Friday, September 21, 2012

MFUMO WAKO


Leo umetaka kuongozwa na nani maana inaashiria mfumo unapajua  unapoelekeza ,pengine ikawa vyote ni vya kijani,kwani kwa vile vinavyosemeka vikiwa na lengo la kufanyika hali kadharika ikawa ikifikirika tumbo la kila mmoja ili ikaeleweka imependeza,maana kwa sasa usipofanya wewe utakufa masikini,hivyo watu wameamua kunyanyuka na kusema nataka bila ya kujua shauku hasa la mioyo yao,maana siyo kila njaa inahitaji chakula,fikiri umeijua njaa yenyewe?pengine hata na chakula chenyewe kiwe tofauti basi.

Ni wazi zinalika,ni wazi utaifa unapotea kwa sisi wenyewe.ikiwa ni kweli wananchi wapo makini,ikiwa ni kweli viongozi wapo makini,hapa hakuna aliyemkosea mwenzake kwani hata Yule anayeongozwa afikirie kuongozwa,zaidi ya kutaka kuongozwa vile unavyotaka ni kutaka kuwa kiongozi.kama umelima mchele na umevuna mahindi jua shamba si lako,na kama uliweka alama ya kusema usipotee basi mshukuru mungu wako kwa maajabu ,maana yatakuwa yamtendeka.la sivyo badili mfumo wa kulima.

Mashati hata tukishikana yatachanika na tutabaki watupu,bila kuelewa mfumo haitawezekana kwenda mbele wala nyuma,wewe ambaye upo katika mfumo ndiye utafahamu maana na mfumo wake unaweza kuwa umeelekea kule unapouelekeza au ulipoelekezwa bila kujua kama unaendana na mfumo wako,maana pengine kwa wengine ikawa ni lawama kwa namna ya hali ilivyo,hizi siasa zinaweza kubadili hata mfumo wa maisha yako.Wenzetu wanatumia lugha’system’kukiwa kuna kila aina ya maana ya neno hilo kutokana na yaliyopo.

BADILI MFUMO WAKO BADILI MATENDO YAKO

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...