Thursday, October 18, 2012

BAADA YA HABARI....



Huwa yanakuwa mazungumzo kwa kuwa aliyeleta habari alidai kumaliza kutoa maelekezo,leo ukiwa unazungumza kwa kutaka kuhadithia habari bila kujua hiyo ndiyo habari yenyewe,pengine ikawa ni taarifa kwa kuwa habari yenyewe ni kama muhtasari,ukijaribu kuonja ni vigumu kuondoa ladha tumboni,labda isingetangulia taarifa basi hakika ingekuja habari kamili ingawaje imeonekana hakuna aliyesikiliza habari kwani baada ya habari kuisha mazungumzo yanaweza yasiendane na habari.


Haki sawa kwa kila mwanajamii,haki si sawa kwa mtoto na mkubwa,labda iwe umesikiliza tofauti na kuona mageuzi katika kichwa cha habari,lakini mazungungumzo yaliyofika baada ya habari yameonekana ni habari yenyewe.mengine hayapaswi kuyazungumzia humu maana wengi wao wamekuja kwa kasi wakitaka japo kuelewa kichwa cha habari lakini wameonekana wataelewa habari yote ikiwa bado umri hauruhusu.


Msomaji wa habari anapaswa kuwa kama daktari,maana kuna mengine yametukia sasa hivi,kuna mgonjwa ameingia wodini baada ya daktari kumaliza muda wake wa kazi,muda mwingine ni wa ziada,muda baada ya kazi..ukifanya kazi muda baada ya kazi bado huitwa ni kazi lakini unakuwa umejitahidi kwa kuzidisha muda,pengine ndiyo huwa ni kazi nzuri zaidi,pengine huwa ni taarifa nzuri zaidi..ikiwa mtangazaji kamaliza habari labda atuletee mazungumzo ili ijulikane baada ya habari nini kifuate ama kilifuata.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...