Tuesday, June 12, 2012

KULA BATA..

Unapofika wakati ni lazima kuacha,embu tazama wengine wakiwa tofauti na wengine,hapa tukiendelea kujua zaidi ndiyo tutagundua kwamba pengine wengine waliacha,maana haya mambo yamekuwa tofauti sana,si ya kuwa watendaji ni tofauti,si ya kuwa kuwa matukio ni tafuta,hapa tukatambua lengo kwanza.
 
Najaribu kushirikisha nafsi naona hazifanani,labda tushike manati ili kuleta ushindani.hapo ndiyo ikajulikane tulipotokea,hapo ndiyo ikajulikane ilipotakiwa maana ilipasa tuwe huko,isingekuwa na sababu bila ya kusema nini,yaani nini ni kuhitajika pale jambo linapofanana na mazingira.



Pengine tunahitaji mashine ili tukazifanyie kazi,ikiwa elimu ni msingi hapo hakuna ushindani,maana kama kimeeleweka hivyo asiyekuwa na elimu atabaki na lake,pengine ni ujuzi tu,hapa katika kusoma lazima tupate uwezo na nadharia za kufanyia kazi na hapo ukaitwe uzoefu.

Baadaye inakuja sasa watoto hawatakiwi kusumbuka kama baba zao ilivyokuwa,ikiwa wazee walikuwa wanatembea zaidi ya kilomita hiyo ikiwa sio ushindani labda Fulani anahitaji kuwa namba Fulani,raha mtu anaziona za mwenzake ikiwa taabu ipo kwake,

Pengine bila kulinganisha nafsi zaidi tutabaki na kuendelea kuwa hivyo,imekuwa inafanana sasa kama ilivyo kwa nyoka na chura,basi mmoja ataruka ruka na mwengine kutambaa hiyo  yote ikiwa ni safari ya maisha yao,na katika kuishi maisha  ni lazima kutaka mazuri.
Ikiwa bila taabu na sababu kwanza,basi lazima tufanye kazi,lakini hapa inategemea na taabu,maana taabu si ya kwako tu,pengine tuchague muda wa kufurahi,na tutafurahi kweli kweli.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...