Thursday, November 15, 2012

HAKUNA MKATO KATIKA MAISHA..



Ni kupambana,ni kutia mkazo ili jema la mtu likaja upande wake,maana lako ni lako,maana wewe ni mtu maalum,ikiwa kuna  wakati unaotofautisha maana na kuleta tafsiri tofauti,ukiwa unaishi fanya lile la kesho maana leo imeshatokea pengine ndiyo maana yapasa kujiandaa kabla ya safari,ikiwa kungalikuwa na uwezo wa kutokusafiri kwa kutumia muda basi wengi wasingechelewa,haina maana ya kupita mkato ama njia ndefu ili kuleta neno maisha,ya leo ukiyaacha utafahamu vyema kuhusu kesho,kivingine ikawa ni ufunuo,hakuna mkato katika maisha kwani kila mtu yapasa aishi yake.

Ikiwa kuna kufananisha  ndiyo kumeleta vitu na utofauti,ukitaka kuachia njia yako jaribu kukalili ulipoishia,maana unaweza ukawa hauelewi na kujikuta umeelewa vyema sana kwa kuwa ndiyo njia uliyotaka kupita,unaweza kurudia jambo mara nyingi na usijue ni kwasababu gani haujaweza fanya lingine,hayo yakiwa ni matendo katika maisha yako,jaribu kufikiri nini unataka,chukua hatua na jaribu kupata na kuyaelewa ya nyuma,sisi wote tuna namna moja ya kuishi,ikiwa unaweza kulichukulia jambo kiuhakika katika mlengo wako wowote,upe muda na njia zilizo sahihi,hata ikiwa haujafahamu nini usahihi wake lakini muda utakuonyesha njia,maana utafanya lile linalokusudiwa na muda.

Kama ukienda na kufikiria kila maisha ya mtu mmoja unaweza usione mafanikio maana ni lazima ujue nini unachohitaji katika muda sahihi,pengine yaweza kuwa tumbo linauma kwa sababu ya njaa,fikiri kama unaijua njaa kihalisia,maana hata ikawa gari bila mafuta ni sawa na kumpa baiskeli mtoto asiyeweza kutembea,yote yanawezekana,ikiwa unaweza kukubali kwa yale yanayokupitia maishani mwako.hakuna mkato katika kupika nyama bila maji maana utakuwa unachoma,jambo ni kujua.

No comments:

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO : Watakwambia unabahati kwakile ulichokifanya kilichokufanya uwepo hapo,kujipa ufalme na kuzungumzia maisha...