Friday, September 21, 2012

ZAMA ZA SASA.


Inapofika wakati kitu kimeharibika huwa inaleta matatizo  katika mazingira hasa ni kutokana na kutokutegemea kwamba kama zama  za sasa si kama zile za zamani,ni wazi nimekubali tekinolojia,ni wazi nimekubali mabadiliko Ni technologia,ikiwa nataka kubadilika na kwenda na mambo ya kisasa,ali mradi ieleweke na ijulikane kama kuna uwezekano wa kufanyika kwa jambo,isiwe imepitiliza kwa kuwa Wakati mambo yaliyotendeka yalitokana Na kile kinachofanyika zama za mda wako huu.

Imekuja kipindi sasa najenga uchumi wa  mwenzangu bila ya kujijua,maisha yangu nimeyafanya bidhaa ya bei rahisi ni si kama zile za kwake anazozitengeneza kwake,maana nimeletewa mng’ao ili nijue kinapendeza,najenga huku nabomoa na ifikapo kipindi najua kutakua hakuna namna ya kuona tena mbele kwa kushikwa akili na mwanga wa vile vinavyong’aa kupotea,pengine kuongezeka umaarufu katika hitirafu,ikiwa nimeruhusiwa kuwa dereva wa maisha yangu.haki taifa linapotea kwa kile kidogo cha zama za leo,maana kila mtu anaminya jicho moja anakuangalia  na anafungua la pili anakula vyake.

Zama za sasa inaonekana ni wazi vyakula vimepungua,ardhi wanalima wageni maana wenyeji mmelima sana.tena mara ya kwanza walikuwa wakilima na kujenga,labda ndiyo wanaanza kujenga tena.maana katika maamuzi ya kiongozi mmoja yanaweza kukupa uhuru kama yanavyowaza kukupa vita na kukunyima amani kwa kiongozi huyo huyo,hapa ikiwa tujiongoze,zama za sasa ni za ukweli na uwazi,hizi ni zama zako

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...