Friday, November 18, 2016

SHIKA YAKO

Kamilisha mipango yako ukitilia maanani kwa kile chochote ukahitaji kufanya katika namna ya kukataa kujilaumu na kukwepa lawama,Utapatwa na mshangao kwa kuona Yale yanayotokea halisia sio kama vile ulivyofokiri, ukiwa na fikra zilizochanganyika na Mawazo ya aina nyingi yenye kujua lipi ni tusi na lipi ni shukrani.

Nashukuru sana Mwenyezi Mungu kwa Pumzi yako kwa vile utakalo wewe hutimia, nakumbuka mengi machache sio kama ya mwengine, Asante Nimekuja duniani nimekuja uwanjani pengine ni mchezo unaohitaji hasira na nikakasirike tofauti.

Watu wanaona wanachowaza wao juu ya wenzao ni sahihi zaidi, yaani mtu anaamua kumwamulia mwengine kwakuwa tu labda wametofautiana katika hali zao hasa katika uchumi wa binafsi na pengine ikawe ni tabia na kujifanya nafsi ya mtu iko mikononi mwao. 

Maisha hayana uelekezi wa moja kwa moja yakakupa kanuni ili ufanye vile na ukafanane, binadamu tumetofautiana katika hali nyingi hasa ikiwa ya kwako umeyaweza Leo mwache kesho aweze mwengine unayemwona kashindwa Leo,haina haja ya kumsemea ikiwa kinachofanyika sio kosa kwake.

Ondoa wivu na roho ya kukunja katika lile jambo aliwezalo mwengine, ikiwa hujui ni bora kuuliza na kumwacha mwandishi aende na faida zake kuliko kusemea kitu kinachokuhusu wewe na kulinganisha na utofauti wa kile anachokifanya mwengine ya kuwa binafsi huna uwezo nacho.

Leo nikiangalia baadhi ya mambo yaliyoonekana na kusema hakuna aliyekamilika katika dunia hii yenye mengi, watu tumetofautiana chaguzi mmoja akaona kibaya ni kizuri  na mwengine akaone kizuri ni kizuri hiyo yote ikiwa ni kutaka kuona mazuri na kuukataa uhalisia, au kuukubali katika namna yake. 

Uhalisia huja katika pande zote lakini binadamu uufanya uhalisia wake pale anapopendezwa nao yeye, ni kheri kukaa kimya kuliko kusema kitu ambacho hakiwezi kufutika maana na kuleta uhalisia tofauti, kwani yanapokuja mabadiliko fitina na uwongo uliokithiri unaweza kuharibu picha na mtazamo wa maisha yanayokuzunguka.

Sibishani na mtu ili akapata faida,aliyetaka kuelewa aliuliza mapema kile kinachohitajika kufanyika na kikafanyika , hakuna haja ya kulazimisha kujulikana kama unajua na wakati haujui, anayefanya jambo moja huacha kutokana na mtu mwengine karibu kufanya jambo lile lile, na aliyeamua kufanya jambo hakatazwi kwa maneno ama kwa  kile kilichofanywa,na akiacha isiwe kwa maneno maana kuna binadamu wanajua ya wenzao kuliko wenzao,wakijiweka wao bora zaidi ama tu kukuchafua kwa vile mpumbavu hachagui neno la kukusemea,

Shika yako na mwache mwengine akiendelea zake.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...