Tuesday, June 5, 2012

JANA NA LEO.


Jana ikawa siku ya maandalizi na leo ndiyo leo,ndiyo ikawa na maana ya uangalizi pale la muhimu likawa matoleo,ikiwa kwa mara chache yakikaribia usoni huruma kwa mwenzio,ikiwa mara chache yakikaribia rohoni ya nini kwa mkeo,hakuna asiyependa maana maadui wapo,hakuna asiyechukia maana tunaopenda tupo,maisha yameharibu kuta kufanya nyufa na kuonekana leo,maisha yameharibu vitu kufanya watu na mahusiano yao,isiwe hatari ya mwenzako ikawe kinywani baada ya kileo,isiwe adhabu ya mwenzako ikawa samahani kwa leo

Pengine umechelewa kucheka,pengine umewahi kununa,maana ulipaswa kucheka jana na kununa leo,vile ikawa jana na leo,pengine hata mavazi ya jana yasionekane ni yaleo,tutasahauliana jamani tusijefanyiana ya haya ungeyafany a jana,usijeugua magonjwa ukasema yamekuja leo,ukitafuta sababu na kurudi jana na kusema walipasa,walileta wao.

Mengine haina haja ya kumwachia mungu,pengine haina haja ya kumsemea ndugu,ya leo uyaache ya jana kafanya nani uangalie usije vuna mabua ukaja fanana na nyani,ya dunia yameongezeka na hizi pilika kiu zikijaa vinywani.

Ya leo yamekuwa machache kwa imani ya wasio tamani,ya jana yalikuwa mengi kwa imani iliyotamani,maana umetaka uje sasa,maana umetaka ufike leo,kumbe ulitamani yale ya jana yaje leo,kumbe haujatamani kwa ya leo yakafika kesho,hapana haya ya leo kwa kweli yabaki hapa,yaishie hapa na kama yakitaka kuondoka yakaenda basi yarudi jana.

Kesho ije itatukuta vizuri,kesho ije kama ni kuta
umezipamba vizuri,

IKULU..

Kule kwetu kuna mahala panaitwa makunguru,ali hali ingalikuwa nzuri tungalihamishia ikulu,



  

mambo yamekuwa mengi hata ya kujistili nayo yamekosa uhuru,ikabaki kupuuza uliyonayo na kusubiri msururu,maana vya kugawiwa  na yenyewe imekuwa ndiyo vinakunusuru,ikidhihilisha nia za watu kuelekea ikulu,ubadilishe maana na tafsiri ya  safari yako usije kupata laana yasiyo ya maana kwa sababu pengine hata sizo zako,ikulu ni patamu labda ujaribu nafsi yayule,ikiwa kila mmoja anayo nafasi ya kuona kile akifikiliacho,ikiwa kila mmoja akitaka yale mazuri machache kumfikiapo.

Matunda yametoka mtini pale,vijana wahini mwende illi mkayale,miti isije kauka mashambani,kijana ufanye hima usilale,pengine wakati wa kueleweka ndiyo huu,ikiwa watu wanahitaji kuelewa tu,kujua kama iliyopo ndiyo sahihi na hakuna nyingine,maana zaidi utafanya kukopi na baadaye kutoa kile kilichotoka,hapo unakuwa umetohoa,usipende viongozi hao,kila aliye mtu aonyeshe nguvu zake na ainuke,shamba liko tayari kwa kulima na miti ni michache,shamba limekuwa laini kwa kulima kwa wa mjini wachache.

Kuitangaza nia sio kama kuzamia,kuitangaza nia sio ya kutaka kushika mkia,maana wa kuongoza akiwa ametangulia wakuongozwa hupaswa kuvumilia,sio zikaje taabu ukasema ungevumilia,yatakiwa upate sababu na moyo kuutia utaishia njiani pale madongo yanapokujia,yataishia kinywani kwa kidogo utakayopatiwa.usiumize sana matumbo kwa kula chakula na mawazo kufikiria,usipate presha sana na moyo wako kwa uwoga wa kutokuchaguliwa.

Leo twende kesho wengine walitangulia,kwa uchache uliopo usipofanya leo ya kesho ni kwa wengine kuwatukia,yapasa sasa ukiwa na imani utaingia,yapasa sasa kuomba ruhusa ili ukafikirika kuingia,haujabuluzwa sana kwa nguvu ukaingia,haujaambiwa sana kwa macho na masikio yakasikia.unaisubiri kesho ije maana wengine walitangulia,unasubiri kesho ije maana majibu yalitangulia,maswali ya leo umetakiwa kujibu kesho kwa kuamkia,maswali ya kesho ujibu leo ukifikiria,ikulu imenona kwa utamu ninaouhisia,ikulu sio Dodoma ni dare s salaam naskia!

Ngoja tuache tuone na utasikia,maana ya kesho kwa wengine ni vigumu kuyafikiria..

TAFUTA..

Ombeni mtapewa tafuteni mtapata,imani na kweli ya mtu kumwelewa,ama imani kujielewa,vyovyote basi na majibu tukayaelewa,leo ni mara ya ngapi nairudia,imekuja sasa naurudia,kwa kuwa umekuwa ni mziki mzuri,pengine kwa kuwaona watu wakicheza,pengine kwa kuona mziki ukicheza wenyewe maana watu wanaweza kucheza vibaya kuliko mziki ulivyocheza wenyewe na hapa tukasema ni makosa ya mtegenezaji ikiwa hatukujua Yule aliyeimba,wimbo huu mtamu kweli,Tanzania Tanzania nitaaiimbimbia daima.

Kwa ufupi tukaja bila kuchoshana,kwa kirefu tukaja ili kuelewana,watu wamekuwa wakali kwa ngoma wapigiwayo,watu wamekasirika kwa ngoma na unyago,pengine tusijue kuucheza tukasema tumeweza maana wengi wao waliotangulia walikuwa wakijikweza,hizi sio stori kwa watanzania walioko jikoni,hizi sio stori kwa watanzania ambao hawaoni.

Hapo nakasirika,hapo nakumbuka,maana kweli mwisho tuweke nukta,tukija huwa tunaeleweka,tukiwapo huwa kinasomeka,kwa wale watanzania walio na hulka,sio kwa vina tukasema yamesababishika sio kwa kina tukasema tukasemeheka,pengine makosa yetu yakawa yao,pengine dhambi zetu wakabeba wao,dunia imekuwa ni chungu kwa kuelekezwa na mtandao,dunia ya kuchunguria haijafanana na sufuria zao.

Mbishi mbishie akitaka jibu mpatie,mjanja msikilize akitaka swali muelekeze,maana hawa wajanja wamekuja wengi,pengine tukawaita majina yao,lakini wasifanane na wayao,pengine tukajiita majina yetu na wala yasifanane na yao,kati na kati wametuweka pembeni yao,karibu na kati yatupasa kufikiria majibu yao,hivi ni vichache baadhi vipo kwa wao,mengine ni machache labda tuanze na kwao.

Tunaondoa uwoga kwa kuomba kilichopo,cha baadaye wacha kije kwa msimamo uliopo.sikubali leo kiduku kukitilia mkong’oto,sikubali leo kwa watanzania kuishi katika maporomoko,tukumbuke leo kwangu kesho kwako,tukumbuke ya leo yangu kesho yako.

tafuta,tafuta iliyo ya kwako..Tafute kile kilicho chako!!

Monday, June 4, 2012

MKAO..

Tuchague pale tunapofanya,tunakuwa kwa vile hali zinatufanya kwa kuchanganya na mengine ni kama kutoa,labda pale tunapofikiria tofauti,zikiwa hazina idadi kwani ndiyo hatutaelewana,pengine tuendelee kutoelewana,yanaskika mengi yanaogeleka mengi na ndiyo tuendelee kuyatenda hayo,tukiwa hatukutaka kutenda mojamaisha ikiwa ni kutafuta tu,tuseme njia ndiyo zinauwalakini muda mwingine tujachague kudanganya,maana tumedanganya mengi sana kama ni kusema uwongotena ni walongo kabisa,muda mwingine tupeleke mbele mambo yetu kwa maana tulikuwa vile kwa kipindi kile,sasa wakati unajificha tena na mambo yenyewe yakidanganya kama itakuwepo tena pale.

Tunapopotea tunajua maana ya kuwepo,ali ikafika tukataka kurudi pale palipo salama maana ndiyo nyumbani,haya yasipoteze maana kwa kutokueleweka ama ikiwa ni kudanganyika tena ikieleweka hivyo iwe ni mtu amechagua mwenyewe,ikiwa kama nafasi inayoshikirwa na mtu wa kwanzahuogopa kuwa ya mwisho,pale tukaseme basi kristu turudie na uje upate mateso tena tutaambiwa tunamchezea mungu ya kuwa alikuja mwanzoni,pengine hata wa mwisho akaogope kuwa wa kwanza,ikiwa kuna bahati ndiyo maana na furaha zikaja,kuwa wa kwanza sio nafasi ya mchezo mchezo hata kwa wale waliopungukiwa akili wa wao ieleweke kwamba mtu huyo yupo halisi katika kuufata uzima.

Usahihi huj ani baada ya kutokea,pengine yaliyotokea si magumu sana bali yalipewa muda,na hapa tukae chini tuone kama muda tuliojipatia ni dhahiri yastahiri kufanya masahihisho,pengine tukawa tumewahi sana na baadaye tukaja kufeli katika namna ile ya mwanzo,ambayo hiyo ilikuwa kama tunafanya na sio kujifunza,pengine tunapofanya mambo yetu tunajitahidi sana,na ikawe kwa mwanadamu kuonekana ni mpaka kuweza,hapa tukijua hakuna kuweza kwa sababu hata ilivyoonekana ni vibaya kwa kusema haikugundulika vile.

Tukae tuote tena,tukae tufikiri tena,tukae tuwaze na kujua yapi ni mema maana kwa kuyatenda mabaya,ama yale mema basi yakawe katika usahihi saidi,yakaunganike kupitia mawazo ya zamani na maumbile ya sasa,kwani kinachotakiwa kufanyika sio tu kulima bali hata kutengeneza majembe kwa ajiri ya walimaji ili kuondoa utegemezi,tukiwa tunategemea sana hapo tunakuwa hatueleweki yakuwa tumeshikiliwa misimamo,hapo tunahitaji jambo ushirikiano.

NGOJA MPENZI..

Nashukuru kwa uwepo wako,usinikimbie ukaniacha mwenzako,nimechoka na mengi huko nitokako,nsubiri karibu mpenzi naja kwako,umalikia na mengine yote sifa zako,nimekaa nakuwaza na hata kwenye mizunguko,Baraka zikujae maisha yaje kwako,busara,utii na tija katika malengo yako,pengine ni fikra zangu pale nikugombezapo,wewe sio mwanangu nikuchunge uendako,umejua mengi mengine katika nafsi yako,napokuwa karibu kufanya ushindi nanyoosha mkono wako,rangi na sura havijalishi tuendako,tukae tufikiri maisha si kunibagua mwenzako.

Nakuwa mshindi pale nikuonapo,nakuwa sishindi pale usipokuwepo,hata nikajaribu kufumba haya yangu macho,imani na mawazo yote yapo kwako,najiskia furaha ninaposikia kauli kutoka kwako,nakupenda ua langu pamoja na familia yako,chochote sitaki ahidi nisitekeleze lawama kwako,ninachokiweza subiri mpenzi muda hujapo,hapa tulipo nahisi kama pepo,hapa tulipo najiskia vizuri ukiwepo,mara nyingine kimwili nisipokuwapo unanishika mkono japo kwa imani kuona kilichomo.

Najaribu tena kurefuka mpenzi nikufikie,najaribu tena mpenzi kujirekebisha ili usichukie,nione peke yangu kwa machozi usintilie,nione peke yangu pendo langu ulifikirie,karibu siku tutaona yaliyonona,karibu siku tutakuwa waliooana.Napigana kesho ya leo yasinisumbue,napigana leo na kesho nikuandalie,karibu sana,karibu sana kwa sebule..hizi zitakuwa bora hasa kwa viumbe watakao kuwa bora,bora tuijaze dunia pamoja,bora tukasherehekea pamoja,ikiwa nafsi yangu ilishakuwa moja,sina la tofauti la msingi kujikongoja,

Mawasiliano kwetu isiwe taabu,mawasiliano kwetu kama kipindi  cha mababu,hali zinabadilika ya leo uizoee,hali zinagawanyika haya ni ya kesho tukayafurahie,pengine tukapate pale ilipotakiwa,pengine pakawa kwetu palipotakiwa,kesho ntakuja kituoni mpenzi ngojea,kesho inakuja penzi letu bora linajongea,isipite siku bila kuongeza,isipite siku bila kuongea,niko pamoja nawe bila kujali dhambi yako,niko pamoja nawe tuyaone mema zaidi yatokeapo,hii ya kwetu isiwe ya kuumiza matumbo,hii ya kwetu iwe ya kuyajaza matumbo hakika tungoje,hakika tusubiri bado muda kidogo,kwani kumbuka furaha ya mtu inatokana na mtu mwenyewe. 

Sunday, June 3, 2012

MY DEAR YUNIA

ni salamu bora kwa ajili yako,pengine uangalie chini na kukaa kitako,ni  gharama kubwa sana 
kwa zawadi yako,hakika unamtukuza mungu wako pengine ni zile aina na namna zako subiri leo uone kesho yako si kutishana bali ni habari zako,mungu wasaidie wengine hata watembeako,muda mwingi  pale jua lizamapo,Kuitana wifi na rafiki zako madada zangu ndiyo wale rafiki zako ntaongea mengi temeke sijafika labda gongo la mboto,ningeona tofauti kwa yale mambo yako,mapenzi bora hujulikana yatokeapo,mapenzi bora ni kwa mtoto wako,nafsi zikaungane na kuwa zako maana ya muunganiko wangu kutoka kwako,maisha ni mafupi tule kiapo,maisha ni matamu japo tuyaonjapo.ufikiri mbele na sio utokako,tufikiri mazuri mpaka tufanikiwapo

Imani yangu ni katika ndoto zako imani yangu ni katika ukifanyacho,maana umekuwa kidonda ,hata ukauma kwa utamu,Mawazo yako yameniinua,nimekuwa mpana wa kufikiri kwa kuona wale wanaotaka kukununua,pengine isiwe siri kuona ama tukaona kwa vile tukasikia,hapa utasikia machache sana kwa kubania  yaliyomuhimu maana imekuja wakati chako kikawa kizuri zaidi,yaani umepitiliza katika unyoofu niliouzoea katika mambo niliyoyategemea,umekuwa kibiriti kwangu my dear,umeniwasha na mwisho nikamalizika umenipuliza kabisa,umeniwasha asante kwa kuitikia,umenilaza na asante kwa kuitikia.

Maisha yamekuwa bora kwangu nahitaji kukutumikia,umekuwa kinara wangu kwa mataa kunimulikia umeniwasha kupindukia,nalijaribu kuangalia pembeni sikusikia,kabla sijasikia ya nani ntayafikiria?umemaliza mawazo kwa machache kuchangia ,unyooshe kijiko ya kuwa sukari yenyewe ni ndogo ya kurumangia ,mtamu usipungue kamwe nawe enedelea kunibembeleza,sipati raha lakini moyoni najisikia,nafsi yangu umeiweka angani mwezi na jua havijulikani


Saturday, June 2, 2012

GOOD WOOD...

Suppose then we saw a good tree, then we get rid timber to obtain the good,
 and not to believe this is where we will see, some wept some will laugh,
 but the tree and itself is kind of cut,
 others will use the machine in order to timber and their years of living increased
is because they spend less time too, time spent to make wooden machinery is limited and a lot of energy used is a machine,
for those who want to get the wood quality is to look at the wood they need,
 not because someone has a timber that some one has and I maybe,
without knowing why someone mold it and even when we parted how does it cost
It's a lot to consider

Not only do we see but when we need them,
 and needed nothing then be done with a goal of bringing quality,perfectly
anything shown  is visible in the minds of people, and when seen it seems difference for the future we are going to say he did this, or that..
if not known at  the beginning is to know why,
 with its more diversity comes to be addressed and the society where the gap there in strengthening or without popularized the profound ideas,
 best wood to accept that your tree was even better as well.
we will stand and heard a tree some you bear much fruit and offer beautiful wood,
 but wood that made to be thin is not recommended in nation-building, for those of all other used one very Little chance there again,
 Its to Battle.

A lot happens and other not be in our sides, when we became infiltration in a narrow space, 
we want hear whats on presence side,
know then you will be asked for your presence as it were also appeared,  
many boards seem to be eaten by insects,  
it will be tiredness for the community as they  begins to use those
We need a good conservation for timbers we posses
the nation will fall before its time, as its construction will be bad,
 without even a hearing seem

I thought of buying wooden rags at marketplace may not be a life.
for we look our trees has been great, here we can remove even the shadows,
 here we can remove even the nature
if we want only the beauty of the wood comes in the form of beginning

 .

'beautiful wood comes from the tree itself'.

Makaya's Forum: ELEWA 2

Makaya's Forum: ELEWA 2 :   Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye n...