Friday, August 17, 2012

KUKOSA SIO TATIZO..

Tatizo ni kwangu maana hata muda bado unazidi kwenda,nimekosa leo nikitegemea kupata kesho,ikiwa kila mtu ana kipato chake,kwa upande wangu sijapata na ikiwa kwa upande wangu ulio kwako umepata basi uhaki kuisubiria ahadi yako kama vile ninavyoisubiri,matatizo ni namna ya kuweza kutafuta,maana kama hautafuti kwa nini una matatizo?hapo ndiyo utasikia wakisema lazima kuna mchawi hapa.maisha mchawi ni wewe,hakuna mlinzi mzuri wa mwili wako zaidi ya wewe mwenyewe,hivyo ukishindwa utajiletea matatizo,tena ‘matatizo’ ni kama ‘maisha’ maana yenyewe yana mazuri na mabaya.

Duniani ndiyo mahala pa kuishi,utasikia ikisemeka kwamba duniani maisha magumu sana ,sasa wapi rahisi,unapoona nyuki wanakukimbilia na wewe kimbia,kwa mfano wa kuku anapotakwa kuchinjwa siku yake inapofika,maana siku yako ikifika hapo utajua tatizo,tena yenyewe huwa hayana hodi wala kalenda labda siku fulani yapasa kupumzika ili kusherehekea,maana itakuwa imepatikana.pengine matatizo yako ikiwa kama ni raha ya mtu mwengine,wewe unacheka wengine wanalia.hapa ikiwa lazima ujue umekosa nini.

Tatizo ni sehemu ya maisha ya mwanadamu ikiwa ameamua kuishi,wengine wanakata tamaa kwa kuona maisha magumu,kama wale wanoenda shule na kuacha,ya kuwa shule ngumu,na bila kugunndua baadaye itasemeka ni kwa sababu shule haikuenda.maisha yenyewe ni shule,matatizo hasa ndiyo yanayomfundisha mwanadamu,kuna mengine yale yanayokosekana yakaonekana kama na yenyewe ni matatizo,sasa kama yakija na yenyewe kwa matatizo yake si utakata roho kabisa?labda ikiwa ni furaha..,maana kama kile kilichokuwepo kimekuwa tatizo basi hata  kisichokuwapo haina haja ya kukisumbukia maana tutaongeza matatizo tu.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...