieleweke,maana pengine  ni  kwa faida ya wananchi,na katika faida ni lazima isiwe na kudanganya toto,na endapo imekuwa bila ya kufahamika basi hiyo ni sahihi maana hata sisi wenyewe tunaishi kwa muda mfupi tu,na pengine kupitia wengine yaweza kuwa ni kwa faida yao tu,maana kama unajijua unakaa kwa muda mfupi ujenge ya nini?

Hapo kwenye kujenga yatasemeka mengi,maana kwa vingine ni lazima kufikiri endapo kuna tegemezi na hiyo ikaeleweke kama ni la muda mfupi ama kudumu,vinadumu vyote lakini si nafsi ya mtu mwenye mawazo mafupi,utanenepa kwa kuwa unakula,utakula na usinenepe kwa kuwa haujaridhika,tena maswala ya muda mfupi yakiwa yanakuchanganya.

Fikiri kwa muda mfupi ili kuweza kueleweka kwa kuwa wengi wanataka majibu,usikurupuke ya kuwa muda ni mfupi ikaja ndiyo sababu,hata yale yaliyofanyika ni namna ya kutaka sababu endapo yakauliziwa,kesho tutaendelea kulalama kwani wale wa kwanza muda wao unaelekea kuisha,tungalikuwa na thamini na yale yanayotutegemea,hakika hata  muda mfupi usingekuwa ni sababu.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...