Friday, October 5, 2012

MCHANGO..

Napenda mchango wako katika kusherehekea kuwa mkubwa,pengine ili kufanikisha mahala au kitu fulani,mchango wako utanisogeza kwa kuwa umekuwa mtu muhimu sana katika maisha yangu,pengine mungu hastahiri shukrani ya kuwa ni zake,pengine isiwe katika kuchangia pumzi ukashindwa msujudu,ukitaka vile utakavyo,ukiwa huna shukrani.maana kama kilitoka kidogo haikupaswa kusemeka kama ilikuwa ni kidogo ya lakini zaidi ya kushukuru,kwangu mimi nashukuru sana maana mchango wako umenifikisha nilipo.
Unaweza kudharau kwa kuwa ni kidogo,ikiwa hujui mchango mdogo ni mkubwa haina haja ya kufanya,leo usikae ukasema unataka mchango utakao kukidhi kwa bila ya kudhani kwa wengine,maana hata kama umechangia lakini si lazima kuchangiwa,changa wewe ili ikijichanga ufanikishe malengo yako,ikifika mwisho wa siku yasije maswali ukashindwa kuelewana kwa kuchangia kidogo,sina maana ya mchango wako endapo unategemea nikuchangie,zaidi kinachohitajika ni shukrani.Shukuru pale unapochangiwa,mungu ametuchangia vingi sana,haina haja ya kutokuelewana na kuchangia kidogo.
Haikuwa na maana ya sherehe katika kufikisha lengo,haikuwa na maana ya matajiri kutoa michango,alisifika Yule maskini aliyekuwa hana na kutoa sadaka kama mchango nzuri,kesho inapokuja usifikiri kurudisha yale ya leo na kuyafanya,maana ukiwa mkubwa utachangia wadogo kufanya vitu vyao,na hiyo ni njema katika mbingu kwa kuwaacha wale watoto wadogo kwenda zao hata wasichange,huo ukiwa ni mchango wako mkubwa sana.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...