Wednesday, July 18, 2012

HALI BADO NGUMU..


Maana bado inaendelea,hali kuwa ngumu.ikiwa kwa mara ya kwanza tulipoambiwa tukajifanya tumeelewa tena sasa tunaambiwa turudie tunashindwa kuelewa.tumekuwa bidhaa sasa mpaka tukashindwa kuzuia upepo,tunapelekwapelekwa tu,hatuna misimamo zaidi ya kugombania vyama,tunapumbazwa na sifa badala ya maisha yanayotuhusu,maana tunataka haki pasipokujua haki tunapata wapi zaidi na badaye ije tumlaumu mtu,eti aahh Yule hakuwa kiongozi bora,sasa tunataka nini,maisha bora,kiongozi bora,chama bora au wewe bora?hata nisifahamu maana kila mtu ana kujifahamu mwenyewe.

Kesho tuangalie tusije gombana,maana hivi tunavyoenda bila ya kuelewa hiyo inaashiria jambo bovu,maana tutaenda kinyume na maana ya mwongozo,hata kama ni mbovu.nzima ipi?hata hivyo hakutunga yeye..hamkujua ya kaisari anapaswa apewe nani?,sijui hata tutajengaje maana kila mtu atataka kuujenga mnara wake,ili uwe wake ndiyo ndiyo hapo tutatofautisha ujuzi na pesa,mwenye nguvu atajenga tu,kwani we hujui namna ya kufyatua tofali?haina maana ya kuitwa mtanzania kama ni mchina.

Haina maana kumkataza mgeni asiingie na wakati ni kwake,maana ameshanunua sasa tunataka kuwalipa mara mia au?mkubwa akielewa amekosa sio kumchapa mkubwa mwenzake,leo tunaondoka bila taarifa,samahani hivi bunge la nyumbani litaongozwa na nani?kama mama na baba wote wamechukia,na familia zenyewe zilivyo za kihindi kila mtu anataka aonyeshe hasira zake,rudini bungeni jamani..swala la kukaa chini na kuangalia ni nini kifanyike,maana tutagombea viti huku watu wanaendelea kuteseka,maana sijui mtueleze mnang’ang’ania nini na wakati mnashindwa kusaidia watu walio katika msaada,hapa mahala hapata kuwa sawa, hali bado inaashiria  vigumu.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...