Monday, November 5, 2012

CHUNGA KAULI..

Hata zikiwa nyingi wachache hutaka moja tu kauli kuielewa,kwa kujua kwa yale mengi hakuna wa kuyaweza naye.ukisikia kauli lazima uishike isiwe kauli  nyingine zikasahaulika,ama ikaonekana vile walivyosema wengine,kwamba kauli ya mtoto kumwambia mkubwa yaweza kuwa makosa ki heshima,lakini siyo ikawe mkubwa kwa mkubwa mwenzake,ikawa si hekima,maana itaoneka dhambi kwa kujaribu kuyafanya ya juani wakati kauli nyingine ni za gizani.

Ni wazi hakuna lililo sahihi zaidi yako Mungu,kwa Yule anayebisha ni sawa na kufananisha ndiyo na hapana ,ukikaa na kukuwa bila kuelewa utanawa sana kichwa kwa kupata moto tena hutaelewa nini cha kufanya pengine ukiwa haujafanya kitu hapo mwanzo lakini kauli zako zikakukuponza.

Ninatoa kauli yangu pale inaponibidi ikiwa nazijua haki zangu,akili yangu inajua cha ziada nje ya mwili kinachoendelea,hivyo kauli yako yaweza kukuliza ikiwa hujachukua dhamna ya kuyabeba majibu yatokanayo na kauli zako,ni mizigo ya ndani,wachache wanafunzi huelewa nini mwalimu anachofundisha,maana kila mwanafunzi anaelewa yake pale inapokuwa nafasi na wakati wa  kila mmoja kutoa kauli yake katika uelewa

Ni kweli kauli nyingine ni makosa sana kutamkwa,si vyema kusema kitu usichokifahamu na kugeuza kauli yako ya kweli,ni wazi hata samahani isimaanishe kitu hata ikawe kwa mtu kuuana na mwenziwe.kauli nyingine hazitakiwi kukumbukwa,kauli nyingine zina maana ya kuleta kauli nyingine zisizo na maana.Chunga kauli.


Friday, November 2, 2012

NISHIKE..


Utawaza kushika maneno ya bwana mungu kwa kuwa yapo katika maandishi na kujifanya kujua kusoma,maana ni wazi kama angekuwa mbuzi sababu zingepigiwa mstari kwa kuwa ni sahihi,pengine ili kutokupigiwa mstari tukae ukinishika mkono kwa kunielekeza,maana pengine naona giza,huo mwanga siyo kama huu,huo nahitaji kushika kwa kunipendezesha,acha harufu kwani umepuliza wa kutosha sasa angarau nikaotee jua,najua japo nikishika moto pengine nitaotea kwa yale mema kuwa mabaya,kwa ule wema kuwa wa mbaya.

Ukishika bilioni lazima utakuwa billionea,ukishika maneno ya bwana mungu wako lazima utakuwa mtoto wa mungu wako,pengine ikiwa umeyashika kwa sababu ipi,ikiwa umeyashika unayoyajua wewe,kesho mwanafunzi anapofeli darasani aulizwe nini anataka ili afauru,pengine isipokuwa kwa kushika ramani ama kuleta amani.maana ikiwa umefeli umetaka kushitaki,haina maana kwa waliofauru kwa kutokwenda kushitaki.

Hapa kunaweza kuwa na chaguzi hasa zaidi katika yale mazuri na mabaya,yale ambayo mmoja akayaona kuwa ndiyo na mwengine akasema  kwa mshituko kwamba siyo,kuwa na imani kwa lolote lile unalohitaji kulishika,imani ya kushika unapohitaji siyo ya kuthubutu endapo kukiwa na mahitaji,tabu zikamfanye mtu ajitambue zaidi yakuwa ameshika yale yaliyomletea taabu ama raha zaidi.ama tuyashike yale tuliyofundishwa zaidi.

SAHAU.


Kuna muda yapasa kujifanya kutokujua kwa kusahau pengine ikiwa ni makusudi ama vile ikawe ni mpango wako mwenyewe,kama ungejulishwa lile lililo katika ndoto zako ndiyo ukweli hakika ungeamini yako,sasa unaweza kuwa umesahau,muda huu unaweza ukawa kama siyo yale uliyokuwa unayaota kwa kuwa ni haki ukweli upo,pengine ukiwa unaamini yako kwa kuwa ndoto hazikusema,ama zimesema lakini umesahau kwani mambo na yenyewe ni mengi mno kwa kujichanganya na nafsi.

Utasikia huyu mimi simpendi,hapo akiwa ameshindwa yeye kukupenda,ikapita dakika kwa yanayofahamika ni lazima kuwa wazi,maana pengine unaweza kutega kwa kusahau,ukijiuliza umesahau yapi kama siyo unayoyajua,maana mapya na yenyewe yanapokuja huleta utofauti na yale ya mwanzo,hawa wa kwanza wakiwa wamekula sana,ikiwa siyo wa kwanza kabisa wao hawakula na wakijifanya wamesahau,na kwa muda unavyokwenda hawa waliokuwa hawajui imekuja kujua,maana kujitambua.

Kesho sahau sema jana nilisahau,usisubiri kukumbushwa maana wengine wanakusahaulisha kwa lazima,wakitaka kukamilisha kauli ile ya kutokupenda mengine yamekuja baada ya wengine nao kuota tofauti,wakiamini kusherehekea ndoto za wenzao kuliko yale ya kwao,unaweza tangaza vita kwa kupotelewa na siraha  bila ya kujua kama ulikuwa hujui matumizi yake,nisisahau mimi Siraha,Nisisahau mimi siku za vitani.

Tuesday, October 30, 2012

KAULI NA VITENDO


Unaweza kusema unataka kushika na wakati bado hujashika, ikiondoka dhana ya kwamba haujui, pengine kisifuatwe kile ambacho Yule mmoja akasema,maana ushauri unapatikana kwa kila mmoja, unapofanya yale yanayo kufurahisha maishani mwako usijaribu kuifananisha na kwa mwenzio, maana Kauli zinaweza kuwa sawa huku matendo yakiwa tofauti.

Usifuate mkumbo kama  hujaweza kutoa kauli, kubali unapokosea si ya kuwa hakuna aliyepatia, nikisema mimi nimesema mimi, nikisema sisi basi tumesema Pamoja, mengine huwa yanatia hamasa ya kufanya ikiwa yanaeleweka mambo yaliyozoeleka hufanyika kwani yanaeleweka na isije ukaamini  sana lako ambalo limefanywa na mwengine.

Siwezi kusema kauli zangu ni nzuri kwani hata wengine wanayaona matendo kwa namna ile wawezavyo, matendo yako yanaweza kuwa mabaya na kauli zikafanya kulainisha matendo hayo. simaanishi mmoja akisema nenda na wewe uende, bali ikawe mmoja kasema nenda na ikafikirika utaendaje, tofautisha kauli  yako kwa namna unavyoweza kutenda, ama matendo yako ili kuweza kutamkwa.

BABY GIRL..

A BUTTYFULL BABYGIRL

ONCE SHE CAME INTO MY LIFE....I  felt no regret as what was going it was just the pasts, but it came a time she deliver something to me, That’s love.

Once you see her smile, you can smile too...once she cry, know she cry for you two, you are genius my beautiful baby!! she knows how her parents feel for her, she knows why God created her, she is an angel, she gives comfort when sadness, she love when you give ,you are the future beautiful role model of mine,im proud for a beautiful baby girl.

She always keeps me fight for I have her, she always gives me hopes for how she use to try, when she try and keep trying, for the love I have I give you a million my lady, I’m sorry for not being there when you needed me, I would love to hear all that your beautiful words and posses you have. Shine my girl my time is not enough .

I better keep all your beauties in my heart as you seem to show it all,
 I LOVE YOU MY BABY GIRL.

Monday, October 29, 2012

USHAURI.


Hapa hakuna nasaha maana si la muhimu kwa yeyote,kwa aliye na umuhimu wa kutaka kuelewa hukaa chini na kusikiliza ushauri,ushauri  si wa bure,ushauri ikiwa ni njia za kutaka ya kule,pengine ukaja japo mchango maana wengi wao wameshauri sana,maisha ya mwanadamu hayapaswi kutembea na ushauri,maana haifai ikafika siku na ushauri akafa bila ya mafanikio,maana kama mwanadamu unashauriwa unastahiri kushaurika.

Mshauri si ushauri,pengine ikafikirika tofauti ya kitu na mtu,kheri ya vyote kuwa wote,maana unaweza penda ushauri bila ya mshauri,kubali yale unayoyafikiria ni kweli,ikiwa umekataa hata kwa kushauriwa basi ni kheri,huu wangu ushauri naupeleka kwako ili ukashauri,pengine mkiwa wawili wewe Pamoja na akili yako,zako ni uwingi usioleta namna ya ushindi maana umetajika kwa wingi,hapa tukasema heli mchina mmoja kuliko mabata kumi,maana kazi ya bata ni kula,kujisaidia na kuogelea.ushauri  mwingine huja baada ya kujua machache ya mwanzo pia

Haifai kukataa ushauri ikiwa umekuja bure,leo kila kitu kimekuwa bidhaa na matapeli watakao kuja hawata taka hata senti,maana wao walishazurumiwa haki zao kwa kutokupenda ushauri,ushauri wa mshauri ni kushindwa ushauri,maana mwanzo ikasemwa pokea ushauri wa bure ili kufikiri zaidi yale yako,maana pengine haikupaswa kushaurika zaidi ya kupokea lawama za kutokushaurika.

SIMAMA...


Haitakuwa njema kwa kuokota bila ya kumfikiria Yule aliyedondosha,haitakuwa na maana ya kuinama bila ya kuangalia pale utakaposimama,leo ikiwa inazungumziwa sana ni lazima kuifikiria kesho itakujaje,yamekuwa magumu sana kwa kulinganisha namna za kufanya,yaani mambo huja kwa kuwa yana njia zake,ikiwa kitu kimedondoshwa kisije bahati ya kuwa umeokota,mara hapo ikafanana na namna ya vidude vilivyo ama ndiyo bahati zilivyo,fikiri endapo utasimama na kukuta umeokota mke,maana ndiyo bahati yenyewe.

Usipojua leo ule nini kesho huja na kukufanya  ushindwe kula hata maini,nimeona mengi..umeona mengi,,ikiwa unamsemea mwenzako ana nini fikiri ya kuwa umefanya nini,fikiri endapo umefanya nini ni sawa na kesho ikaja na yako yakawa kama maini,maisha ni mapambano..maisha ni kusimama vijana wakisema kidete,kwa imani yenye msimamo ndiyo kuweza kufanya vitu vilivyo simama,hakika haina haja ya kifikiri wakati hauna uwezo wa kusimama,japo  kiakili.

Usiogope ya  mtaani kwa kuwa bado hujasimama,usiombe samahani kwa kusema kana kwamba unataka kusimama,labda kwa waliokuwa wamesimama wakae,ama kwa ilivyo kusimama na kuwaziba walio mbele,hakuna anayeweza kukueleza yale unayoyataka ikiwa yamesimama katika fikra zako,pengine ukielewa tofauti ya jambo yapasa kusimamia lengo na kueleza Mawazo yako.

Makaya's Forum: ELEWA 2

Makaya's Forum: ELEWA 2 :   Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye n...