Sunday, February 19, 2012

Makaya's Forum: MAKINI.

Makaya's Forum: MAKINI.: Tuangalie,tuone ni tunatumika katika utofauti wa namna gani ikiwa pamoja na mashine au mashine zinatumika ikiwa kama ni mifano yetu,zik...

MAKINI.


NIangalie,Nione ni natumika katika utofauti wa namna gani ikiwa pamoja na mashine au mashine zinatumika ikiwa kama  ni mifano yangu,zikimaanisha mimi ndiyo mashine na zenyewe zimetengenezwa kwa mifano yangu pia.bora hivi ilivyo maana ikawa haina haja ya kuzoea kile kilicho halisia,kwa umakini ni lazima ujitambue ya kuwa nisiwe mvivu,nataka kazi na nisijue huko makazini kuna nini nachokifuata,Haina haja ya kuwalazimisha walimu na wakati wanafunzi wenyewe hawaelewi,nikisema waelekezwe wanafunzi nitaingilia majukumu ya walimu,tena inaweza kuwa chukizo kwani muda wote huo shuleni wanafunzi wanajifunza nini?au unavyovijua hujui kama ndivyo unavyovifanya,maana tabia yao ni kufundishwa ili iweze kufanyika,ikiwa kwa kuona ama kusikiliza yote ni lazima niwe na umakini nayo,kwani yale yanayopita yananipitia hapa nilipo,utachaanganyikiwa kwa kutokuwa makini,kwa kutokuwa mwangalifu na ufuatiliaji wa mambo yako usifanye kuwa unapelekwa kila mara,kwani itafika kipindi utachoka kupelekwa pelekwa kama mashine,ikiwa ulikuwa unapelekwa basi wapo waliokuwa wana upeleka peleka,na wao wanaweza wakaamua kukupeleka kipindi pale umechoka,hautakuwa utumwa,hayatakuwa mateso,ni sawa na jambo usilolijua,labda kwa namna itakavyo tokea ndivyo italeta maana itakayo kuwepo,labda kwa tahadhari ufikiri na uamue kwamba unahitaji kujitambua.

Yule anayefundisha bila kuyajua mazingira yake ana uwalakini wa kuitwa mwalimu,lakini ya kuwa kuna uhaba wa kufikiri bora ikawe kujikimu,maana imefikia wakati utaamua kuwa mwizi alafu ukakataza kuiba, ,na ukija kukamatwa uelewe ulikuwa kama magurudumu ya gari,ikiwa kuna kona ulikatishwa tu,kwa hiyo siyo mageni sana katika kutokuyaelewa,wachache wanaelewa  kwa jinsi tunavyoelewa,anapotangulia mwalimu darasa hupanga yale waliyoambiwa na mwalimu,njia mara nyingi huonekana kutokana na hali ya hewa,ingawa unaona kwa umakini lakini unajikuta ukielekea mahala usipopafahamu,na hii yote ikiwa bado unaona labda njia hizi zinahitajika kufanyiwa ukarabati kila muda na watu wakajua,maana tulio maskini tunalia muda wote,na sio kwamba hatupo makini,kwani mengine sio ya daktari.unapolia sio ni watoto,unatoa machungu uliyonayo ukifikiria ulipotoka mpaka ulipofika,kama mtu afanyapo kazi kwa nguvu na kutoa jasho ndivyo ilivyo kwa mateso ya moyo inapokupasa kulia.
Kama walivyojijengea,nguvu usimalize kwa yale waliyokuwekea,ikiwamo inaruhusu usiiruhusu kwanza,wajichunguze wenyewe wanafunzi,hata ukageuza ramani Yule aliyemakini hapotei kwao,ingawaje, zaidi uendelee na umakini wako ili yale ya mbele yakafanane na ya nyuma pia.Umakini unahitajika kwani yaliyobadilishwa kutoka juu kuja chini mengine ni mepesi yakaweza kudondoka yenyewe ,ukumbuke wokovu upo,na kama uliokolewa jana haina haja ya kurudia kwani wengine wanahitaji pia,vingine ujiokoe mwenyewe maana umepewa kila kitu,na Yule asiye nacho kwa kuona hivyo afanye lolote na ataelewa maana, ,maana tena ikiwa wale ambao hawawezi wamepewa nafasi za mwisho kabisa katika kufauru,ikiwa umakini mdogo pamoja na fikra  ndiyo huo unaweza kuwa uwezo wetu.

By:         Benson G.Makaya.
Email:bensonsmakaya@gmail.com

FIKRA.



Kufikiri ni kuwa na hitaji la kurekebisha jambo,kunatokana na mawazo,kwa hiyo fikra zinaweza kuwa ni mawazo,kufikiri ni kitendo,kurekebisha ni kufanya,fikra hujaza matendo hayo,zikiwa kama fikra halisi huwa haina ulazima ya kuwa iwe vile ama hivi,itakavyo kuwapo ndiyo hivyo,ya kuwa kila mtu ana fikra zake,akiwa na malengo mwanadamu hupanua fikra ili kuyafikia,hiyo yote ikiwa tunaamini kwa yale tunayotaka yatokee katika mandhari yetu ikiwa ni baada ya matendo yetu au yenyewe tunayoyafikiria yatokee ndiyo tutende,tunapotaka kuyafikia yale yaliyo mema,fikra zetu ndiyo huonyesha usahihi wetu,fikra ndiyo zinatutambulisha kwani inasemeka kwa kile tunachokifikiria ndiyo hasa tutakacho kitenda ikiwa tu kimeonekana. Mara nyingine kisionekane kwa Yule anayetenda na hiyo inatokana na kuwa haijulikani,Yule anayetenda  anaweza kuwa na ufahamu mdogo ingawaje yeye mwenyewe akiona anaweza,kwa muonekano  ni wengi tunaweza,ndiyo maana ikawa  fikra zetu zikatutuma mahala na muda tofauti.

Mara nyingi tumekuwa tukikaa na fikra zetu,tukiziamini ndiyo zenyewe,ingawaje vile vya mtu anapewa yeye mwenyewe,ikiwa tunavitenda au tuonyeshe maana ya kile tunachokitenda,mabovu yapo mengi sana,ikiwa na mazima yapo,mabovu ni haya hasa tunayoyafanya kwa kila fikra za kila mmoja wetu ikiwa kwa Yule anayefanya pia naye anasema yake ni mazuri sasa sijui tunayafuata yapi,hata kama sio ya kuyafuata tufikiri tumeyafuata mangapi mpaka hapa tulipo,maana tusingeweza fika katika wakati huu bila kujua ni wapi tumetoka,hata tunapoenda tutayafanyaje hayo?basi tuyaangalie yale machache waliyofanya wengine yakaitwa ni mazuri,maana hata tukiwafuata watu wazuri tutakuwa kama wao zaidi kibaya kinakuja pale tutakapo fikiri zaidi,na hapo tutakuta kuna upande mmoja umetokezea katika upande mmoja ule mwingine wa kwanza,yaani nafsi moja imekuwa kupitia nyingine,na mara nyingine nafsi itakayo iga isifanye vizuri vile ilivyofanya ya kwanza,hapa tutachafua hata wale tuliowaita watakatifu,tutawakuza zaidi wale tunaohitaji kuwaita watakatifu ikiwa hata kwa Yule aliye fuata muelekeo alifuata njia nyingine,ni haki kutumia njia yako pale ufanyapo ili mradi jibu liwe sawa,hii ni katika maisha na sio darasani..maisha ni kama darasa.labda tuone utofauti wa walimu,wanafunzi,majengo na mazingira yote ya shule hii iitwayo maisha,maana kwa upande mwingine mazingira yanachanganya.

Kama shule ilishindikana ni vigumu kwa mtu kumweleza fikra ni nini,sio kwamba haiwezekani,ila inaweza kushindikana kuelewa ikiwa fikra ni tofauti,sio kama 1+1=2 au hesabu ya kinamna yeyote ili lije jibu ambalo kwa aliyefundishwa anajua,au atakuwa amesahau,ikafike kipindi tukaelewe ni namna gani tunaweza kuziendesha fikra zetu,binadamu tunaishi tofauti na hii inatokana na fikra,ikuzwapo fikra ya mtu mmoja ni tofauti na mwingine,labda tuambiane kuhusu ukuaji wa fikra zetu,isije tukashindwa na hili darasa la maisha kwa kutaka tuelewe namna ambayo fikra ya mmoja ikataka tuelewe hivyo,lengo ni kuelewa,na hili kuelewa inakupasa uelewe,vile inavyokuwa tofauti ndiyo njia ya kupanua uelewa,kwani utofauti unakuja pale mtu anapoelewa sahihi,na ikiwa mtu ameiona tofauti basi hataweza kuitenda tena tofauti labda iwe fikra zake zimemtuma,na sio kwa Yule anayetaka kuelewa,kwa wengine imekuwa ni vigumu,wao wakitaka kuelewa namna ile wanavyoelewa wao,tunapofika hapo tunakuwa hatueleweshani wala hakuna maelewano, kwani kila mtu anaelewa lake zaidi ni tujue lipi ni la msingi tutalazimisha kuongea ili ieleweke kuna maelewano lakini  watakaoelewa ni wale hasa wanaolazimisha,maana walikua na nia hiyo ya kueleweka kinamna yeyote walivyolazimisha.

By:       Benson G. Makaya,
Tel:     +255 71 33 66 57.
Email;bensonsmakaya@gmail.com

Saturday, February 18, 2012

Makaya's Forum: MACHO YANAONA SAHIHI..

Makaya's Forum: MACHO YANAONA SAHIHI..: Ni wazi macho hutumika kwa kuangalia,kuona,kutazama yote yakiwa kama ni matendo yake,na hii yote inatokana na namna tofauti ambazo zim...

MACHO YANAONA SAHIHI.



Ni wazi macho hutumika kwa kuangalia,kuona,kutazama yote yakiwa kama ni matendo yake,na hii yote inatokana na namna tofauti ambazo zimefikirika,na hata ukazifikia.macho ni moja kati ya viungo vya mwanadamu,NI macho!!

Pale mtu anapofahamu inapoelekea yeye mwenyewe katika nafsi yake kuwa na utambuzi na wakati mwingine unaweza usiwe wa kiujumla mtu wa kujielewa,unapoelekea ni mbali zaidi ya ulipotoka,ni kama pale umefika mahala  na kusahau yote uliyokuwa ukilalama nayo kwa mara ya mwanzo,yakiwa yale yamegeuka kuwa mazuri,na uzuri wake haujaja tu baada ya kuacha kulalama,bali ni pale uliposifia vizuri,maana unaweza kushukuru mungu kwa kufika bila kujua mahala unapoelekea,ulipo.tumshukuru mungu,tena kwa njia nyingine hazina waelekezaji…inahitaji nguvu kweli na uvumilivu ili kujua pia kuelekeza,si watakuja na wengine,wao ndiyo wakiwa hawajui kitu kabisaa,watatulilia pamoja na hata ukiwakataa utakuwa umezikataa nafsi zetu,maana ikiwa unakubari mifano hai isiyoonekana ,uangalie yasije timamu yasiyowezekana,yatatusumbua tu ingawa yanaonekana yasiyokuwa na ufahamu,tena hata kuwa na ubishi,wakiamini wao ndiyo wameishi,au tuone labda kama utasahau hata majina yetu maana ingali wote tungeitwa “SALUMU” ingelikuwa haina haja ya kuhukumu,labda ubaki ukituhumu ingawaje wanaonekana lakini ushaidi hautadumu,wanapoteza wao ili ieleweke wanayoitaka,maana ndiyo chaguzi pekee litakalo baki.na hii pekee usizani kwamba ni ya kwao tu hata kwako pia,yaani yangu ndiyo itabaki.maana kila mtu ataona ya kwake.

Yaliyopo yametoka mahala,yaliyopo sijui yametoka wapi,kwani nasema hivyo ya kuwa siyo yote mwanadamu akayafahamu,mengine yapo katika miliki na uwezo wa watu wengine,na endapo ukikubariana na hili basi lazima ujue kwamba lile au yale uliyoyashindwa ndiyo yetu,maana yangelikuwa si yetu usingeyafanya,au useme kweli sio yetu basi uangalie mara ya pili,maana wakati unavyosema si vile unavyomaanisha,ikiwezekana ujue wakati ni mwanadamu mwenyewe,kama kijana wa kiume akaota ndevu na asinyoe huo utakuwa ni wakati wake,amemaanika hivyo.na hata ikawe siyo mara ya pili ila ni tendo lililoonekana,maana kama tendo linaloeleweka ni litatimia kwa kitendo ni lazima ujue chanzo,ili  yakija mafuriko usilalame,maana ulijua yatakuja na kutuzomba,tena kwa walio mbali wafahamu..MAFURIKO!!.shida za kuonekana hazipaswi kumwinua  na kumtuma mwanadamu,anayeona na kutenda katika utatuzi ni mwana adamu mwenyewe,isifike kipindi ukalazimishwa kuishi,tena ikawe ni amri kwamba sasa ni “LAZIMA” ,ingawa usipoitumia lugha hii katika mambo yetu utashika mitutu,watoto wataona baba zao wanachokifanya na kwa sababu wao wamekuja kujifunza,wamekuja kukua,wamekuja ili wawe wakaitwe watu wazima na wakajue,watashika mitutu yenye technolojia ya kizazi chao,hapo vita itakuwa haina heshima..watoto wataonekana wakubwa,na kwa wakubwa labda uwasikilizie,ingawa wanasema vita haina baba. 

Tunapoelekea hakutazamwi mtu ukaambiwa ona,sio kwa macho.unapoelekea ni mbali lakini si kama kule ukasema ulipotoka,kwani wengine watasema ni karibu kutokana na maisha yao kiujumla,unapoelekea ndiyo kwa mungu.tunapokaribishana majumbani mwetu tunategemea HODI,kama kuna mgeni ataingia bila hodi huyo atakuwa mwenyeji sema ni sababu ya mgeni aliyetangulia hakumkuta mara ya kwanza.

 UKITAKA KUJUA NI LAZIMA KUJUA UMEJUAJE?

By:        Benson G.Makaya,
Tel:     +255714 33 66 57.
email:bensonsmakaya@gmail.com

Friday, February 17, 2012

Makaya's Forum: USHINDI…UNAHITAJI KUJIANDAA.

Makaya's Forum: USHINDI…UNAHITAJI KUJIANDAA.: Maandalizi ni malengo katika kutekeleza yale yanayotaka kufanyika,ikiwa katika mmoja mmoja hadi pale ikafikia kundi,hii yote hutokana ikiw...

USHINDI UNAHITAJI KUJIANDAA.

Maandalizi ni malengo katika kutekeleza yale yanayotaka kufanyika,ikiwa katika mmoja mmoja hadi pale ikafikia kundi,hii yote hutokana ikiwa kila mmoja aliyepo naye akiwa na timamu ya kutaka kufanya jambo lisiloonekana na likaonekana kama ni jambo limefanyika,ikiwa tu,kwake naye lilikuwa ni lengo.katika kujiandaa kuna mengi ili kufikia mwisho,mwisho ndio timilisho la maandalizi ikiwa hapo ndio tunaweza kujua kama ni maandalizi yalikuwa mazuri au la kuwa vyote hivyo inategemea na mtu kufuatana na (ma)lengo lake,USHINDI ni pale mtu anapotimiza lengo,ikiwa tu alijiandaa,hata mara nyingine ushindi huja kwa watu wasio jiandaa,na hiyo siyo ya kuitegemea ikiwa ni bahati,wala hatuwezi kusema ushindi usio kuwa wa kutegemea ni ule wa kukosa.tuna hitaji ushindi ili kutekeleza mambo yetu,tunahitaji kujiandaa ili tuweze kushinda.

useme ni wangapi wanaojiandaa,na utakuta ni wote maana kila mtu ajiandaaye hujiandaa mwenyewe,yule anayeandaliwa ni lazima ajue kuandaa pia kwani endapo akishinda hataweza kuulinda ushindi ya kuwa hana maandalizi useme wale wanaoamka ndio wa kuweza kujiandaa kwani walikuwa wamelala,na wale walio lala ni kuwaamsha ili waweze kujiandaa ikiwa ushindi mtu anaupata pale hasa alipojiandaa mwenyewe,maana unaweza kuja kidogo ama ukazidi na kufanya karaha,kivingine ikawe ni ile bahati maana haukuwa wa maandalizi yale,ushindi wa bila kuongea unaweza usisikike,na mara nyingine ukiongea sana wanaweza kunyamazisha,maana wao hawamjui mungu na labda nisiseme hivyo zaidi iwe wanamjua mungu wao.pale unapokosa ndio pale majibu yalipo,ni kama pale unapopata ingawa haitaweza kulingana,ni tofauti ya kuwa moja ni ushindi nyingine ni kinyume yake.

Kile kinachoweza kuzuilika ni kile kisichopangika,maana kitakaaje?kama maji hupita kokote,hata yakaleta uharibu hata ikawe sio lengo kubomoa,pale yanapobomoa yenyewe ushinda ikiwa yalipotoka yalikuja na yakabomoa,labda yangeenda pengine ili ungejua kuwa haikuwa lengo,na iweje yangefanikiwa ungeeiita ni bahati yake,kwa yule anayejenga ukuta kwa ajili ya kuzuia maji hayo anajiandaa,kwa yule anayeyasubili yaingie mpaka ndani basi atafanikiwa,maana amesubiri hivyo,muda mwingine huwa inakuwa haiwezekani,ikiwa katika hali ya kawaida hasa mtanzania ikiwa wengi hatufahamu mazingira yetu,ikiwa ni miili pekee tunayoifahamu,tukisahau mazingira mengine tukataka afya bora,hii itakuja kwa kunenepa ikiwa ni bora basi itakuwa bahati,siwezi kusema sana hapa labda tungeulizana nani au na flani wanapenda nini,maana utofauti upo,na matokeo sio maandalizi,ikiwa yenyewe yakawe na kusudio la kuleta ushindi.

Vizuizi ni haki kuviweka pale unapojiandaa.lakini ni pale tu utakapo jua ni unazuia nini,Katika utofauti wa malengo tuseme yawe yanayofaa yote,yakitofautiana kwa mabaya na mazuri kwani tunaweza kuchanganyana kwa muda mbadala,endapo yale yasiyokuwa ni malengo kufanyika kama malengo wakati Fulani,yule anayejiandaa ndiye anayejua lengo hasa,labda na ije tofauti..hapo tunasema anapanga mungu.
mda mwingine lawama hazifai labda ujue nini unachokifanya,maana kama ni unajiandaa na imetoka kipindi maandalizi yakawa magumu unaweza kuyakimbia endapo haujafahamu unajiandaa na nini, 

'tutaishia kunawa maji ikiwa na chakula tumekiona mbele yetu'.
kwani hata meza zenyewe waligeuza kitambo!!

By:          Benson G, Makaya,
Tel:         +255 714 33 66 57.
email.   bensonsmakaya@gmail.com

Makaya's Forum: ELEWA 2

Makaya's Forum: ELEWA 2 :   Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye n...